< Mhubiri 6 >

1 Kuna ubaya ambao nimeuona chini ya jua, na ni mbaya kwa watu.
There is an evil which I have seen under the sun, and it is abundant with man:
2 Mungu anaweza kumpa mtu mali na utajiri na heshima kwa kiasi kwamba hakosi chochote anachokitamani mwenyewe, lakini kisha hampi uwezo wa kukifurahia. Badala yake mtu mwingine hutumia vitu vyake. Huu ni mvuke, teso baya.
a man to whom God shall give wealth, and substance, and honour, and he wants nothing for his soul of all things that he shall desire, yet God shall not give him power to eat of it, for a stranger shall devour it: this is vanity, and an evil infirmity.
3 Kama mtu akizaa watoto mia moja na kuishi miaka mingi, ili kwamba siku za miaka yake ni nyingi, lakini kama moyo wake hautosheki kwa mema na hazikwi kwa heshima, kisha ninasema kwamba, mtoto aliyezaliwa akiwa amekufa ni bora kuliko alivyo.
If a man beget a hundred [children], and live many years, yes, however abundant the days of his years shall be, yet [if] his soul shall not be satisfied with good, and also he have no burial; I said, An untimely birth is better than he.
4 Hata mtoto huyo amezaliwa bila faida na anapita katika giza, na jina lake linabaki limefichika.
For he came in vanity, and departs in darkness, and his name shall be covered in darkness.
5 Ingawa mtoto huyu haoni jua au kujua kitu chochote, ana pumziko ingawa mtu huyo hakupumzika.
Moreover he has not seen the sun, nor known rest: there is [no more rest] to this one than another.
6 Hata kama mtu akiishi miaka elfu mbili lakini hajifunzi kufuraia vitu vizuri, aenda sehemu moja kama mtu yeyote yule.
Though he has lived to the return of a thousand years, yet he has seen no good: do not all go to one place?
7 Ingawa kazi yote ya mtu ni kujaza mdomo wake, ila hamu yake haishibi.
All the labour of a man is for his mouth, and yet the appetite shall not be satisfied.
8 Hakika ni faida gani aliyo nayo mwenye hekima kuliko mpumbavu? Ni faida gani aliyo nayo masikini hata kama anajua jinsi ya kutenda mbele ya watu?
For [what] advantage has the wise man over the fool, since [even] the poor knows how to walk in the direction of life?
9 Ni bora kuridhika na kile ambacho macho hukiona kuliko kutamani kile ambacho hamu isiyo tulia inatamani, ambayo pia ni mvuke na kujaribu kuuchunga upepo.
The sight of the eyes is better than that which wanders in soul: this is also vanity, and waywardness of spirit.
10 Chochote ambacho kimekuwepo, tayari kimekwisha kupewa jina lake, na vile mtu alivyo ni kama tayari amekwisha fahamika. Hivyo imekuwa haifai kugombana na yule ambaye ni muhukumu mkuu wa wote.
If anything has been, its name has already been called: and it is known what man is; neither can he contend with him who is stronger than he.
11 Maneno mengi ambayo yanaongelewa, ndivyo yasiyo na maana yanaongezeka, kwa hiyo ni faida gani iliyopo kwa mwanadamu?
For there are many things which increase vanity.
12 Kwa kuwa ni nani ajuaye nini kilicho kizuri kwa mtu katika maisha yake wakati wa ubatili wake, siku zilizo hesabika ambazo kwa hizo anapita kama kivuri? Ni nina anayeweza kumwambia mtu kile kitakacho kuja chini ya jua baada ya kupita?
What advantage has a man? for who knows [what is] good for a man in his life, [during] the number of the life of the days of his vanity? and he has spent them as a shadow; for who shall tell a man what shall be after him under the sun?

< Mhubiri 6 >