< Ezekieli 18 >

1 Neno la Yahwe likanijia tena, kusema,
و کلام خداوند بر من نازل شده، گفت:۱
2 “Je mnamaana gani, ninyi mliotumia hii mithali kuhusiana na nchi ya Israeli na kusema, 'Wababa wamekula zabibu mbichi, na meno ya watoto imetiwa ganzi'?
«شما چه‌کار دارید که این مثل رادرباره زمین اسرائیل می‌زنید و می‌گویید: پدران انگور ترش خوردند و دندانهای پسران کندگردید.»۲
3 Kama nishivyo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-bila shaka hakutakuwa na fursa yoyote tena kwa ajili yenu kuitumia hii mithali katika Israeli.
خداوند یهوه می‌گوید: «به حیات خودم قسم که بعد از این این مثل را در اسرائیل نخواهیدآورد.۳
4 Tazama! Kila uhai ni mali yangu-uhai wa baba na uhai wa mwana pia, ni mali yangu! roho itendayo dhambi ndiyo itakayokufa!
اینک همه جانها از آن منند چنانکه جان پدر است، همچنین جان پسر نیز، هردوی آنها ازآن من می‌باشند. هر کسی‌که گناه ورزد او خواهدمرد.۴
5 Itasemwaje kuhusu mtu mwenye haki na achukuaye yaliyo halali na haki-
و اگر کسی عادل باشد و انصاف و عدالت رابعمل آورد،۵
6 kama asipokula juu ya milima au kuinua macho yake kwa sananmu za nyumba ya Israeli, na hakumnajisi mke wa jirani yake, wala kumsemesha mwanamke katika kipindi chake cha mwezi, je! Yu mwenye haki?
و بر کوهها نخورد و چشمان خودرا بسوی بتهای خاندان اسرائیل برنیفرازد و زن همسایه خود را بی‌عصمت نکند و به زن حایض نزدیکی ننماید،۶
7 Je! Itasemwaje kuhusu mtu ambaye hakumkandamiza yeyote, na kumrudisha mdeni wake kwa kile kilichokuwa kimewekwa kwa ajili ya rehani, na hakuiba lakini kuwapatia chakula wenye njaa na kuwafunika uchi kwa nguo, je yu mwenye haki?
و بر کسی ظلم نکند و گروقرضدار را به او رد نماید و مال کسی را به غصب نبرد، بلکه نان خود را به گرسنگان بدهد وبرهنگان را به‌جامه بپوشاند،۷
8 Je! Itasemwaje kuhusu mtu ambaye hakuchukua faida kubwa kwa ile pesa aliyokopa, na hakuchukua faida kubwa kwa kile alichokiuza?
و نقد را به سودندهد و ربح نگیرد، بلکه دست خود را از ستم برداشته، انصاف حقیقی را در میان مردمان اجرادارد،۸
9 Amesemwa kwamba amechukua yaliyo halali na kuimarisha uaminifu kati ya watu. Kama huyo mtu akitembea katika sheria zangu na kuzishika hukumu zangu kufanya kwa uaminifu, kisha ahadi kwa ajili ya mtu mwenye haki ni hii: Ataishi hakika! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
و به فرایض من سلوک نموده و احکام مرانگاه داشته، به راستی عمل نماید. خداوند یهوه می‌فرماید که آن شخص عادل است و البته زنده خواهد ماند.۹
10 Lakini akizaa mwana mnyang'anyi mmwaga damu na kufanya mengi katika haya mambo kama yalivyotajwa hapa,
«اما اگر او پسری ستم پیشه و خونریز تولیدنماید که یکی از این کارها را بعمل آورد،۱۰
11 hata kama baba yake hakufanya mojawapo katika haya mambo, lakini akala juu ya milima na akamnajisi mke wa jirani yake, Je! itasemwaje juu yake?
وهیچکدام از آن اعمال نیکو را بعمل نیاورد بلکه برکوهها نیز بخورد و زن همسایه خود را بی‌عصمت سازد،۱۱
12 Huyu mtu huwakandamiza maskini na wahitaji, na huwakamata na kuwanyang'anya, na hawarudishii dhamana, na huyanua macho yake kwa sanamu na kufanya matendo maovu,
و بر فقیران و مسکینان ظلم نموده، مال مردم را به غصب ببرد و گرو را پس ندهد، بلکه چشمان خود را بسوی بتها برافراشته، مرتکب رجاسات بشود،۱۲
13 na hukopesha pesa kwa faida ya juu sana na kufanya faida kubwa juu ya anachokiuza, Je! huyo mtu ataishi? Hakika hataishi! Atakufa hakika na damu yake itakuwa juu yake kwa sababu amefanya haya mambo ya chuki.
