< Yeremia 50 >

1 Hili ni neno alilolisema Yahwe juu ya Babeli, nchi ya Wakalidayo, kwa mkono wa Yeremia nabii,
The word that the LORD spoke concerning Babylon, concerning the land of the Chaldeans, by Jeremiah the prophet.
2 “Wajulishe mataifa ili wasikie. Toa ishara ili wasikie. Usiiache. Sema, 'Babeli imetwaliwa. Beli ameaibika. Merodaki amefadhaika. Sanamu zake zimeaibishwa; vinyago vyake vimefadhaika
Declare ye among the nations and announce, and set up a standard; announce, and conceal not; say: 'Babylon is taken, Bel is put to shame, Merodach is dismayed; her images are put to shame, her idols are dismayed.'
3 Taifa kutoka kaskazini litainuka kinyume chake, ili kuifanya nchi yake ukiwa. Hakuna hata mmoja, awe mtu au mnyama, atakayeishi ndani yake. Wataondoka.
For out of the north there cometh up a nation against her, which shall make her land desolate, and none shall dwell therein; they are fled, they are gone, both man and beast.
4 Katika siku hizo na wakati huo - hili ni tamko ya Yahwe - watu wa Israeli na watu wa Yuda watakusanyika ili kwenda kwa kulia na kumtafuta Yahwe Mungu wao.
In those days, and in that time, saith the LORD, the children of Israel shall come, they and the children of Judah together; they shall go on their way weeping, and shall seek the LORD their God.
5 Watauliza njia ya kwenda Sayuni nao watakwenda huko, wakisema, tutakwenda wenyewe ili kuungana na Yahwe katika agano la milele lisilosahaulikal
They shall inquire concerning Zion with their faces hitherward: 'Come ye, and join yourselves to the LORD in an everlasting covenant that shall not be forgotten.'
6 Watu wangu wamekuwa kondoo waliopotea. Wachungaji wao wamewapoteza milimani; wamewageuza kutoka mlima hata mlima. Walikwenda, wakasahau mahali walipokuwa wanaishi.
My people hath been lost sheep; their shepherds have caused them to go astray, they have turned them away on the mountains; they have gone from mountain to hill, they have forgotten their resting-place.
7 Kila awaendeaye anawararua. Washitaki wao walisema, 'Hatuna hatia, kwa sababu walimtenda dhambi Yahwe, nyumbani kwao halisi - Yahwe, tumaini la mababu zao.'
All that found them have devoured them; and their adversaries said: 'We are not guilty'; because they have sinned against the LORD, the habitation of justice, even the LORD, the hope of their fathers.
8 Tokeni kati ya Babeli; tokeni katika nchi ya Wakalidayo; iweni kama wafanyavyo mabeberu mbele ya kundi lote.
Flee out of the midst of Babylon, and go forth out of the land of the Chaldeans, and be as the he-goats before the flocks.
9 Maana tazama, ninaelekea kupeleka na kuinua kinyume cha Babeli kundi la mataifa makubwa kutoka kaskazini. Yatajipanga yenyewe kinyume chake. Kutoka hapo Babeli utatekwa. Mishale yao ni kama shujaa mzoefu asiyerudi mikono tupu.
For, lo, I will stir up and cause to come up against Babylon an assembly of great nations from the north country; and they shall set themselves in array against her, from thence she shall be taken; their arrows shall be as of a mighty man that maketh childless; none shall return in vain.
10 Ukaldayo itakuwa mateka. Wate waitekao wataridhika - asema Yahwe.
And Chaldea shall be a spoil; all that spoil her shall be satisfied, saith the LORD.
11 Mnafurahi, mnasherehekea kuteka urithi wangu; mnarukaruka kama ndama anayekanyaga katika malisho yake; mnalia kama farasi mwenye nguvu.
Because ye are glad, because ye rejoice, O ye that plunder My heritage, because ye gambol as a heifer at grass, and neigh as strong horses;
12 Hivyo mama yenu ataaibika sana; aliyewazaa atafadhaika. Tazama, atakuwa wa mwisho katika mataifa, nyika, nchi kame, na jangwa.
