< Ezekieli 26 >

1 Hivyo ilikuwa katika mwaka wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
And it was in one plus ten year on [day] one of the month it came [the] word of Yahweh to me saying.
2 “Mwanadamu, kwa sababu Tiro amesema juu ya Yerusalemuu, 'Aha! Malango ya watu waliovunjika! Amenigeukia; Nitajazwa kwa sababu ameharibika.'
O son of humankind because that it said Tyre on Jerusalem aha! it is broken [the] doors of the peoples it has been turned over to me I will be filled it has been laid waste.
3 Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi, 'Tazama! Niko juu yako, Tiro, na nitayainua mataifa mengi juu yako kama bahari iiunuavyo mawimbi yake.
Therefore thus he says [the] Lord Yahweh here I [am] on you O Tyre and I will bring up on you nations many as brings up the sea waves its.
4 Wataziharibu kuta za Tiro na kuiangusha chini minara yao. Nitafagia mavumbi yake mbali na kumfanya kama jiwe tupu.
And they will destroy [the] walls of Tyre and they will tear down towers its and I will scrape away dust its from it and I will make it into bareness of rock.
5 Atakuwa sehemu ya kuwekea nyavu kati ya bahari, kwa kuwa nimesema hilo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-na atakuwa mateka kwa ajili ya mataifa.
A spreading place of nets it will be in [the] middle of the sea for I I have spoken [the] utterance of [the] Lord Yahweh and it will become spoil for the nations.
6 Binti zake walioko mashambani watachinjwa kwa panga, na watajua kwamba mimi ni Yahwe.'
And daughters its which [are] on the land with the sword they will be killed and they will know that I [am] Yahweh.
7 Kwa kuwa hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Tazama, kutoka kaskazini namleta Nebukadreza mfalme wa Babeli, mfalme wa wafalme, dhidi ya Tiro, pamoja na farasi na magari ya farasi, na pamoja na waendesha farasi na watu wengi.
For thus he says [the] Lord Yahweh here I [am] about to bring against Tyre Nebuchadnezzar [the] king of Babylon from [the] north [the] king of kings with horse[s] and with chariotry and with horsemen and a company and a people numerous.
8 Atawaua binti zako katika shamba. Ataweka kazi ya boma na kujenga ulaghai dhidi ya kuta zako na kuziinua ngao dhidi yao.
Daughters your on the land with the sword he will kill and he will make on you a siege-wall and he will pour out on you a mound and he will raise up on you a body shield.
9 Ataweka vyombo vya kubomolea dhidi ya kuta zako, na vyombo vyake vitaanguka chini ya minara yako.
And [the] blow of battering-ram his he will set on walls your and towers your he will break down with swords his.
10 Farasi zake zitakuwa nyingi kwamba mavumbi yao yatawafunika. Kuta zako zitatikisika kwa mlio wa waendesha farasi, magurudumu, na magari ya farasi. Wakati atakapoingia malango yako, ataingia kama watu waingiavyo kwenye mji ambao kuta zimebomolewa.
From [the] abundance of horses his it will cover you dust their from [the] sound of a horseman and wheel[s] and chariot[s] they will shake walls your when comes he in gates your like [the] entering of a city broken into.
11 Kwato za farasi zake zitaikanyaga mitaa yako yote. Atawaua watu wako kwa upanga na nguzo za uweza wako zitaanguka chini.
With [the] hooves of horses his he will trample all streets your people your with the sword he will kill and [the] pillars of strength your to the ground it will come down.
12 Watauteka nyara utajiri wako na bidhaa iliyoporwa. Watabomoa kuta zako na kuziharibu nyumba zako za kifahari. Mawe yako, mbao zako, na kokoto watazitupa kwenye maji.
And they will plunder wealth your and they will take as spoil merchandise your and they will tear down walls your and [the] houses of desire your they will pull down and stones your and wood your and dust your in [the] midst of [the] waters they will put.
13 Nitaikomesha sauti ya nyimbo zako. Sauti ya vinubi haitasikika tena.
And I will put an end to [the] noise of songs your and [the] sound of harps your not it will be heard again.
14 Nitakufanya jiwe tupu, utakuwa mahali ambapo nyavu zitasambazwa kuzikausha. Hutajengwa tena, kwa kuwa mimi, Bwana Yahwe nimesema-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
And I will make you into bareness of rock a spreading place of nets you will be not you will be built again for I Yahweh I have spoken [the] utterance of [the] Lord Yahweh.
15 Bwana Yahwe amwambia hivi Tiro, 'Je visiwa havitatetemeka kwa mlio wa kuanguka kwako, na pamoja na watakaogumia kwa jeraha wakati machinjio mabaya yatakapokuwa kati yako?
Thus he says [the] Lord Yahweh to Tyre ¿ not - from [the] sound of downfall your when groan [the] fatally wounded when is killed a slaughter in [the] midst of you will they quake the islands.
16 Kisha wakuu wote wa bahari watakaposhuka kutoka kwenye viti vyao vya enzi na kuvua mavazi yao rasmi na kutupa mavazi yaliyonakshiwa. Watavaa wenyewe kwa kutetemeka, wataketi chini na kutetemeka kila wakati, na wataogopa kwa sababu yako.
And they will go down from on thrones their all [the] princes of the sea and they will remove robes their and [the] clothes of multicolored cloth their they will strip off trembling - they will be clothed on the ground they will sit and they will tremble to moments and they will be appalled on you.
17 Watainua maombolezo juu yako na kukwambia, umekuwaje, uliyekuwa umekaliwa na manahodha wa meli, umeharibika. Mji mashuhuri ulikuwa imara sana-sasa umetoka kwenye bahari. Wale wanaoishi ndani yake wanaotia hofu kuhusu wenyewe juu ya kila mmoja aliyeishi karibu nao.
And they will take up on you a lamentation and they will say to you how! you have perished O inhabited [city] from [the] seas O city that was praised which it was mighty in the sea it and inhabitants its which they gave terror their to all inhabitants its.
18 Sasa fukwe zitatetemeka katika siku ya kuanguka kwako. Visiwa katika bahari vimeogofya, kwa sababu umekufa.'
Now they will tremble the islands [the] day of downfall your and they will be terrified the islands which [are] in the sea because went out you.
19 Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: wakati nitakapokufanya wewe mji kuwa ukiwa, kama miji mingine ambayo haikaliwi, wakati nitakapoviinua vilindi dhidi yako, na wakati maji makuu yatakapokufunika,
For thus he says [the] Lord Yahweh when make I you a city desolate like cities which not they are inhabited when bring up over you [the] deep and they will cover you the waters many.
20 kisha nitakushusha chini kwenda kwa watu wa nyakati za zamani, kama wengingine walioenda chini kwenye shimo; kwa kuwa nitakufanya uishi katika falme za chini za dunia kama uharibifu wa nyakati za zamani. Kwa sababu hii hutarudi na kusimama katika nchi ya walio hai.
And I will send down you with [those who] have gone down of [the] pit to a people of antiquity and I will cause to dwell you in [the] earth of [the] lowest parts like waste places from long ago with [those who] have gone down of [the] pit so that not you will remain and I will put splendor in [the] land of [the] living.
21 Nitaweka janga juu yako, na hutakuwepo tena milele. Kisha utatafutwa, lakini hutapatikana milele tena-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
Terrors I will give to you and there not [will be] you so you may be sought and not you will be found again for ever [the] utterance of [the] Lord Yahweh.

< Ezekieli 26 >