< Ezekieli 45 >

1 Wakati mtakapogawanya nchi kama urithi, mtafanya sadakwa kwa Yahwe; sadaka hiyo itakuwa sehemu takatifu ya nchi, dhiraa elfu ishirini na tano urefu, na dhiraa elfu kumi upana. Patakuwa patakatifu, ndani ya mipaka yake yote.
“‘“Moreover, when you divide by lot the land for inheritance, you shall offer an offering to Yahweh, a holy portion of the land. The length shall be the length of twenty-five thousand reeds, and the width shall be ten thousand. It shall be holy in all its border all around.
2 Kutoka hapa kutakuwa na dhiraa mia tano kwa dhiraa mia tano za mraba kuzunguka mahali patakatifu, kwa kuuzunguka mpaka dhiraa hamsini upana.
Of this there shall be a five hundred by five hundred square for the holy place, and fifty cubits for its pasture lands all around.
3 Kutoka hili eneo utapima fungu ambalo ni dhiraa elfu ishirini na tano urefu na elfu kumi upana; patakuwa patakatifu; mahali patakatifu palipo tukuka.
Of this measure you shall measure a length of twenty-five thousand, and a width of ten thousand. In it shall be the sanctuary, which is most holy.
4 Patakuwa patakatifu katika nchi kwa ajili ya makuhani wanaomtumikia Yahwe, ajaye kwa Yahwe kumtumikia. Patakuwa mahali kwa ajili ya nyumba na eneo takatifu kwa ajili mahali patakatifu.
It is a holy portion of the land; it shall be for the priests, the ministers of the sanctuary, who come near to minister to Yahweh. It shall be a place for their houses and a holy place for the sanctuary.
5 Hivyo itakuwa dhiraa elfu ishirini na tano urefu na elfu kumi upana, patakuwa kwa ajili ya miji ya Walawi wanaotumika kwenye nyumba.
Twenty-five thousand cubits in length and ten thousand in width shall be for the Levites, the ministers of the house, as a possession for themselves, for twenty rooms.
6 Mtadhihirisha eneo moja kwa ajili ya mji, dhiraa elfu tano na urefu ishirini na tano, hapo patakuwa kando kando ya eneo lililohifadhiwa kwa ajili ya mahali patakatifu; huu mji utakuwa wa mali ya nyumba yote ya Israeli.
“‘“You shall appoint the possession of the city five thousand cubits wide and twenty-five thousand long, side by side with the offering of the holy portion. It shall be for the whole house of Israel.
7 Nchi ya mwana mfalme itakuwa kwa pande zote za eneo lililohifadhiwa kwa ajili ya mahali patakatifu na mji. Patakuwa kwa upande wao wa magaharibi na upande wa mashariki. Urefu utalingana na urefu wa moja ya hayo mafungu, kutoka magaribi hata mashariki.
“‘“What is for the prince shall be on the one side and on the other side of the holy allotment and of the possession of the city, in front of the holy allotment and in front of the possession of the city, on the west side westward, and on the east side eastward, and in length corresponding to one of the portions, from the west border to the east border.
8 Hii nchi itakuwa mali ya mwana mfalme katika Isaraeli. Wana wafalme hawatawakandamiza watu wangu; badala yake, watawapatia nchi kwa nyumba ya Israeli, kwa ajili ya makabila yao.
In the land it shall be to him for a possession in Israel. My princes shall no more oppress my people, but they shall give the land to the house of Israel according to their tribes.”
9 Bwana Yahwe asema hivi: Inatosha kwa ajili yenu, mwana mfalme wa Israeli! Ondoa dhuluma na mgogoro; fanya hukumu na haki! Usiwafukuze wapangaji wa watu wangu! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
“‘The Lord Yahweh says: “Enough you, princes of Israel! Remove violence and plunder, and execute justice and righteousness! Stop dispossessing my people!” says the Lord Yahweh.
10 Mtakuwa na mzani sahihi, efa sahihi, na bathi sahihi!
“You shall have just balances, a just ephah, and a just bath.
11 Efa na bathi zitakuwa kiasi kile kile, ili kwamba bathi iwe zaka ya homeri; efa itakuwa zaka ya hamori moja. Vipimo vyao vitakuwa vinafanana na homeri.
The ephah and the bath shall be of one measure, that the bath may contain one tenth of a homer, and the ephah one tenth of a homer. Its measure shall be the same as the homer.
12 Shekeli zitakuwa gera ishirini, shekeli sita zitakuwa mane yenu.
The shekel shall be twenty gerahs. Twenty shekels plus twenty-five shekels plus fifteen shekels shall be your mina.