و نقد را به سود داده، ربح گیرد، آیا او زنده خواهد ماند؟ البته او زنده نخواهد ماند و به‌سبب همه رجاساتی که بجاآورده است خواهد مرد و خونش بر سرش خواهد بود.۱۳
14 Lakini Tazama! tuseme kuna mtu aliyezaa mwana, na mwana wake huona dhambi zote za baba yake alizozifanya, na kupitia kuziona, hakuyafanya hayo mambo.
«و اگر پسری تولید نماید که تمامی گناهان را که پدرش بجا می‌آورد دیده، بترسد و مثل آنهاعمل ننماید،۱۴
15 Huyo mwana hakula juu ya milima, na hakuinua macho yake kwa sanamu za nyumba ya Israeli, na hakumtia unajisi mke wa jirani yake, Je! itasemwaje juu yake?
و بر کوهها نخورد و چشمان خود را بسوی بتهای خاندان اسرائیل برنیفرازد وزن همسایه خویش را بی‌عصمت نکند،۱۵
16 Yule mwana hakumkandamiza yeyote, au kutwaa dhamana, au kupoteza vitu, lakini badala yake kutoa chakula chake kwa wenye njaa na kuwafunika wenye uchi kwa nguo.
و برکسی ظلم نکند و گرو نگیرد و مال احدی را به غصب نبرد بلکه نان خود را به گرسنگان دهد وبرهنگان را به‌جامه پوشاند،۱۶
17 Huyo mwana hakumkandamiza yeyote au au kuchukua faida ambayo ni ya juu sana au kufanya manufaa kwa ajili ya mkopo, lakini ameyashika maagizo yangu na kuenenda sawa sawa na sheria zangu; huyo mwana hatakufa kwa ajili ya dhambi za baba yake: Ataishi hakika!
و دست خود را ازفقیران برداشته، سود و ربح نگیرد و احکام مرا بجاآورده، به فرایض من سلوک نماید، او به‌سبب گناه پدرش نخواهد مرد بلکه البته زنده خواهد ماند.۱۷
18 Baba yake, kwa kuwa aliwakandamiza wengine kwa nguvu nyingi na kumnyang'anya ndugu yake, na kufanya yasiyo mema miongoni mwa watu wake-tazama, atakufa katika uovu wake.
و اما پدرش چونکه با برادران خود به شدت ظلم نموده، مال ایشان را غصب نمود و اعمال شنیع را در میان قوم خود بعمل آورد او البته به‌سبب گناهانش خواهد مرد.۱۸
19 Lakini ninyi husema, 'Kwa nini mwana asibebe uovu wa baba yake?' Kwa sababu mwana hubeba yaliyo halali na haki na kuzitunza amri zangu; huzifanya. Ataishi hakika!
«لیکن شما می‌گویید چرا چنین است؟ آیاپسر متحمل گناه پدرش نمی باشد؟ اگر پسرانصاف و عدالت را بجا آورده، تمامی فرایض مرانگاه دارد و به آنها عمل نماید، او البته زنده خواهد ماند.۱۹
20 Yule atendaye dhambi, ndiye ambaye atakufa. Mwana hatabeba uovu wa baba yake, na baba hatabeba uovu wa mwana wake. Haki ya yule atendaye haki itakuwa juu yakwe mwenyewe, na uovu wa mwenye uovu utakuwa juu yake mwenyewe.
هر‌که گناه کند او خواهد مرد. پسر متحمل گناه پدرش نخواهد بود و پدرمتحمل گناه پسرش نخواهد بود. عدالت مردعادل بر خودش خواهد بود و شرارت مرد شریربر خودش خواهد بود.۲۰
21 Lakini kama mwovu ageukapo kutoka dhambi zake zote alizofanya, na kuzitunza sheria zangu zote na kufanya yaliyo halali na haki, kisha hakika ataishi na hatakufa.
«و اگر مرد شریر از همه گناهانی که ورزیده باشد بازگشت نماید و جمیع فرایض مرا نگاه داشته، انصاف و عدالت را بجا آورد او البته زنده مانده نخواهد مرد.۲۱
22 Makosa yote aliyoyafanya hayatakumbukwa juu yake. Ataishi kwa hiyo haki aliyoitenda.
تمامی تقصیرهایی که کرده باشد به ضد او به یاد آورده نخواهد شد بلکه در عدالتی که کرده باشد زنده خواهد ماند.»۲۲
23 Je! Nitafurahia juu ya kifo cha mwovu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-na sio katika kugeuka kwake kutoka njia yake ili kwamba aweze kuishi?
