< Mhubiri 3 >

1 Kwa kuwa kila kitu na wakati wake, na majira kwa kila kusudi chini ya mbingu.
To all things there is a time, and a season for every matter under heaven.
2 Kuna wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa, wakati wa kupanda na wakati wa kung'oa yaliyopandwa,
A time of birth, and a time to die; a time to plant, and a time to pluck up what has been planted;
3 wakati wa kuua na wakati wa kuponya, wakati wa kubomo na wakati wa kujenga.
a time to kill, and a time to heal; a time to pull down, and a time to build up;
4 Kuna wakati wa kulia na wakati wa kucheka, wakati wa kuomboleza na wakati kucheza,
a time to weep, and a time to laugh; a time to lament, and a time to dance;
5 wakati wa kutupa mawe na wakati wa kukusanya mawe, wakati wa kukumbatia watu wengine wakati wa kutokumbatia.
a time to throw stones, and a time to gather stones together; a time to embrace, and a time to abstain from embracing;
6 Kuna wakati wa kutafuta vitu na wakati wa kutotafuta, wakati wa kutunza vitu na wakati wa kuvitupa,
a time to seek, and a time to lose; a time to keep, and a time to cast away;
7 wakati kuchana mavazi na wakati wa kuyashona, wakati wa kunyamaza na wakati wa kuzungumza.
a time to rend, and a time to sew; a time to be silent, and a time to speak;
8 Kuna wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia, wakati wa vita na wakati wa amani.
a time to love, and a time to hate; a time of war, and a time of peace.
9 Ni faida gani mfanyakazi aipatayo katika kazi yake?
What advantage [has] he that works in those things wherein he labours?
10 Nimeona kazi ambayo Mungu amewapa wanadamu kuitimiza.
I have seen all the trouble, which God has given to the sons of men to be troubled with.
11 Mungu amefanya kila kitu kufaa kwa wakati wake. Pia ameweka umilele ndani ya mioyo yao. Lakini mwanadamu hawezi kuelewa matendo ambayo Mungu ameyafanya, tangu mwanzo wao hadi mwisho.
All the things which he has made are beautiful in his time: he has also set the whole world in their heart, that man might not find out the work which God has wrought from the beginning even to the end.
12 Ninajua kuwa hakuna kilicho bora kwa mtu yeyote kuliko kufurahi na kutenda mema maadamu anaishi-
I know that there is no good in them, except [for a man] to rejoice, and to do good in his life.
13 na kwamba kila mmoja anapaswa ale na kunywa na anapaswa kuelewa jinsi ya kufurahia mazuri ambayo yanatoka katika kazi zake zote. Hii ni zawadi kutoka kwa Mungu.
Also [in the case of] every man who shall eat and drink, and see good in all his labour, [this] is a gift of God.
14 Ninajua kwamba chochote afanyacho Mungu kinadumu milele. Hakuna kinaweza kuongezwa au kuondolea, kwa sababu Mungu ndiye aliyekifanya, ili kwamba watu wamsogelee kwa heshima.
I know that whatever things God has done, they shall be for ever: it is impossible to add to it, and it is impossible to take away from it: and God has done [it], that [men] may fear before him.
15 Chochote kilichopo kimekwisha kuwepo; chochote kitakachokuwepo kimekwisha kuwepo. Mungu huwafanya wanadamu kutafuka vitu vilivyjificha.
That which has been is now; and whatever things [are appointed] to be have already been; and God will seek out that which is past.
16 Na nimeona kwamba chini ya jua ubaya upo mahali palipopaswa kuwa na haki, na sehemu ya haki mara nyingi ina ubaya.
And moreover I saw under the sun the place of judgement, there was the ungodly one; and the place of righteousness, there was the godly one.
17 Nikasema moyoni mwangu, “Mungu atahukumu mwenye haki na mbaya kwa wakati muafaka kwa kila jambo na kila tendo.
And I said in my heart, God will judge the righteous and the ungodly: for there is a time there for every action and for every work.
18 Nikasema moyoni mwangu, “Mungu huwajaribu wanadamu kuwaonyesha kwamba wao ni kama wanyama.”
I said in my heart, concerning the speech of the sons of man, God will judge them, and that to show that they are breasts.
19 Kwa kuwa mwisho watoto wa wanadamu na mwisho wa wanyama ni sawa. Kifo cha mmoja ni sawa na kifo cha mwingine. Wote wana pumzi sawa. Hakuna faida kwa mwanadamu zaidi ya wanyama. Kwa kuwa hakuna kila kitu isipokuwa pumzi?
Also to them is the event of the sons of man, and the event of the brute; one event befalls them: as is the death of the one, so also the death of the other; and there is one breath to all: and what has the man more than the brute? nothing; for all is vanity.
20 Kila kitu kinaenda sehemu moja. Kila kitu kinatoka mavumbini, na kila kitu kinarudi katika mavumbini.
All [go] to one place; all were formed of the dust, and all will return to dust.
21 Ni nani ajuaye kama roho ya mwanadamu inaenda juu na roho ya wanyama inaenda chini ya nchi?
And who has seen the spirit of the sons of man, whether it goes upward? and the spirit of the beast, whether it goes downward to the earth?
22 kwa hiyo tena nikatambua kwamba hakuna lililo jema kwa yeyote zaidi ya kufurahia kazi yake, kwa kuwa hilo ndilo jukumu lake. Ni nani awezaye kumleta tena kuona kinachotokea baada yake?
And I saw that there was no good, but that wherein a man shall rejoice in his works, for it is his portion, for who shall bring him to see any thing of that which shall be after him?

< Mhubiri 3 >