Your mother shall be sore ashamed, she that bore you shall be confounded; behold, the hindermost of the nations shall be a wilderness, a dry land, and a desert.
13 Kwa sababu ya hasira ya Yahwe, Babeli haitakaliwa, lakini itakuwa ukiwa mtupu. Kila apitaye kando ataogopa kwa sababu ya Babeli na atatoa sauti kwa sababu ya majeraha yake.
Because of the wrath of the LORD it shall not be inhabited, but it shall be wholly desolate; every one that goeth by Babylon shall be appalled and hiss at all her plagues.
14 Jipangeni wenyewe kumzunguka Babeli kinyume chake. Kila apindaye upinde na ampige. Msizuie mshale wenu wowote, maana amemtenda dhambi Yahwe.
Set yourselves in array against Babylon round about, all ye that bend the bow, shoot at her, spare no arrows; for she hath sinned against the LORD.
15 Pigeni kelele za ushindi kinyume chake ninyi nyote mmzungukao. Amesalimu mamlaka yake; minara yake imeanguka. Kuta zake zimebomolewa, maana hiki ni kisasi cha Yahwe. Jilipizeni kisasi juu yake! Mtendeeni kama alivyoyatenda mataifa mengine.
Shout against her round about, she hath submitted herself; her buttresses are fallen, her walls are thrown down; for it is the vengeance of the LORD, take vengeance upon her; as she hath done, do unto her.
16 Waaribuni wote mkulima apandaye mbegu naye atumiaye mundu wakati wa mavuno katika Babeli. Haya kila mtu na arudi kwa watu wake kutoka upanga wa mtesaji; na wakimbilie katika nchi yao wenyewe.
Cut off the sower from Babylon, and him that handleth the sickle in the time of harvest; For fear of the oppressing sword they shall turn every one to his people, and they shall flee every one to his own land.
17 Israeli ni kondoo aliyetawanywa na kupelekwa na simba mbali. Kwanza mfalme wa Ashuru alimrarua; kisha baadaye, Nebukadneza mfalme wa Babeli akavunja mifupa yake.
Israel is a scattered sheep, the lions have driven him away; first the king of Assyria hath devoured him, and last this Nebuchadrezzar king of Babylon hath broken his bones.
18 Kwa hiyo Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi: Tazama, nitamwadhibu mfalme wa Babeli na nchi yake, kama nilivyomwadhibu mfalme wa Ashuru.
Therefore thus saith the LORD of hosts, the God of Israel: Behold, I will punish the king of Babylon and his land, as I have punished the king of Assyria.
19 Nitamrudisha Israeli katika nchi yake; atajilisha katika Karmeli na Bashani. Kisha atajishibisha katika nchi ya kilima ya Efraimu na Gileadi.
And I will bring Israel back to his pasture, and he shall feed on Carmel and Bashan, and his soul shall be satisfied upon the hills of Ephraim and in Gilead.
20 Siku hizo na wakati huo, asema Yahwe, uovu utatafutwa katika Israeli, lakini hautaonekana. Nitauliza kuhusu dhambi za Yuda, lakini hazitaonekana, maana nitawasamehe mabaki niliowaacha.”
In those days, and in that time, saith the LORD, the iniquity of Israel shall be sought for, and there shall be none, and the sins of Judah, and they shall not be found; for I will pardon them whom I leave as a remnant.
21 Inuka dhidi ya nchi ya Merathaimu, kinyume chake nao waishio Pekodi. Wapigeni kwa makali ya upanga na mwatenge kwa ajili ya maangamizo - asema Yahwe - fanyeni kila ninachowaamru.
Go up against the land of Merathaim, even against it, and against the inhabitants of Pekod; waste and utterly destroy after them, saith the LORD, and do according to all that I have commanded thee.
22 Sauti ya vita na maangamizi ya kustaajabisha yamo katika nchi.
Hark! battle is in the land, and great destruction.
23 Jinsi gani nyundo ya mataifa yote imekatiliwa mbali na kuharibiwa. Jinsi Babeli amekuwa kitu cha kushangaza kati ya mataifa.
How is the hammer of the whole earth cut asunder and broken! How is Babylon become a desolation among the nations!
