< Mwanzo 21 >

1 Yahwe akamsikiliza Sara kwa umakini kama alivyo kuwa amemwambia, Yahwe akamfanyia Sara kama alivyo kuwa amemwahidi.
Adonai visited Sarah [Princess] as he had said, and Adonai did to Sarah [Princess] as he had spoken.
2 Sara akachukua mimba na akamzalia Abraham mtoto wa kiume katika uzee wake, katika muda ule ule ambao Mungu alikuwa amemwambia.
Sarah [Princess] conceived, and bore Abraham [Father of a multitude] a son in his old age, at the set time of which God had spoken to him.
3 Abraham akamwita jina mwanawe, ambaye alizaliwa kwake, na Sara, Isaka.
Abraham [Father of a multitude] called his son who was born to him, whom Sarah [Princess] bore to him, Isaac [Laughter].
4 Abraham akamtahiri mwanawe Isaka alipofikisha siku nane, kama vile Mungu alivyokuwa amemwagiza.
Abraham [Father of a multitude] circumcised his son, Isaac [Laughter], when he was eight days old, as God had enjoined him.
5 Abraham alikuwa na umri wa miaka mia moja wakati mwanawe Isaka anazaliwa kwake.
Abraham [Father of a multitude] was one hundred years old when his son, Isaac [Laughter], was born to him.
6 Sara akasema, “Mungu amenifanya nicheke; kila mtu atakaye sikia atacheka pamoja na nami.”
Sarah [Princess] said, “God has made me laugh. Everyone who sh'ma ·hears obeys· will laugh with me.”
7 Pia akasema, “Nani angesema kwa Abraham kwamba Sara atalea mtoto, na sasa kweli nimemzalia mtoto wakiume katika uzee wake!”
She said, “Who would have said to Abraham [Father of a multitude], that Sarah [Princess] would nurse children? For I have borne him a son in his old age.”
8 Mtoto akakua na akaachishwa kunyonya, na Abraham akafanya sherehe kubwa katika siku ambayo Isaka aliachishwa.
The child grew, and was cameled. Abraham [Father of a multitude] made a great feast on the day that Isaac [Laughter] was cameled.
9 Sara akamwona mwana wa Hajiri Mmisri, ambaye alikuwa amezaliwa kwa Abraham, akidhihaki.
Sarah [Princess] saw the son of Hagar [Flight] the Egyptian [person from Abode of slavery], whom she had borne to Abraham [Father of a multitude], metzahek ·lewd and irreverent jokes·.
10 Kwa hiyo akamwambia Abraham, “Mfukuze huyu mwanamke huyu mtumwa pamoja na mtoto wake: kwa kuwa mtoto huyu wa mwanamke mtumwa hawezi kuwa mrithi pamoja na mwanangu Isaka.”
Therefore she said to Abraham [Father of a multitude], “Divorce and cast out this servant and her son! For the son of this servant will not be heir with my son, Isaac [Laughter].”
11 Jambo hili likamuhuzunisha sana Abraham kwa sababu ya mwanawe.
The thing was very grievous in Abraham [Father of a multitude]’s sight on account of his son.
12 Lakini Mungu akamwambia Abraham, “Usihuzunike kwa sababu ya kijana huyu, na kwa sababu ya mwanamke huyu mtumwa wako. Sikiliza maneno asemayo Sara juu ya jambo hili, kwa sababu itakuwa kupitia Isaka kwamba uzao wako utaitwa.
God said to Abraham [Father of a multitude], “Don’t let it be grievous in your sight because of the boy, and because of your servant. In all that Sarah [Princess] says to you, sh'ma ·hear obey· her voice. For your offspring will be accounted as from Isaac [Laughter].
13 Nitamfanya pia mtoto wa mjakazi kuwa taifa, kwa sababu ni uzao wako.”
I will also make a nation of the son of the servant, because he is your child.”
14 Abraham akaamka asubuhi na mapema, akachukua mkate na kiriba cha maji, akampatia Hajiri, akiweka juu ya bega lake. Akamtoa kijana akampatia Hajiri na akawaondoa. Hajiri akaondoka akapotea katika jangwa la Beerisheba.
Abraham [Father of a multitude] rose up early in the morning, and took bread and a bottle of water, and gave it to Hagar [Flight], putting it on her shoulder; and gave her the child, and sent her away. She departed, and wandered in the wilderness of Be'er-Sheva [Well of Seven, Well of an Oath].
15 Maji yalipokwisha kwenye kiriba akamtelekeza kijana katika moja ya vichaka.
The water in the bottle was spent, and she cast the child under one of the shrubs.
16 Kisha akaondoka, na akakaa umbali kidogo na yule kijana, umbali kama wa kutupa mshale, kwa vile alisema, “Na nisitazame kifo cha mtoto.” Alipokuwa amekaa kumkabili, akapaza sauti yake akalia.
She went and sat down opposite him, a good way off, about a bow shot away. For she said, “Don’t let me see the death of the child.” She sat over against him, and lifted up her voice, and wept.
