< Mwanzo 29 >

1 Kisha Yakobo akaendelea na safari yake na akafika katika nchi ya watu wa mashariki.
Then Jacob [Supplanter] went on his journey, and came to the land of the children of the east.
2 Hata alipotazama, akaona kisima kondeni, na, tazama, makundi matatu ya kondoo yalikuwa yamelala kando yake. Kwani kutoka katika hicho wangeyanywesha makundi, na jiwe juu ya mdomo wa kisima lilikuwa kubwa.
He looked, and behold, a well in the field, and, behold, three flocks of sheep lying there by it. For out of that well they watered the flocks. The stone on the well’s mouth was large.
3 Wakati makundi yote yangekusanyika pale, wachungaji wangevingirisha jiwe kutoka katika mdomo wa kisima na kuwanywesha kondoo, na kisha kurudisha jiwe juu ya mdomo wa kisima, mahali pake.
There all the flocks were gathered. They rolled the stone from the well’s mouth, and watered the sheep, and put the stone again on the well’s mouth in its place.
4 Yakobo akawambia, “Ndugu zangu, ninyi mnatokea wapi?” nao wakasema, “Tunatoka Harani.”
Jacob [Supplanter] said to them, “My relatives, where are you from?” They said, “We are from Haran [Mountaineer].”
5 Akawambia, “Mnamfahamu Labani mwana wa Nahori?” Wakasema, “Tunamfahamu.”
He said to them, “Do you know Laban [White], the son of Nahor?” They said, “We know him.”
6 Akawambia, “Je hajambo?” Wakasema, “Hajambo, na, tazama pale, Raheli binti yake anakuja na kondoo.”
He said to them, “Is it well with him?” They said, “It is well. See, Rachel [Ewe sheep], his daughter, is coming with the sheep.”
7 Yakobo akasema, “Tazama, ni mchana. Siyo wakati wa kukusanya kondoo pamoja. Mnapaswa kuwanywesha kondoo na kisha mkaenda na kuwaacha wachunge.”
He said, “Behold, it is still the middle of the day, not time to gather the livestock together. Water the sheep, and go and feed them.”
8 Wakamwambia, “Hatuwezi kuwanywesha mpaka makundi yote yakusanyike pamoja. Ndipo wanaume watakapovingirisha jiwe kutoka mlangoni mwa kisima, na ndipo tutakapowanywesha kondoo.”
They said, “We can’t, until all the flocks are gathered together, and they roll the stone from the well’s mouth. Then we water the sheep.”
9 Wakati bado Yakobo anaongea nao, Raheli akaja pamoja na kondoo wa babaye, kwani alikuwa akiwachunga.
While he was yet speaking with them, Rachel [Ewe sheep] came with her father’s sheep, for she kept them.
10 Yakobo alipomwona Raheli, binti wa Labani, kaka wa mamaye, na kondoo wa Labani, kaka wa mama yake, Yakobo akaja juu, akalivingirisha jiwe kutoka mlangoni mwa kisima, na akawanywesha kondoo wa Labani, kaka wa mama yake.
When Jacob [Supplanter] saw Rachel [Ewe sheep] the daughter of Laban [White], his mother’s brother, and the sheep of Laban [White], his mother’s brother, Jacob [Supplanter] went near, and rolled the stone from the well’s mouth, and watered the flock of Laban [White] his mother’s brother.
11 Yakobo akambusu Raheli na akalia kwa sauti.
Jacob [Supplanter] kissed Rachel [Ewe sheep], and lifted up his voice, and wept.
12 Yakobo akamwambia Raheli kwamba alikuwa ni ndugu wa baba yake, na kwamba alikuwa mwana wa Rebeka. Kisha yeye akakimbia kumwambia baba yake.
Jacob [Supplanter] told Rachel [Ewe sheep] that he was her father’s brother, and that he was Rebekah [Securely bound]’s son. She ran and told her father.
13 Labani aliposikia habari kuhusu Yakobo mwana wa dada yake, akaenda kukutana naye, akamkumbatia, akambusu, na kumleta nyumbani kwake. Yakobo akamwambia Labani mambo haya yote.
When Laban [White] sh'ma ·heard obeyed· the news of Jacob [Supplanter], his sister’s son, he ran to meet Jacob [Supplanter], and embraced him, and kissed him, and brought him to his house. Jacob [Supplanter] told Laban [White] all these things.
14 Labani akamwambia, “Kwa hakika wewe ni mfupa wangu na nyama yangu.” Kisha Yakobo akakaa naye kama mwezi mmoja.
Laban [White] said to him, “Surely you are my bone and my flesh.” He lived with him for a month.
15 Kisha Labani akamwambia Yakobo, “Je unitumikie bure kwa kuwa wewe ni ndugu yangu? Niambie, ujira wako utakuwaje?
Laban [White] said to Jacob [Supplanter], “Because you are my brother, should you therefore serve me for nothing? Tell me, what will your wages be?”
16 Basi Labani alikuwa na binti wawili. Jina la mkubwa lilikuwa ni Lea, na jina la mdogo lilikuwa Raheli.
Laban [White] had two daughters. The name of the elder was Leah [Weary], and the name of the younger was Rachel [Ewe sheep].
17 Macho ya Lea yalikuwa dhaifu, lakini Raheli alikuwa mzuri wa umbo na mwonekano.
Leah [Weary]’s eyes were weak, but Rachel [Ewe sheep] was beautiful in form and attractive.