24 Nimetega mtego dhidi yako. Umenaswa, Babeli, nawe haukutambua! Ulionekana na kukamatwa, tangu uliponidhihaki, Yahwe.
I have laid a snare for thee, and thou art also taken, O Babylon, and thou wast not aware; thou art found, and also caught, because thou hast striven against the LORD.
25 Yahwe amefungua ghala lake la silaha na anachukua silaha kwa ajili ya kutekekeleza hasira yake. Kuna kazi kwa ajili ya Yahwe wa majeshi katika nchi ya Wakaldayo.
The LORD hath opened His armoury, and hath brought forth the weapons of His indignation; for it is a work that the Lord GOD of hosts hath to do in the land of the Chaldeans.
26 Mshambulie kutokea mbali. Fungua maghala yake ya chakula na kumrundika kama marundo ya nafaka. Mtenge mbali na maangamizi. Usimbakizie masalia.
Come against her from every quarter, open her granaries, cast her up as heaps, and destroy her utterly; let nothing of her be left.
27 Ua madume wake wote wa ng'ombe. Washushe sehemu ya machinjio. Ole wao, maana siku yao imefika - wakati wa kuadhibiwa kwao.
Slay all her bullocks, let them go down to the slaughter; woe unto them! for their day is come, the time of their visitation.
28 Kuna sauti ya wale wanaokimbia, walionusurika, katika nchi ya Babeli. Hawa watatoa taarifa ya kisasi cha Yahwe Mungu wetu kwa Sayuni, kisasi kwa hekalu lake.”
Hark! they flee and escape out of the land of Babylon, to declare in Zion the vengeance of the LORD our God, the vengeance of His temple.
29 Ita wapiga pinde dhidi ya Babeli - wale wote wapindao pinde zao. Piga kambi kinyume chake, na msimwache yeyote kutoroka. Mlipeni kwa kile alichofanya. Mfanyieni kwa kipimo alichotumia. Maana amemdharau Yahwe, Mtakatifu wa Israeli.
Call together the archers against Babylon, all them that bend the bow; encamp against her round about, let none thereof escape; recompense her according to her work, according to all that she hath done, do unto her: for she hath been arrogant against the LORD, against the Holy One of Israel.
30 Hivyo vijana wake wataanguka katika viwanja vya mji, na wapiganaji wake wote wataangamizwa siku hiyo - hili ni tamko la Yahwe.”
Therefore shall her young men fall in her broad places, and all her men of war shall be brought to silence in that day, saith the LORD.
31 Tazama, mimi ni kunyume chako, mwenye majivuno - hili ni tamko la Bwana Yahwe wa majeshi - maana siku yako imefika, mwenye kiburi, wakati nitakapokuadhibu.
Behold, I am against thee, O thou most arrogant, saith the Lord GOD of hosts; for thy day is come, the time that I will punish thee.
32 Hivyo wenye kiburi watajikwaa na kuanguka. Hakuna atakaye wainua. Nitawasha moto katika miji yao; utateketeza kila kitu kati yake.
And the most arrogant shall stumble and fall, and none shall raise him up; and I will kindle a fire in his cities, and it shall devour all that are round about him.
33 Yahwe wa majeshi asema hivi: watu wa Israeli wamenyanyaswa, pamoja na watu wa Yuda. Wate waliowateka bado wanawashikilia; wanakataa kuwaacha waondoke.
Thus saith the LORD of hosts: The children of Israel and the children of Judah are oppressed together; and all that took them captives hold them fast; they refuse to let them go.
34 Yeye awaokoaye ni mwenye nguvu. Yahwe wa majeshi ni jina lake. Kwa hakika atalitetea shitaka lao, ili kuleta pumziko katika nchi, na kuwapiga wakaao Babeli.
Their Redeemer is strong, the LORD of hosts is His name; He will thoroughly plead their cause, that He may give rest to the earth, and disquiet the inhabitants of Babylon.
35 Upanga u juu ya Wakalidayo - asema Yahwe - na juu ya wakaao Babeli, viongozi wake, na wenye hekima wake.
A sword is upon the Chaldeans, saith the LORD, and upon the inhabitants of Babylon, and upon her princes, and upon her wise men.
