< Ezekieli 13 >

1 Tena, neno la Yahwe likanijia, kusema,
And the word of the LORD came unto me, saying:
2 “Mwanadamu, tabiri dhidi ya manabii wanaotabiri katika Israeli, na uwaambie wale wanotabiri nje ya fikra zao wenyewe, 'Lisikilizeni neno la Yahwe.
'Son of man, prophesy against the prophets of Israel that prophesy, and say thou unto them that prophesy out of their own heart: Hear ye the word of the LORD:
3 Bwana Yahwe asema hivi: Ole wao manbii wajinga ambao wafwatao roho zao wenyewe, lakini wale wasioona kitu!
Thus saith the Lord GOD: Woe unto the vile prophets, that follow their own spirit, and things which they have not seen!
4 Israeli, manabii zako wamekuwa kama mbeha kwenye aridhi iliyoharibiwa na vita.
O Israel, thy prophets have been like foxes in ruins.
5 Hamkwenda kwenye nyufa katika ukuta uliozunguka nyumba ya Israeli kwa ajili ya kuukarabati, ili kupigana katika vita katika siku ya Yahwe.
Ye have not gone up into the breaches, neither made up the hedge for the house of Israel, to stand in the battle in the day of the LORD.
6 Watu wameona uongo na kufanya utabiri wa uongo, wale wasemao, “Hivi na hivi ndvyo Yahwe asemavyo.” Yahwe hajawatuma, lakini hata hivyo wamewafanya watu kutumaini kwamba ujumbe wao utakuwa kweli.
They have seen vanity and lying divination, that say: The LORD saith; and the LORD hath not sent them, yet they hope that the word would be confirmed!
7 Je hamkusikia maono ya uongo na kufanya utabiri wa uongo, ninyi msemao, “Hivi na hivi ndivyo Yahwe asemavyo” Wakati mimi mwenyewe sikuongea?'
Have ye not seen a vain vision, and have ye not spoken a lying divination, whereas ye say: The LORD saith; albeit I have not spoken?
8 Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi, 'Kwa sababu mmesikia maono ya uongo na kuwaambia uongo-kwa hiyo hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo dhidi yenu:
Therefore thus saith the Lord GOD: Because ye have spoken vanity, and seen lies, therefore, behold, I am against you, saith the Lord GOD.
9 Mkono wangu utakuwa juu yenu ninyi manabii mliodanganya maono na wale waliofanya unabii wa uongo. Hawatakuwepo kwenye kusanyiko la watu wangu, au kuandikishwa katika kumbukumbu ya nyumba ya Israeli; hawataenda kwenye nchi ya Israeli. Kwa kuwa mtajua yakwamba mimi ni Bwana Yahwe!
And My hand shall be against the prophets that see vanity, and that divine lies; they shall not be in the council of My people, neither shall they be written in the register of the house of Israel, neither shall they enter into the land of Israel; and ye shall know that I am the Lord GOD.
10 Kwa sababu hiyo, na kwa sababu wamewaongoza watu wangu kuwapotosha na kusema, “Amani!” wakati hakuna amani, wanajenga ukuta ambao wataupaka rangi ya chokaa.'
Because, even because they have led My people astray, saying: Peace, and there is no peace; and when it buildeth up a slight wall, behold, they daub it with whited plaster;
11 Waambie wale wanaopaka chokaa ukuta, 'Utaanguka chini; kutakuwa na mvua ya kufurika, na nitaleta mvua ya mawe kuufanya uanguke chini, na upepo wa dhoruba kupuliza hata kuuvunja chini.
say unto them that daub it with whited plaster, that it shall fall; there shall be an overflowing shower, and ye, O great hailstones, shall fall, and a stormy wind shall break forth,
12 Tazama, ukuta utaanguka chini. Je wengine hawakuwaambia, “Iko wapi chokaa mliyoipaka juu yake?”
and, lo, when the wall is fallen, shall it not be said unto you: Where is the daubing wherewith ye have daubed it?
13 Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi: Nitaleta upepo wa dhoruba katika ghadhabu yangu, na kutakuwa na mafuriko ya mvua kwenye ghadhabu yangu! Mvua ya mawe katika ghadhabu yangu itauharibu kabisa.
Therefore thus saith the Lord GOD: I will even cause a stormy wind to break forth in My fury; and there shall be an overflowing shower in Mine anger, and great hailstones in fury to consume it.
