< Ezekieli 11 >

1 Kisha Roho akaniacha juu na kunileta kwenye lango la mashariki la nyumba ya Yahwe, kuelekea mashariki, na tazama, kwenye njia ya mlango wa lango kulikuwa na watu ishirini na tano. Nikamwona Yaazania mwana wa Azuri na Pelatia mwana wa Benaya, viongozi wa watu, miongoni mwao.
Then a spirit lifted me up, and brought me unto the east gate of the LORD'S house, which looketh eastward; and behold at the door of the gate five and twenty men; and I saw in the midst of them Jaazaniah the son of Azzur, and Pelatiah the son of Benaiah, princes of the people.
2 Mungu akanambia, “Mwana wa adamu, hawa ndio wale watu walioshauri udhalimu, na kuamua mipango miovu kwenye huu mji.
And He said unto me: 'Son of man, these are the men that devise iniquity, and that give wicked counsel in this city;
3 Wakisema, 'Mda wa kujenga nyumba sio sasa; huu mji ni sufuria, na sisi ni nyama.'
that say: The time is not near to build houses! this city is the caldron, and we are the flesh.
4 Kwa hiyo tabiri juu yao. Tabiri, mwana wa adamu.”'
Therefore prophesy against them, prophesy, O son of man.'
5 Kisha Roho wa Yahwe akanijaza na akaniambia, “akisema: Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: kama usemavyo, nyumba ya Israeli; kwa kuwa najua kinachoendelea kwenye fikra zenu.
And the spirit of the LORD fell upon me, and He said unto me: 'Speak: Thus saith the LORD: Thus have ye said, O house of Israel; for I know the things that come into your mind.
6 Mmewazidisha watu mliowaua kwenye huu mji na kuijaza mitaa kwa hao.
Ye have multiplied your slain in this city, and ye have filled the streets thereof with the slain.
7 Kwa hiyo, Bwana Yahwe asema hivi: Wale watu milowaua, ambao mmeilaza miili yao kati ya Yerusalemu, ni nyama, na huu mji ni sufuria. Lakini mnaenda kutolewa nje kutoka kati ya huu mji.
Therefore thus saith the Lord GOD: Your slain whom ye have laid in the midst of it, they are the flesh, and this city is the caldron; but ye shall be brought forth out of the midst of it.
8 Mmeuogopa upanga, kwa hiyo nauleta huo upanga juu yenu-huu ndio usemi wa Bwana Yahwe.
Ye have feared the sword; and the sword will I bring upon you, saith the Lord GOD.
9 Nitawatoa nje kutoka kati ya mji, na kuwaweka kwenye mikono ya wageni, kwa kuwa nitaleta hukumu dhidi yenu.
And I will bring you forth out of the midst thereof, and deliver you into the hands of strangers, and will execute judgments among you.
10 Mtaanguka kwa upanga. Nitawahukumu kati ya mipaka ya Israeli hivyo mtajua yakwamba mimi ni Yahwe.
Ye shall fall by the sword: I will judge you upon the border of Israel; and ye shall know that I am the LORD.
11 Huu mji hautakua sufuria yenu ya kupikia, wala hamtakuwa nyama ndani yake. Nitawahukumu kati ya mipaka ya Israeli.
Though this city shall not be your caldron, ye shall be the flesh in the midst thereof; I will judge you upon the border of Israel;
12 Kisha mtajua yakwamba mimi ni Yahwe, yule ambaye hamuishe kwenye amri zake na ambaye hamkuzishika sheria zake. Badala yake, mmebeba hukumu za mataifa wanayowazunguka.”
and ye shall know that I am the LORD; for ye have not walked in My statutes, neither have ye executed Mine ordinances, but have done after the ordinances of the nations that are round about you.'
13 Ikawa kwamba nilipokuwa natabiri, Pelatia mwana wa Benaya, akafa. Hivyo nikaanguka kwenye uso wangu na kulia kwa sauti na kusema, “Ee, Bwana Yahwe, Je utayaharibu kabisa mabaki ya Israeli?”
