< Ezekieli 3 >

1 Akanambia, “Mwanadamu, kile ulichokikuta, kula. Kula hili gombo, kisha nenda kaongee na nyumba ya Israeli.”
And He said unto me: 'Son of man, eat that which thou findest; eat this roll, and go, speak unto the house of Israel.'
2 Basi nikafungua kinywa changu, na akanilisha hilo gombo.
So I opened my mouth, and He caused me to eat that roll.
3 Akanambia, “Mwana wa adamu, lisha tumbo lako na jaza tumbo lako kwa hili gombo ambalo nimekupa!” Basi nikalila, na lilikuwa tamu kama asali kwenye mdomo wangu.
And He said unto me: 'Son of man, cause thy belly to eat, and fill thy bowels with this roll that I give thee.' Then did I eat it; and it was in my mouth as honey for sweetness.
4 Kisha akanambia, “Mwana wa adamu, nenda kwenye nyumba ya Israeli na ongea maneno yangu kwao.
And He said unto me: 'Son of man, go, get thee unto the house of Israel, and speak with My words unto them.
5 Kwa kuwa hujatumwa kwa watu wenye maneno ya kushangaza au lugha ngumu, lakini kwa nyumba ya Israeli-
For thou art not sent to a people of an unintelligible speech and of a slow tongue, but to the house of Israel;
6 sio kwa taifa lenye nguvu ya maneno ya ajabu au lugha ngumu ambao maneno yao hutaweza kuyaelewa! Kama nikikutuma kwao, watakusikiliza.
not to many peoples of an unintelligible speech and of a slow tongue, whose words thou canst not understand. Surely, if I sent thee to them, they would hearken unto thee.
7 Lakini nyumba ya Israeli haitakuwa tayari kukusikiliza, kwa kuwa hawako tayari kunisikiliza mimi. Hivyo nyumba yote ya Israeli ni paji gumu na moyo mgumu.
But the house of Israel will not consent to hearken unto thee; for they consent not to hearken unto Me; for all the house of Israel are of a hard forehead and of a stiff heart.
8 Kumbe nimeufanya uso wako kama kaidi kama nyuso zao na paji lako kuwa gumu kama mapaji yao.
Behold, I have made thy face hard against their faces, and thy forehead hard against their foreheads.
9 Nimekufanya paji lako kama almasi, gumu kuliko jiwe la kiberiti! Usiwaogope wala kufadhaika kwa nyuso zao, kwa kuwa ni nyumba ya uasi.”
As an adamant harder than flint have I made thy forehead; fear them not, neither be dismayed at their looks, for they are a rebellious house.'
10 Kisha akanambia, “Mwana wa adamu, maneno yote niliyokutangazia-yachukue kwenye moyo wako na wasikize kwa sikio lako!
Moreover He said unto me: 'Son of man, all My words that I shall speak unto thee receive in thy heart, and hear with thine ears.
11 Kisha nenda kwa watumwa, kwa watu wako, na uzungumze nao. Waambie, 'Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo; iwapo watasikia au hapana.”
And go, get thee to them of the captivity, unto the children of thy people, and speak unto them, and tell them: Thus saith the Lord GOD; whether they will hear, or whether they will forbear.'
12 Kisha Roho akaniinua juu, na nikasikia nyuma yangu sauti yenye tetemeko la aridhi: “Ubarikiwe utukufu wa Yahwe kutoka mahali pake!”
Then a spirit lifted me up, and I heard behind me the voice of a great rushing: 'Blessed be the glory of the LORD from His place';
13 Ilikuwa sauti ya mabawa ya viumbe hai vilipokuwa vikigusana kila kimoja, na sauti ya magurudumu ambayo yalikuwa pamoja na hivyo viumbe, na sauti ya tetemeko kubwa arithi.
also the noise of the wings of the living creatures as they touched one another, and the noise of the wheels beside them, even the noise of a great rushing.
14 Roho akaniinua juu na kunichukua, Nikaenda kwa uchungu katika hasira kali rohoni mwangu, kwa kuwa mkono wa Yahwe ulikuwa na nguvu ukigandamiza juu yangu!
So a spirit lifted me up, and took me away; and I went in bitterness, in the heat of my spirit, and the hand of the LORD was strong upon me.
15 Hivyo nikaenda kwa watumwa huko Tel Abibu waliokuwa wakiishi karibu na Kebari Kanali, na niliishi miongoni mwao huko kwa mda wa miaka saba, kushinda kabisa katika mshangao.