36 Upanga unakuja juu ya waganga, ili wajione kuwa wajinga. Upanga utakuwa juu ya askari wake, hivyo watajaa hofu.
A sword is upon the boasters, and they shall become fools; a sword is upon her mighty men, and they shall be dismayed.
37 Upanga utakuwa juu ya farasi wake, vibandawazi vyao na na watu wote waliomo Babeli, hivyo watakuwa kama wanawake. Upanga utakuwa juu ya ghala zake, nazo zitatekwa.
A sword is upon their horses, and upon their chariots, and upon all the mingled people that are in the midst of her, and they shall become as women; a sword is upon her treasures, and they shall be robbed.
38 Ukame unakuja juu ya maji yake, hivyo yatakauka. Maana ni nchi ya miungu wasiofaa, na wanafanya kama watu waliofanywa punguani kwa miungu yao isiyosaidia.
A drought is upon her waters, and they shall be dried up; for it is a land of graven images, and they are mad upon things of horror.
39 Hivyo wanyama wa jangwani wakaishi na mbwea wataishi huko, na watoto wa mbuni wataishi ndani yake. Kwa muda wote, hatakaliwa tena. Kutoka kizazi hata kizazi, hatakaliwa tena na watu.
Therefore the wild-cats with the jackals shall dwell there, and the ostriches shall dwell therein; and it shall be no more inhabited for ever, neither shall it be dwelt in from generation to generation.
40 Kama vile Mungu alivyoziangamiza Sodoma na Gomora na majirani zake - asema Yahwe - hakuna atakayeishi huko; hakuna mtu atakayekaa ndani yake.”
As when God overthrew Sodom and Gomorrah and the neighbour cities thereof, saith the LORD; so shall no man abide there, neither shall any son of man dwell therein.
41 “Tazama, watu wanakuja kutoka kaskazini, maana taifa kubwa na wafalme wengi wamemtikisa kutokea mbali.
Behold, a people cometh from the north, and a great nation, and many kings shall be roused from the uttermost parts of the earth.
42 Watachukua pinde na mishale. Ni wakatili na hawana huruma. Sauti yao ni kama mngurumo wa bahari, na wamepanda farasi katika mpangilio kama watu wapiganao, dhidi yako, bindi Babeli.
They lay hold on bow and spear, they are cruel, and have no compassion; their voice is like the roaring sea, and they ride upon horses; set in array, as a man for war, against thee, O daughter of Babylon.
43 Mfalme wa Babeli amesikia habari yao na mikono yake imelegea kwa huzuni. Mashaka yamemshika kama mwanamke katika utungu.
The king of Babylon hath heard the fame of them, and his hands wax feeble; anguish hath taken hold of him, and pain, as of a woman in travail.
44 Tazama! Anakwenda juu kama simba atokaye katika miinuko ya Yordani kuelekea katika eneo la malisho ya uvumilivu. Maana kwa haraka nitawafanya wakimbie kutoka humo, nami nitamweka mtu aliyechaguliwa kwa uangalizi wake. Maana ni nani aliye kama mimi, na ni nani atakayeniagiza? Mchungaji gani awezaye kunizuia?
Behold, he shall come up like a lion from the thickets of the Jordan against the strong habitation; for I will suddenly make them run away from it, and whoso is chosen, him will I appoint over it; for who is like Me? and who will appoint Me a time? and who is that shepherd that will stand before Me?
45 Sikilizeni mipango ambayo Yahwe ameamua juu ya Babeli, mipango aliyonayo dhidi ya nchi ya Wakaldayo. Kwa hakika wataondolewa, hata kundi dogo zaidi. Eneo lao la malisho litageuzwa kuwa sehemu zenye magofu.
Therefore hear ye the counsel of the LORD, that He hath taken against Babylon, and His purposes, that He hath purposed against the land of the Chaldeans: surely the least of the flock shall drag them away, surely their habitation shall be appalled at them.
46 Kwa sauti ya kuangushwa kwa Babeli nchi inatikisika, na sauti ya mateso yao inasikiwa kati ya mataifa.”
At the noise of the taking of Babylon the earth quaketh, and the cry is heard among the nations.

< Yeremia 50 >