18 Yakobo alimpenda Raheli, hivyo akasema, “Nitakutumikia miaka saba kwa ajili ya Raheli, binti yako mdogo.”
Jacob [Supplanter] 'ahav ·affectionately loved· Rachel [Ewe sheep]. He said, “I will serve you seven years for Rachel [Ewe sheep], your younger daughter.”
19 Labani akasema, Itakuwa vema kukupa wewe, kuliko kumpa mtu mwingine. Kaa nami.”
Laban [White] said, “It is better that I give her to you, than that I should give her to another man. Stay with me.”
20 Hivyo Yakobo akamtumikia kwa miaka saba kwa ajili ya Raheli; nayo ilionekana kwake kama siku chache tu, kwa ajili ya upendo aliokuwa nao kwake.
Jacob [Supplanter] served seven years for Rachel [Ewe sheep]. They seemed to him but a few days, for the love he had for her.
21 Kisha Yakobo akamwambia Labani, “Nipe mke wangu, kwani siku zangu zimetimia - ili kwamba nimwoe!
Jacob [Supplanter] said to Laban [White], “Give me my wife, for my days are fulfilled, that I may go in to her.”
22 Hivyo Labani akawaalika watu wa mahali hapo na kuandaa sherehe.
Laban [White] gathered together all the men of the place, and made a feast.
23 Wakati wa jioni, Labani akamchukua Lea binti yake mkubwa na kumleta kwa Yakobo, aliyelala naye.
In the evening, he took Leah [Weary] his daughter, and brought her to him. He went in to her.
24 Labani akampa mtumishi wake wakike Zilpa kuwa mjakazi wa Lea.
Laban [White] gave Zilpah [Frailty] his servant to his daughter Leah [Weary] for a servant.
25 Ilipofika asubuhi, tazama, kumbe ni Lea! Yakobo akamwambia Labani, “Ni nini hiki ulichonifanyia? Je sikukutumikia kwa ajili ya Raheli? Kwa nini basi umenihadaa?
In the morning, behold, it was Leah [Weary]. He said to Laban [White], “What is this you have done to me? Didn’t I serve with you for Rachel [Ewe sheep]? Why then have you deceived me?”
26 Labani akamwambia, “Siyo utamaduni wetu kumtoa bindi mdogo kabla ya mzaliwa wa kwanza.
Laban [White] said, “It is not done so in our place, to give the younger before the firstborn.
27 Timiza juma la bibi arusi, na tutakupa yule mwingine pia kwa mbadala wa kunitumikia miaka mingine saba.”
Fulfill the week of this one, and we will give you the other also for the service which you will serve with me yet seven other years.”
28 Yakobo akafanya hivyo, na akatimiza juma la Lea. Kisha Labani akampa Raheli binti yake kuwa mke wake.
Jacob [Supplanter] did so, and fulfilled her week. He gave him Rachel [Ewe sheep] his daughter as wife.
29 Lakini pia Labani akampa Raheli binti yake Bilha, kuwa mjakazi wake.
Laban [White] gave to Rachel [Ewe sheep] his daughter Bilhah [Bashful], his servant, to be her servant.
30 Hivyo Yakobo akalala na Raheli, pia, lakini akampenda Raheli zaidi ya Lea. Hivyo Yakobo akamtumikia Labani kwa miaka saba mingine.
He went in also to Rachel [Ewe sheep], yet he 'ahav ·affectionately loved· Rachel [Ewe sheep] more than Leah [Weary]. Jacob [Supplanter] served Laban [White] yet seven other years.
31 Yahwe akaona kwamba Lea hakupendwa, hivyo akalifungua tumbo lake, lakini Raheli hakuwa na mtoto.
Adonai saw that Leah [Weary] was hated, and he opened her womb, but Rachel [Ewe sheep] was barren.
32 Lea akashika mimba na kuzaa mwana, naye akamwita Rubeni. Kwani alisema, “Kwa sababu Yahwe ameliangalia teso langu; bila shaka mme wangu sasa atanipenda.”
Leah [Weary] conceived, and bore a son, and she named him Reuben [See, a son!]. For she said, “Because Adonai has looked at my affliction. For now my husband will 'ahav ·affectionately love· me.”
33 Kisha akashika mimba tena na kuzaa mwana. Akasema, “Kwa sababu Yahwe amesikia kwamba sipendwi, kwa hiyo amenipa mwana mwingine,” na akamwita Simoni.
She conceived again, and bore a son, and said, “Because Adonai has sh'ma ·heard obeyed· that I am hated, he has therefore given me this son also.” She named him Simeon [Hearing].
34 Kisha akashika mimba tena na kuzaa mwana. Akasema, “Wakati huu mme wangu ataungana nami, kwa kuwa nimemzalia wana watatu.” Kwa hiyo akaitwa Lawi.
She conceived again, and bore a son. Said, “Now this time will my husband be joined to me, because I have borne him three sons.” Therefore his name was called Levi [United with].
35 Akashika mimba tena na kuzaa mwana. Akasema, “Wakati huu nitamsifu Yahwe.” Kwa hiyo akamwita jina lake Yuda; kisha akaacha kuzaa watoto.
She conceived again, and bore a son. She said, “This time will I yadah ·extend hands in thankful praise· to Adonai.” Therefore she named him Judah [Praised]. Then she stopped bearing.

< Mwanzo 29 >