Then I came to them of the captivity at Tel-abib, that dwelt by the river Chebar, and I sat where they sat; and I remained there appalled among them seven days.
16 Kisha ikatokea baada ya siku saba kwamba neno la Yahwe likanijia, likisema,
And it came to pass at the end of seven days, that the word of the LORD came unto me, saying:
17 “Mwana wa adamu, nimekufanya uwe mwangalizi kwa ajili ya nyumba ya Israeli, hivyo sikiliza neno kutoka kinywani mwangu, na uwapatie onyo langu.
'Son of man, I have appointed thee a watchman unto the house of Israel; and when thou shalt hear a word at My mouth, thou shalt give them warning from Me.
18 Nitakaposema kwa waovu, 'Utakufa hakika' na usimuonye au kuzungumza onyo kwa waovu kuhusu matendo yao maovu hivyo anaweza kuishi-yule muovu atakufa kwa ajili ya dhambi yake, lakini nitaitaka damu yake kutoka kwenye mkono wako.
When I say unto the wicked: Thou shalt surely die; and thou givest him not warning, nor speakest to warn the wicked from his wicked way, to save his life; the same wicked man shall die in his iniquity, but his blood will I require at thy hand.
19 Lakini kama ukimuonya muovo, na asiuache uovu wake au kutoka matendo yake maovu, kisha atakufa kwa dhambi yake, lakini utaokoa maisha yako mwenyewe.
Yet if thou warn the wicked, and he turn not from his wickedness, nor from his wicked way, he shall die in his iniquity; but thou hast delivered thy soul.
20 Kama mwenye haki ataicha haki yake na kutenda yasiyohaki, na nikaweka kizuizi mbele yake, atakufa. Kwasababu hukumuonya, atakufa katika dhambi yake, na sintokumbuka matendo ya haki aliyoyafanya, lakini nitaitaka damu yake kutoka kwenye mkono wako.
Again, when a righteous man doth turn from his righteousness, and commit iniquity, I will lay a stumblingblock before him, he shall die; because thou hast not given him warning, he shall die in his sin, and his righteous deeds which he hath done shall not be remembered; but his blood will I require at thy hand.
21 Lakini kama ukimuonya mwenye mtu mwenye haki kuacha kufanya dhambi halafu akaacha kutenda dhambi, ataishi hakika tangu alipo unywa; na utakuwa umeokoa maisha yako mwenyewe.”
Nevertheless if thou warn the righteous man, that the righteous sin not, and he doth not sin, he shall surely live, because he took warning; and thou hast delivered thy soul.'
22 Hivyo mkono wa Yahwe ulikuwa juu yangu huko, akanambia, “Inuka! nenda uwandani, na nitaongea na wewe huko!”
And the hand of the LORD came there upon me; and He said unto me: 'Arise, go forth into the plain, and I will there speak with thee.'
23 Nikainuka na kwenda uwandani, na huko utukufu wa Yahwe ulisimama, kama utukufu ambao niliokuwa nimeuona karibu na Kebari Kanali; hivyo nikaanguka kifudifudi.
Then I arose, and went forth into the plain; and, behold, the glory of the LORD stood there, as the glory which I saw by the river Chebar; and I fell on my face.
24 Roho akaja kwangu na kusimama juu ya miguu yangu; akaongea na mimi, na kunambia, “Nenda na jifungie mwenyewe kwenye nyumba yako,
Then spirit entered into me, and set me upon my feet; and He spoke with me, and said unto me: 'Go, shut thyself within thy house.
25 kwa sasa, mwana wa adamu, wataweka kamba juu yako na kukufunga ili usiweze kutoka nje miongoni mwao.
But thou, son of man, behold, bands shall be put upon thee, and thou shalt be bound with them, and thou shalt not go out among them;
26 Nitaufanya ulimi wako ugandamane na paa ya mdomo wako, ili kwamba uwe kimya, na hutaweza kuwakemea, kwa kuwa ni nyumba ya waasi.
and I will make thy tongue cleave to the roof of thy mouth, that thou shalt be dumb, and shalt not be to them a reprover; for they are a rebellious house.
27 Lakini nitakapozungumza na wewe, nitafungua mdomo wako hivyo utawaambia, 'Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.' Yeye asikiaye na asikie; yeye asiyesikia na asisikie, kwa kuwa wao ni nyumba ya kuasi!”
But when I speak with thee, I will open thy mouth, and thou shalt say unto them: Thus saith the Lord GOD; he that heareth, let him hear, and he that forbeareth, let him forbear; for they are a rebellious house.

< Ezekieli 3 >