خداوند یهوه می‌فرماید: «آیا من از مردن مرد شریر مسرور می‌باشم؟ نی بلکه از اینکه ازرفتار خود بازگشت نموده، زنده ماند.۲۳
24 Lakini kama mtu mwenye haki ageukapo kutoka kwenye haki yake na kufanya maovu na kutenda machukizo kama machukizo yote ambayo mtu mwovu afanyayo, basi ataishi? Haki yake yote aliyoifanya haitakumbukwa wakati atakaponisaliti katika uhaini wake. Hivyo atakufa katika dhambi alizofanya.
و اگرمرد عادل از عدالتش برگردد و ظلم نموده، موافق همه رجاساتی که شریران می‌کنند عمل نماید آیااو زنده خواهد ماند؟ نی بلکه تمامی عدالت او که کرده است به یاد آورده نخواهد شد و در خیانتی که نموده و در گناهی که ورزیده است خواهدمرد.۲۴
25 Lakini ninyi husema, 'Njia ya Bwana si sawa!' sikilizeni, nyumba ya Israeli! Je njia zangu haziko sawa? Je si njia ambazo haziko sawa?
«اما شما می‌گویید که طریق خداوندموزون نیست. پس حال‌ای خاندان اسرائیل بشنوید: آیا طریق من غیر موزون است و آیاطریق شما غیر موزون نیست؟۲۵
26 Wakati mtu mwenye haki ageukapo kutoka kwenye makosa yake, na kufanya maovu na kufa kwa sababu ya hayo, kisha atakufa katika uovu ambao alioufanya.
چونکه مردعادل از عدالتش برگردد و ظلم کند در آن خواهدمرد. به‌سبب ظلمی که کرده است خواهد مرد.۲۶
27 Lakini wakati mtu mwovu ageukapo kutoka uovu wake alioufanya na kufanya yaliyo halali na haki, kisha ataulinda uhai wake.
و چون مرد شریر را از شرارتی که کرده است بازگشت نماید و انصاف و عدالت را بجا آورد، جان خود را زنده نگاه خواهد داشت.۲۷
28 Kwa kuwa ameona na kugeuka kutokana na makosa yake yote ambayo aliyoyafanya. Hakika ataishi, na hatakufa.
چونکه تعقل نموده، از تمامی تقصیرهایی که کرده بودبازگشت کرد البته زنده خواهد ماند و نخواهدمرد.۲۸
29 Lakini nyumba ya Israeli husema, 'Njia ya Bwana haiko sawa!' Ni namna gani njia zangu si sawa, nyumba ya Israeli? Ni njia zenu ndizo si sawa.
لیکن شما‌ای خاندان اسرائیل می‌گوییدکه طریق خداوند موزون نیست. ای خاندان اسرائیل آیا طریق من غیر موزون است و آیاطریق شما غیر موزون نیست؟»۲۹
30 Kwa hiyo nitamuhukumu kila mtu miongoni mwenu kulingana na njia zake, nyumba ya Israeli! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo. Tubuni na rudini kutoka kwenye makosa yenu yote ili kwamba wasiwe kikwazo cha uovu dhidi yenu.
بنابراین خداوند یهوه می‌گوید: «ای خاندان اسرائیل من برهریک از شما موافق رفتارش داوری خواهم نمود. پس توبه کنید و از همه تقصیرهای خودبازگشت نمایید تا گناه موجب هلاکت شما نشود.۳۰
31 Tupilia mbali makosa yenu yote mliyoyafanya; jifanyieni moyo mpya na roho mpya. Kwa nini mfe, nyumba ya Israeli?
تمامی تقصیرهای خویش را که مرتکب آنها شده‌اید از خود دور اندازید و دل تازه و روح تازه‌ای برای خود ایجاد کنید. زیرا که‌ای خاندان اسرائیل برای چه بمیرید؟۳۱
32 Kwa kuwa sifurahii kifo cha yule afaye-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-hivyo tubuni na muishi!”
زیرا خداوند یهوه می‌گوید: من از مرگ آنکس که می‌میرد مسرورنمی باشم. پس بازگشت نموده، زنده مانید.»۳۲

< Ezekieli 18 >