And it came to pass, when I prophesied, that Pelatiah the son of Benaiah died. Then fell I down upon my face, and cried with a loud voice, and said: 'Ah Lord GOD! wilt Thou make a full end of the remnant of Israel?'
14 Neno la Yahwe likanijia, likisema,
And the word of the LORD came unto me, saying:
15 “Mwana wa adamu, ndugu zako! Ndugu zako! Watu wa ukoo wako na nyumba yote ya Israeli! Wote hao ndio hao ambao inasemekana wale wanaoishi Yerusalemu, 'Wako mbali sana kutoka kwa Yahwe! Hii nchi tulipewa sisi kama milki yetu.'
'Son of man, as for thy brethren, even thy brethren, the men of thy kindred, and all the house of Israel, all of them, concerning whom the inhabitants of Jerusalem have said: Get you far from the LORD! unto us is this land given for a possession;
16 Kwa hiyo sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: kote nimewapitisha mbali kati ya mataifa, na kote nimewasambaza kati ya nchi, bado nimekuwa patakatifu kwa ajili yao kwa mda kidogo kwenye nchi ambazo walizoenda.'
therefore say: Thus saith the Lord GOD: Although I have removed them far off among the nations, and although I have scattered them among the countries, yet have I been to them as a little sanctuary in the countries where they are come;
17 Kwa hiyo sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Nitawakusanya kutoka kwa watu, na kuwakutanisha kutoka kwenye nchi mlizokuwa mmetawanyika, na nitawapatia nchi ya Israeli.'
therefore say: Thus saith the Lord GOD: I will even gather you from the peoples, and assemble you out of the countries where ye have been scattered, and I will give you the land of Israel.
18 Kisha wataenda huko na kuondoa kila kitu chenye karaha na kila chukizo kutoka hiyo sehemu.
And they shall come thither, and they shall take away all the detestable things thereof and all the abominations thereof from thence.
19 Nitawapatia moyo mmoja, na nitaweka roho mpya kati yao. Nitaondoa moyo wa jiwe kutoka kwenye miili wao na kuwapatia moyo wa nyama,
And I will give them one heart, and I will put a new spirit within you; and I will remove the stony heart out of their flesh, and will give them a heart of flesh;
20 ili kwamba waweze kutembea kwenye amri zangu, watayachukua maagizo yangu na kuyatenda. Kisha watakuwa watu wangu, na nitakuwa Mungu wao.
that they may walk in My statutes, and keep Mine ordinances, and do them; and they shall be My people, and I will be their God.
21 Lakini kwa wale watembeao kwa kujifanya kuendeleza mambo yao ya karaha na machukizo yao, nitaleta tabia yao kwenye vichwa vyao-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
But as for them whose heart walketh after the heart of their detestable things and their abominations, I will bring their way upon their own heads, saith the Lord GOD.'
22 Makerubi wakainua mabawa yao na magurudumu yaliyokuwa karibu nao, na utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.
Then did the cherubim lift up their wings, and the wheels were beside them; and the glory of the God of Israel was over them above.
23 Kisha utukufu wa Yahwe ukaenda juu kutoka katikati ya mji na kusimama kwenye mlima hata mashariki mwa mji.
And the glory of the LORD went up from the midst of the city, and stood upon the mountain which is on the east side of the city.
24 Roho akanichukua juu na kunileta hata Ukaldayo, hata uhamishoni, katika maono kutoka kwa Roho wa Mungu, na maono niliyokuwa nimeyaona yakaenda juu yakaniacha.
And a spirit lifted me up, and brought me in the vision by the spirit of God into Chaldea, to them of the captivity. So the vision that I had seen went up from Me.
25 Kisha nikawaambia wale watumwa mambo yote ya Yahwe niliyokuwa nimeyaona.
Then I spoke unto them of the captivity all the things that the LORD had shown me.

< Ezekieli 11 >