13 Hili ndilo toleo mtakalotoa: efa sita kwa kila homeri ya ngano, na mtatoa efa sita kwa kila homeri ya shayiri.
“‘“This is the offering that you shall offer: the sixth part of an ephah from a homer of wheat, and you shall give the sixth part of an ephah from a homer of barley,
14 Sadaka ya kawaida ya mafuta itakuwa zaka ya bathi kwa kila kori (ambazo ni bathi), au kwa kila hamori, kwa kuwa hamori moja ni bathi kumi pia.
and the set portion of oil, of the bath of oil, one tenth of a bath out of the cor, which is ten baths, even a homer (for ten baths are a homer),
15 Kondoo mmoja au mbuzi kutoka mifugo kwa kila wanyama mia mbili kutoka malisho ya maji ya mikoa ya Israeli yatatumika kwa sadaka ya kuteketezwa yoyote au sadaka ya amani kufanya upatanisho kwa ajili ya watu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
and one lamb of the flock out of two hundred, from the well-watered pastures of Israel—for a meal offering, for a burnt offering, and for peace offerings, to make atonement for them,” says the Lord Yahweh.
16 Watu wote wa nchi watatoa hii sadaka kwa mwana mfalme wa Israeli.
“All the people of the land shall give to this offering for the prince in Israel.
17 Utakuwa wajibu wa mwana mfalme kutoa wanyama kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, sadaka ya unga, sadaka ya kinywaji, katika siku za sikukuu na sherehe za mwezi mpya, na katika siku za Sabato-sikukuu zote za kudumu za nyumba ya Israeli. Ataandaa kwa ajili ya sadaka za dhambi, sadaka za unga, sadaka za kuteketezwa, na sadaka za amani kwa ajili ya upatanisho badala ya nyumba ya Israeli.
It shall be the prince’s part to give the burnt offerings, the meal offerings, and the drink offerings, in the feasts, and on the new moons, and on the Sabbaths, in all the appointed feasts of the house of Israel. He shall prepare the sin offering, the meal offering, the burnt offering, and the peace offerings, to make atonement for the house of Israel.”
18 Bwana Yahwe asema hivi: Katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi, utachukua ng'ombe mmoja asiyekuwa na dosari kutoka kwenye kundi na kufanya sadaka ya dhambi kwa ajili ya patakatifu.
“‘The Lord Yahweh says: “In the first month, on the first day of the month, you shall take a young bull without defect, and you shall cleanse the sanctuary.
19 Kuhani atachukua baadhi ya damu ya sadaka ya dhambi na kuiweka juu ya miimo ya mlango na kwenye pembe nne za mpaka wa madhabahu, na miimo ya lango la uzio wa ndani.
The priest shall take of the blood of the sin offering and put it on the door posts of the house, and on the four corners of the ledge of the altar, and on the posts of the gate of the inner court.
20 Utafanya hivyo siku ya saba ya mwezi kwa dhambi ya kila mtu kwa ajali au ujinga; katika njia hii mtaipatanisha hekalu.
So you shall do on the seventh day of the month for everyone who errs, and for him who is simple. So you shall make atonement for the house.
21 Katika siku ya mwezi siku ya kumi na nne ya mwezi, mtakuwa na sikukuu, sikukuu ya siku saba. Matakula makate usiotiwa chachu.
“‘“In the first month, on the fourteenth day of the month, you shall have the Passover, a feast of seven days; unleavened bread shall be eaten.
22 Siku hiyo, mwana mfalme ataandaa ng'ombe kwa ajili yake na kwa ajili ya watu wote wa nchi kama sadaka ya dhambi.
On that day the prince shall prepare for himself and for all the people of the land a bull for a sin offering.
23 Kwa siku saba za sikukuu, mwana wa mfalme ataandaa sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya Yahwe: ng'ombe saba na kondoo dume saba zisizokuwa na dosari kila siku kwa mda wa siku saba, na mbuzi dume kila siku kama sadaka ya dhambi.
The seven days of the feast he shall prepare a burnt offering to Yahweh, seven bulls and seven rams without defect daily the seven days; and a male goat daily for a sin offering.
24 Kisha mwana mfalme atatengeneza sadaka ya chakula ya efa moja kwa kila ng'ombe na efa moja kwa kila kondoo dume pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
He shall prepare a meal offering, an ephah for a bull, an ephah for a ram, and a hin of oil to an ephah.
25 Katika siku ya saba ya mwezi siku ya kumi na tano ya mwezi, katika sikukuu, mwana wa mfalme atafanya matoleo katika siku hizi saba: sadaka za dhambi, sadaka za kuteketezwa, sadaka za chakula, na sadaka za mafuta.
“‘“In the seventh month, on the fifteenth day of the month, during the feast, he shall do like that for seven days. He shall make the same provision for sin offering, the burnt offering, the meal offering, and the oil.”

< Ezekieli 45 >