< Mwanzo 28 >

1 Isaka akamwita Yakobo, akambariki, na kumwagiza, “Usichukuwe mwanamke katika wanawake wa Kikanaani.
Isaac [Laughter] called Jacob [Supplanter], blessed him, and enjoined him, “You shall not take a wife of the daughters of Canaan [Humbled].
2 Inuka, nenda Padani Aramu, katika nyumba ya Bethueli baba wa mama yako, na uchukue mwanamke pale, mmojawapo wa binti za Labani, kaka wa mama yako.
Arise, go to Paddan Aram [Elevated], to the house of Bethuel your mother’s father. Take a wife from there from the daughters of Laban [White], your mother’s brother.
3 Mungu Mwenyezi na akubariki, akupe uzao na akuzidishe, hata uwe wingi wa watu.
May El Shaddai [God Almighty] bless you, and make you fruitful, and multiply you, that you may be a company of peoples,
4 Na akupe baraka ya Ibrahimu, wewe, na uzao wako baada yako, kwamba uweze kumilki nchi ambapo umekuwa ukiishi, ambayo Mungu alimpa Ibrahimu.”
and give you the blessing of Abraham [Father of a multitude], to you, and to your offspring with you, that you may inherit the land where you travel, which God gave to Abraham [Father of a multitude].”
5 Hivyo Isaka akamwondoa Yakobo. Yakobo akaenda Padani Aramu, kwa Labani mwana wa Bethueli Mwaramu, kaka wa Rebeka, mama yao Yakobo na Esau.
Isaac [Laughter] sent Jacob [Supplanter] away. He went to Paddan Aram [Elevated] to Laban [White], son of Bethuel the Syrian, Rebekah [Securely bound]’s brother, Jacob [Supplanter]’s and Esau [Hairy]’s mother.
6 Basi Esau alipoona kwamba Isaka amembariki Yakobo na kumpeleka Padani Aramu, kuchukua mke kutoka pale. Lakini pia akaona kwamba Isaka alikuwa amembariki na kumwagiza, akisema, “Usichukue mke katika wanawake wa Kanaani.”
Now Esau [Hairy] saw that Isaac [Laughter] had blessed Jacob [Supplanter] and sent him away to Paddan Aram [Elevated], to take him a wife from there, and as he blessed him, Issac [Laughter] enjoined these words to Esau [Hairy], saying, “You shall not take a wife of the daughters of Canaan [Humbled],”
7 Esau pia akaona kwamba Yakobo alikuwa amemtii baba yake na mama yake, na alikuwa amekwenda Padani Aramu.
and that Jacob [Supplanter] sh'ma ·heard obeyed· his father and his mother, and was gone to Paddan Aram [Elevated].
8 Esau akaona kwamba wanawake wa Kanaani hawakumpendeza Isaka baba yake.
Esau [Hairy] saw that the daughters of Canaan [Humbled] didn’t please Isaac [Laughter], his father.
9 Hivyo akaenda kwa Ishmaeli, na kuchukua, mbali na wake aliokuwa nao, Mahalathi binti Ishmaeli, mwana wa Ibrahimu, dada wa Nebayothi, kuwa mke wake.
Esau [Hairy] went to Ishmael [Pays attention God], and took, besides the wives that he had, Mahalath the daughter of Ishmael [Pays attention God], Abraham [Father of a multitude]’s son, the sister of Nebaioth, to be his wife.
10 Yakobo akatoka Beersheba na akaelekea Harani.
Jacob [Supplanter] went out from Be'er-Sheva [Well of Seven, Well of an Oath], and went toward Haran [Mountaineer].
11 Akaja mahali fulani na akakaa pale usiku kucha, kwa kuwa jua lilikuwa limekuchwa. Akachukua mojawapo ya mawe katika eneo hilo, akaliweka chini ya kichwa chake, na akalala usingizi katika eneo hilo.
He came to a certain place, and stayed there all night, because the sun had set. He took one of the stones of the place, and put it under his head, and lay down in that place to sleep.
12 Akaota na kuona ngazi imewekwa juu ya nchi. Ncha yake ilifika hata mbinguni na malaika wa Mungu walikuwa wakishuka na kupanda juu yake.
He dreamed. Behold, a stairway set upon the earth, and its top reached to heaven. Behold, the angels of God ascending and descending on it.
13 Tazama, Yahwe amesimama juu yake na kusema, “Mimi ni Yahwe, Mungu wa Ibrahimu baba yako, na Mungu wa Isaka. Nchi uliyolala juu yake, nitakupa wewe na uzao wako.
Behold, Adonai stood above it, and said, “I am Adonai, the God of Abraham [Father of a multitude] your father, and the God of Isaac [Laughter]. The land whereon you lie, to you will I give it, and to your offspring.
14 Uzao wako utakuwa kama mavumbi ya ardhi, na utaenea mbali kuelekea magharibi, mashariki, kaskazini, na kusini. Kupitia kwako na kupitia uzao wako familia zote za dunia zitabarikiwa.
Your offspring will be as the dust of the earth, and you will spread abroad to the west, and to the east, and to the north, and to the south. In you and in your offspring will all the families of the earth be blessed.
15 Tazama, mimi nipo nawe, na nitakulinda kila uendako, Nitakurudisha katika nchi hii tena; kwani sitakuacha. Nitafanya kila nililokuahidi.”
Behold, I am with you, and will keep you, wherever you go, and will bring you again into this land. For I will not leave you, until I have done that which I have spoken of to you.”
16 Yakobo akaamka katika usingizi, na akasema, “Hakika Yahwe yupo mahali hapa, sikujua hili.”
Jacob [Supplanter] awakened out of his sleep, and he said, “Surely Adonai is in this place, and I didn’t know it.”
17 Akaogopa na kusema, “Eneo hili linatisha kama nini! Hili sio kingine zaidi ya nyumba ya Mungu. Hili ni lango la mbinguni.”
He was afraid, and said, “How dreadful is this place! This is none other than God’s house, and this is the gate of heaven.”
18 Yakobo akaamka mapema asubuhi na akachukua jiwe alilokuwa ameliweka chini ya kichwa chake. Akaliweka kama nguzo na kumimina mafuta juu yake.
Jacob [Supplanter] rose up early in the morning, and took the stone that he had put under his head, and set it up for a pillar, and poured oil on its top.
19 Akapaita pale Betheli, lakini jina la kawaida la mji lilikuwa Luzu.
He called the name of that place Beth-el [House of God], but the name of the city was Luz at the first.
20 Yakobo akatoa nadhiri, kusema, “Ikiwa Mungu atakuwa nami na atanilinda katika njia nipitayo, na atanipa mkate wa kula, na mavazi ya kuvaa,
Jacob [Supplanter] vowed a vow, saying, “If God will be with me, and will keep me in this way that I go, and will give me bread to eat, and clothing to put on,
21 hata nikarudi salama katika nyumba ya baba yangu, ndipo Yahwe atakapokuwa Mungu wangu.
so that I come again to my father’s house in peace, and Adonai will be my God,
22 Kisha jiwe hili nililoliweka kama nguzo litakuwa jiwe takatifu. Kutoka katika kila utakachonipa, kwa hakika nitakupa tena sehemu ya kumi.”
then this stone, which I have set up for a pillar, will be God’s house. Of all that you will give me I will surely give a tenth to you.”

< Mwanzo 28 >