17 Mungu akasikia kilio cha kijana, na malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, “Nini kinakusumbua? Usiogope, kwa kuwa Mungu amesikia kilio cha kijana mahali alipo.
God sh'ma ·heard obeyed· the voice of the boy. Ha mal'ak Elohim [The Angel of God] called to Hagar [Flight] out of the sky, and said to her, “What ails you, Hagar [Flight]? Don’t be afraid. For God has sh'ma ·hear obey· the voice of the boy where he is.
18 Inuka msimamishe mtoto, na umtie moyo; kwa kuwa nitamfanya kuwa taifa kubwa.”
Get up, lift up the boy, and hold him in your hand. For I will make him a great nation.”
19 Kisha Mungu akayafunua macho ya Hajiri, natazama akaona kisima cha maji. Akaenda akajaza kiriba maji, na akampatia kijana akanywa.
God opened her eyes, and she saw a well of water. She went, filled the bottle with water, and gave the boy drink.
20 Mungu akawa pamoja na kijana, na akakua. Akaishi jangwani akawa mwindaji.
God was with the boy, and he grew. He lived in the wilderness, and became, as he grew up, an archer.
21 Akaishi katka jangwa la Parani, na mama yake akampatia mke kutoka Misri.
He lived in the wilderness of Paran. His mother took a wife for him out of the land of Egypt [Abode of slavery].
22 Ikawa kwamba katika wakati ule Abimeleki na Fikoli kamanda wa jeshi lake akamwambia Abraham, akisema, “Mungu yuko pamoja na wewe katika yote uyatendayo.
At that time, Abimelech [My father king] and Phicol the captain of his army spoke to Abraham [Father of a multitude], saying, “God is with you in all that you do.
23 Sasa niapie kwa Mungu kwamba hutanifanyia baya, wala mwanangu, wala uzao wangu. Onesha kwangu na kwa nchi ambayo umekuwa ukikaa agano lile lile la uaminifu ambalo nimekuonesha wewe.”
Now, therefore, swear to me here by God that you will not deal falsely with me, nor with my son, nor with my son’s son. But according to the cheshed ·loving-kindness· that I have done to you, you shall do to me, and to the land in which you have lived as a foreigner.”
24 Abraham akasema, “Nina apa.”
Abraham [Father of a multitude] said, “I will swear.”
25 Abraham pia akamlalamikia Abimeleki kuhusu kisima cha maji ambacho watumishi wa Abimeleki wamekinyang'anya.
Abraham [Father of a multitude] complained to Abimelech [My father king] because of a water well, which Abimelech [My father king]’s servants had violently taken away.
26 Abimeleki akasema, “Sijui ni nani amefanya jambo hili. Hukuniambia mapema; na sijalisikia ila leo hii.”
Abimelech [My father king] said, “I don’t know who has done this thing. You didn’t tell me, and I didn’t sh'ma ·heard obeyed· of it until today.”
27 Kwa hiyo Abraham akachukua kondoo na ng'ombe maksai akampatia Abimeleki, na wawili hawa wakafanya agano.
Abraham [Father of a multitude] took sheep and cattle, and gave them to Abimelech [My father king]. Those two made a covenant ·binding contract between two or more parties·.
28 Kisha Abraham akatenga wanakondoo wa kike saba pekeyao.
Abraham [Father of a multitude] set seven ewe lambs of the flock by themselves.
29 Abimeleki akamwambia Abraham, “Nini maana ya hawa wanakondoo wa kike saba ambao umewatenga pekeyao?”
Abimelech [My father king] said to Abraham [Father of a multitude], “What do these seven ewe lambs which you have set by themselves mean?”
30 Akajibu, “Hawa wanakondoo wa kike saba utawapokea kutoka mkonono mwangu, ili kwamba uwe ushahidi kwangu, kuwa nichimba kisima hiki.”
He said, “You shall take these seven ewe lambs from my hand, that it may be a witness to me, that I have dug this well.”
31 Kwa hiyo akaita mahali pale Beerisheba, kwa sababu mahali pale wote wawili wali apa kiapo.
Therefore he called that place Be'er-Sheva [Well of Seven, Well of an Oath], because they both swore there.
32 Walifanya agano hapo Bersheba, kisha Abimeleki na Fikoli, amiri wa jeshi, wakarudi katika nchi ya Wafilisti.
So they made a covenant at Be'er-Sheva [Well of Seven, Well of an Oath]. Abimelech [My father king] rose up with Phicol, the captain of his army, and they returned into the land of the Philistines [To roll in dust (As an insult)].
33 Abraham akapanda mti wa mkwaju katika Beerisheba. Na pale akamwabudu Yahwe, Mungu wa milele.
Abraham [Father of a multitude] planted a tamarisk tree in Be'er-Sheva [Well of Seven, Well of an Oath], and called there on the name of Adonai, the El 'Olam [God Everlasting].
34 Abraham akasalia kuwa mgeni katika nchi ya Wafilisti kwa siku nyingi.
Abraham [Father of a multitude] lived as a foreigner in the land of the Philistines [To roll in dust (As an insult)] many days.

< Mwanzo 21 >