< Mwanzo 20 >

1 Abraham akasafiri kutoka pale hadi nchi ya Negebu, na akakaa kati ya Kadeshi na Shuri. Akawa mgeni akiishi Gerari.
Abraham [Father of a multitude] traveled from there toward the land of the South, and lived between Kadesh and Shur. He lived as a foreigner in Gerar.
2 Abraham akasema kususu mkewe Sara, “ni dada yangu.” Kwa hiyo Abimeleki mfalme wa Gerari akatuma watu wake kumchukua Sara.
Abraham [Father of a multitude] said about Sarah [Princess] his wife, “She is my sister.” Abimelech [My father king] king of Gerar sent, and took Sarah [Princess].
3 Lakini Mungu akamtokea Abimeleki usiku katika ndoto, akamwambia, “Tazama, wewe ni mfu kutokana na mwanamke uliye mchukua, kwa kuwa ni mke wa mtu.”
But God came to Abimelech [My father king] in a dream of the night, and said to him, “Behold, you are a dead man, because of the woman whom you have taken. For she is a man’s wife.”
4 Basi Abimeleki alikuwa bado hajamkaribia hivyo akasema, “Bwana, Je utaua hata taifa lenye haki?
Now Abimelech [My father king] had not come near her. He said, “Lord, will you kill even a upright nation?
5 Je si yeye mwenyewe aliye niambia, 'Sara ni dada yangu?' Hata Sara mwenyewe alisema, 'ni kaka yangu.' Nimefanya hili katika uadilifu wa moyo wangu na katika mikono isiyo na hatia.”
Didn’t he tell me, ‘She is my sister?’ She, even she herself, said, ‘He is my brother.’ In the integrity of my heart and the innocence of my hands have I done this.”
6 Kisha Mungu akasema naye katika ndoto, “Kweli, ninajua pia kwamba umefanya hili katika uadilifu wa moyo wako, na pia nilikuzuia usitende dhambi dhidi yangu mimi. Ndiyo maana sikuruhusu umshike.
God said to him in the dream, “Yes, I know that in the integrity of your heart you have done this, and I also withheld you from sinning against me. Therefore I didn’t allow you to touch her.
7 Kwa hiyo, mrudishe huyo mke wa mtu, kwa kuwa ni nabii. Atakuombea, na utaishi. Lakini usipo mrudisha, ujuwe kwamba wewe pamoja na wote walio wa kwako mtakufa hakika.
Now therefore, restore the man’s wife. For he is a prophet, and he will pray for you, and you will live. If you don’t restore her, know for sure that you will die, you, and all who are yours.”
8 Abimeleki akaamka asubuhi na mapema akawaita watumishi wake wote waje kwake. Akawasimulia mambo haya yote, na watu wale wakaogopa sana.
Abimelech [My father king] rose early in the morning, and called all his servants, and told all these things in their ear. The men were very scared.
9 Kisha Abimeleki akamwita Abraham na kumwambia, “Umetufanyia jambo gani? Ni kwa jinsi gani nimekutenda dhambi kwamba umeniletea mimi na ufalme wangu dhambi hii kubwa? Umenifanyia mimi jambo ambalo halipaswi kufanywa.”
Then Abimelech [My father king] called Abraham [Father of a multitude], and said to him, “What have you done to us? How have I sinned against you, that you have brought on me and on my kingdom a great sin? You have done deeds to me that ought not to be done!”
10 Abimeleki akamwambia Abraham, “Nini kilikushawishi wewe kutenda jambo hili?”
Abimelech [My father king] said to Abraham [Father of a multitude], “What did you see, that you have done this thing?”
11 Abraham akasema, “Ni kwasababu nilifikiri hakika hakuna hofu ya Mungu katika sehemu hii, na kwamba wataniua kwa ajili ya mke wangu.'
Abraham [Father of a multitude] said, “Because I thought, ‘Surely the fear of God is not in this place. They will kill me for my wife’s sake.’
12 Licha ya kwamba kweli ni dada yangu, binti wa baba yangu, ingawa si binti wa mama yangu; na ndiye alifanyika kuwa mke wangu.
Besides, she is indeed my sister, the daughter of my father, but not the daughter of my mother; and she became my wife.
13 Wakati Mungu aliponiondoa katika nyumba ya baba yangu na kusafiri kutoka mahali kwenda mahali pengine, nilimwambia mke wangu, kwa kila sehemu tutakayo kwenda, unioneshe uaminifu wako kama mke wangu: Kila mahali tutakapo kwenda, useme juu yangu kuwa, “Ni kaka yangu.”'''
When God caused me to wander from my father’s house, I said to her, ‘This is your cheshed ·loving-kindness· which you shall show to me. Everywhere that we go, say of me, “He is my brother.”’”
14 Ndipo Abimeleki akatwaa kondoo, maksai, watumwa wa kiume na wa kike akampatia Abraham. Basi Abimeleki akamrudisha Sara, mke wa Abraham.
Abimelech [My father king] took sheep and cattle, male servants and female servants, and gave them to Abraham [Father of a multitude], and restored Sarah [Princess], his wife, to him.
15 Abimeleki akasema, Tazama, Nchi yangu i mbele yako. Kaa mahali utakapopendezewa.”
Abimelech [My father king] said, “Behold, my land is before you. Dwell where it pleases you.”
16 Na kwa Sara akasema, Tazama, nimempatia kaka yako vipande elfu vya fedha. Navyo ni kwa ajili ya kufunika kosa lolote dhidi yako machoni pa wote walio pamoja na wewe, na mbele ya kila mtu ambaye umemfanya kuwa na haki.”
To Sarah [Princess] he said, “Behold, I have given your brother a thousand pieces of silver. Behold, it is for you a covering of the eyes to all that are with you. In front of all you are vindicated.”
17 Kisha Abraham akaomba kwa Mungu, Na Mungu akamponya Abimeleki, mkewe, na watumwa wake wa kike kiasi kwamba wakaweza kupata watoto.
Abraham [Father of a multitude] prayed to God. God healed Abimelech [My father king], and his wife, and his female servants, and they bore children.
18 Kwa kuwa Yahwe alikuwa amewafanya wanawake wote wa nyumaba ya Abimeleki kuwa tasa kabisa, kwa sababu ya Sara, mke wa Abraham.
For Adonai had closed up tight all the wombs of the house of Abimelech [My father king], because of Sarah [Princess], Abraham [Father of a multitude]’s wife.

< Mwanzo 20 >