< Wagalatia 1 >

1 Mimi ni Paulo mtume. Mimi sio mtume kutoka kwa wanadamu wala kupitia kwa mwanadamu, lakini kupitia kwa Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua kutoka kwa wafu.
Paul, apôtre, non de la part des hommes et par les hommes, mais par Jésus-Christ et Dieu le Père, qui l'a ressuscité des morts,
2 Pamoja na ndugu wote na mimi, ninayaandikia makanisa ya Galatia.
et tous les frères qui sont avec moi, aux assemblées de la Galatie.
3 Neema iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo,
Que la grâce et la paix vous soient données par Dieu le Père et par notre Seigneur Jésus-Christ,
4 aliyejitoa mwenyewe kwa ajili ya dhambi zetu ili kwamba atukomboe na nyakati hizi za uovu, kutokana na mapenzi ya Mungu wetu na Baba. (aiōn g165)
qui s'est livré lui-même pour nos péchés, afin de nous délivrer du présent siècle mauvais, selon la volonté de notre Dieu et Père, (aiōn g165)
5 Kwake uwe utukufu milele na milele. (aiōn g165)
à qui soit la gloire aux siècles des siècles. Amen. (aiōn g165)
6 Ninashangaa kwamba mnageukia haraka kwenye injili nyingine. Ninashangaa kwamba mnageukia mbali kutoka kwake yeye aliyewaita kwa neema ya Kristo.
Je m'étonne que vous abandonniez si vite celui qui vous a appelés dans la grâce de Christ pour une autre « bonne nouvelle »,
7 Hakuna injili nyingine, lakini kuna baadhi ya watu wanao wasababishieni nyinyi matatizo na kutaka kubadilisha injili ya Kristo.
mais il n'y a pas d'autre « bonne nouvelle ». Seulement, il y a des gens qui vous troublent et qui veulent pervertir la Bonne Nouvelle du Christ.
8 Lakini hata kama ni sisi au malaika kutoka mbinguni atatangaza kwenu injili tofauti na ile tuliyoitangaza kwenu, na alaaniwe.
Mais si nous-mêmes, ou un ange du ciel, vous annonçons une autre « bonne nouvelle » que celle que nous vous avons annoncée, qu'il soit maudit.
9 Kama tulivyo sema mwanzoni, na sasa nasema tena, “Kama kuna mtu atawatangazia kwenu injili tofauti na mliyoipokea, na alaaniwe.”
Ce que nous avons déjà dit, je le répète maintenant: si quelqu'un vous annonce une autre « bonne nouvelle » que celle que vous avez reçue, qu'il soit maudit.
10 Kwani sasa hivi ninatafuta uthibitisho wa watu au Mungu? Ninatafuta kuwafurahisha wanadamu? Kama ninaendelea kujaribu kuwafurahisha wanadamu, mimi sio mtumishi wa Kristo.
Car est-ce que je cherche maintenant la faveur des hommes, ou celle de Dieu? Ou bien est-ce que je cherche à plaire aux hommes? Car si je cherchais encore à plaire aux hommes, je ne serais pas un serviteur du Christ.
11 Ndugu, ninataka ninyi mjue kwamba injili niliyoitangaza haitokani na wanadamu.
Mais je vous fais savoir, frères, au sujet de la Bonne Nouvelle qui a été prêchée par moi, qu'elle n'est pas selon l'homme.
12 Sikuipokea kutoka kwa mtu, wala sikufundishwa. Badala yake, ilikuwa ni kwa ufunuo wa Yesu Kristo kwangu.
Car je ne l'ai pas reçue d'un homme, et on ne me l'a pas enseignée, mais elle m'est venue par révélation de Jésus-Christ.
13 Mmekwisha sikia juu ya maisha yangu ya nyuma katika dini ya Kiyahudi, jinsi nilivyokuwa nikilitesa kwa ukali kanisa la Mungu zaidi ya kipimo na kuliteketeza.
Car vous avez appris comment j'ai vécu autrefois dans la religion des Juifs, et comment j'ai persécuté l'assemblée de Dieu et l'ai ravagée.
14 Nilikuwa nimeendelea katika Dini ya Kiyahudi zaidi ya ndugu zangu wengi Wayahudi. Nilikuwa na bidii sana katika tamaduni za baba zangu.
J'étais plus avancé dans la religion juive que beaucoup de mes compatriotes de mon âge, étant plus zélé pour les traditions de mes pères.
15 Lakini Mungu alipendezwa kunichagua mimi kutoka tumboni mwa mama. Aliniita mimi kupitia neema yake
Mais lorsque Dieu, qui m'a séparé du sein de ma mère et m'a appelé par sa grâce, eut le bon plaisir
16 kumdhihirisha Mwanawe ndani yangu, ili kwamba nimtangaze yeye miongoni mwa watu wa mataifa. Wala sikutafuta ushauri wa mwili na damu
de révéler son Fils en moi, afin que je l'annonce parmi les païens, je ne me suis pas immédiatement entretenu avec la chair et le sang,
17 na sikupanda kwenda Yerusalem kwa wale waliokuwa mitume kabla yangu. Badala yake nilienda Uarabuni na baadae kurudi Damesiki.
et je ne suis pas monté à Jérusalem auprès de ceux qui ont été apôtres avant moi, mais je suis parti en Arabie. Puis je suis retourné à Damas.
18 Kisha baada ya miaka mitatu nilipanda kwenda Yerusalemu kumtembelea Kefa, nikakaa naye kwa siku kumi na tano.
Puis, au bout de trois ans, je montai à Jérusalem pour visiter Pierre, et je restai avec lui quinze jours.
19 Lakini sikuona mitume wengine isipokuwa Yakobo, ndungu yake na Bwana.
Mais des autres apôtres, je n'ai vu que Jacques, le frère du Seigneur.
20 Tazama, mbele za Mungu, sidanganyi kwa kile niandikacho kwenu.
Or, pour ce qui est des choses que je vous écris, voici que, devant Dieu, je ne mens pas.
21 Kisha nilikwenda mikoa ya Shamu na Kilikia.
Puis je suis arrivé dans les régions de Syrie et de Cilicie.
22 Sikuwa najulikana kwa macho kwa makanisa ya Uyahudi yale yaliyokuwa katika Kristo,
J'étais encore inconnu de visage aux assemblées de Judée qui étaient en Christ,
23 lakini walikuwa wakisikia tu, “Yeye aliyekuwa akitutesa sasa anatangaza imani aliyokuwa akiiharibu.”
mais elles entendaient seulement dire: « Celui qui nous persécutait autrefois prêche maintenant la foi qu'il s'efforçait autrefois de détruire. »
24 Walikuwa wakimtukuza Mungu kwa ajili yangu.
Ils ont donc glorifié Dieu en moi.

< Wagalatia 1 >