14 Kwa kuwa nitaurarua chini ukuta ambao mlioufunika kwa chokaa, na nitaubomoa hata kwenye nchi na kuifunua misingi yake. Hivyo utaanguka, nanyi nyote mtaangamizwa katikati ya huo.
So will I break down the wall that ye have daubed with whited plaster, and bring it down to the ground, so that the foundation thereof shall be uncovered; and it shall fall, and ye shall be consumed in the midst thereof; and ye shall know that I am the LORD.
15 Ndivyo nitakavouangamiza kwa ghadhabu yangu ukuta na wale walioupaka chokaa. Nitawaambia, “Ukuta hautaonekana tena, wala watu wanaoupaka chokaa-
Thus will I spend My fury upon the wall, and upon them that have daubed it with whited plaster; and I will say unto you: The wall is no more, neither they that daubed it;
16 manabii wa Israeli wale waliotabiri kuhusu Yerusalemu na wale waliokuwa wameona amani kwa ajili yake. Lakini hakuna amani! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
to wit, the prophets of Israel that prophesy concerning Jerusalem, and that see visions of peace for her, and there is no peace, saith the Lord GOD.
17 Hivyo wewe, mwanadamu, weka uso wako dhidi ya binti za watu wako wale wanaotabiri kwa akili zao wenyewe, na kutabiri dhidi yao.
And thou, son of man, set thy face against the daughters of thy people, that prophesy out of their own heart; and prophesy thou against them,
18 Sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Ole kwa wanawake washonao hiziri kwenye kila sehemu ya mkono wao na kutengeza vitambaa vya shela kwa ajili ya vichwa vyao kwa kila kipimo, ili kuwinda watu. Je mtawawinda watu wangu ila kuokoa maisha yenu wenyewe?
and say: Thus saith the Lord GOD: Woe to the women that sew cushions upon all elbows, and make pads for the head of persons of every stature to hunt souls! Will ye hunt the souls of My people, and save souls alive for yourselves?
19 Ninyi mmenikufuru mbele ya watu wangu kwa ajili ya makonzi ya shayiri na vipande vya mkate, kuwaua watu ambao hawakutakiwa kufa, na kuyalinda maisha ya wale ambao hawatakiwi kuendelea kuishi, kwa sababu ya uongo wenu kwa watu wangu walio wasikiliza.
And ye have profaned Me among My people for handfuls of barley and for crumbs of bread, to slay the souls that should not die, and to save the souls alive that should not live, by your lying to My people that hearken unto lies.
20 Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi: Niko kinyume dhidi ya hirizi ambazo mlizozitumia kuyakamata kwa hila maisha ya watu kana kwamba wamekuwa ndege. Naam, nitazichana kutoka kwenye mikono yenu; na wale watu mlio watega kama ndege-nitawaacha waende huru.
Wherefore thus saith the Lord GOD: Behold, I am against your cushions, wherewith ye hunt the souls as birds, and I will tear them from your arms; and I will let the souls go, even the souls that ye hunt as birds.
21 Nitavichana mbali vitambaa vya shela na kuwaokoa watu wangu kutoka kwenye mikono yangu, kwa hiyo hawatategwa tena kwenye mikono yenu. Mtajua kwamba mimi ni Yahwe.
Your pads also will I tear, and deliver My people out of your hand, and they shall be no more in your hand to be hunted; and ye shall know that I am the LORD.
22 Kwa sababu mmeuvunja moyo wa mtu mwenye haki kwa uongo, ingawa hata mimi sikutamani kuvunjwa kwake moyo, na kwa sababu mmemtia moyo badala yake matendo ya mtu mwovu ili kwamba asitaweze kurudi kutoka kwenye njia yake kuokoa maisha yake-
Because with lies ye have cowed the heart of the righteous, when I have not grieved him; and strengthened the hands of the wicked, that he should not return from his wicked way, that he be saved alive;
23 kwa hiyo hamtayaona tena maono ya uongo au kuendelea kufanya utabiri, kwa kuwa nitawaokoa watu wangu kutoka kwenye mkono wako. Nanyi mtajua kwamba mimi ni Yahwe.'”
therefore ye shall no more see vanity, nor divine divinations; and I will deliver My people out of your hand; and ye shall know that I am the LORD.'

< Ezekieli 13 >