< Torati 6 >

1 Sasa haya ni maagizo, amri, na sheria ambazo Yahwe Mungu wetu ameniamuru mimi kuwafundisha ninyi, ili kwamba muweze kuzishika katika nchi ambayo mnaenda ng'ambo ya pili ya Yordani kumiliki,
Now this is the mitzvot ·instructions·, the statutes, and the judgments, which Adonai your God enjoined to teach you, that you might do them in the land where you go over to possess it;
2 ili kwamba mpate kumheshimu Yahwe wenu, ili muzishike amri zake zote na maagizo ninayowaamuru-ninyi, wana wenu na wana wa wana wenu, siku zenu zote za maisha, ili kwamba siku zenu ziongezeke.
that you might fear Adonai your God, to keep all his statutes and his mitzvot ·instructions·, which I enjoin you; you, and your son, and your son’s son, all the days of your life; and that your days may be prolonged.
3 Kwa hiyo wasikilizeni, Israeli, na kuzishika ili kwamba iweze kuwa vizuri kwenu, ili kusudi muweze kuzidi mno kwenye nchi itiririkayo maziwa na asali, kama Yahwe Mungu wa Baba zenu, amewaahidi atafanya.
Sh'ma ·Hear understand obey· therefore, Israel [God prevails], and observe to do it; that it may be well with you, and that you may increase mightily, as Adonai, the God of your fathers, has promised to you, in a land flowing with milk and honey.
4 Sikiliza, Israel: Yahwe Mungu wetu ni mmoja.
Sh'ma ·Hear obey·, Israel [God prevails]: Adonai is our God. Adonai is echad ·one, one unity·.
5 Mtampenda Yahwe Mungu wenu kwa moyo wenu wote, kwa roho zenu zote, na kwa akili zenu zote.
You shall 'ahav ·affectionately love· Adonai your God with all your heart, with all your soul, and with all your might.
6 Maneno ninayowaamuru ninyi leo yatakuwa katika moyo wenu;
These words, which I enjoin you today, shall be on your heart;
7 na mtayafundisha kwa bidii kwa watoto wenu, mtayazungumza wakati mkaapo katika nyumba zenu, wakati mlalapo, na wakati mwinukapo.
and you shall teach them diligently to your children, and shall talk of them when you sit in your house, and when you walk by the way, and when you lie down, and when you rise up.
8 Utazifunga kama ishara juu ya mkono wako, nayo yatakuwa utepe kati ya macho yako.
You shall bind them for a sign on your hand, and they shall be for frontlets between your eyes.
9 Utaziandika kwenye miimo ya mlango ya nyumba yako na kwenye malango.
You shall write them on the door posts of your house, and on your gates.
10 Wakati Yahwe Mungu wako akuleta kwenye nchi ambayo aliaapa kwa baba zako, Ibrahimu, Isaka, na Yakobo, kwamba angekupa, pamoja na miji mikubwa na mizuri ambayo hamkuijenga,
It shall be, when Adonai your God brings you into the land which he swore to your fathers, to Abraham [Father of a multitude], to Isaac [Laughter], and to Jacob [Supplanter], to give you, great and goodly cities, which you didn’t build,
11 na nyumba zilizojaa kila aina ya vitu vizuri ambavyo hamkuzifanya, visima ambavyo hamkuvichimba, mashamba na miti ya mizeituni ambayo hamkuipanda, mtakula na kutosheka-
and houses full of all good things, which you didn’t fill, and cisterns dug out, which you didn’t dig, vineyards and olive trees, which you didn’t plant, and you shall eat and be full;
12 basi iweni makini ili kwamba msije kumsahau Yahwe, aliyewaleta toka nchi ya Misri, toka nyumba ya utumwa.
then beware lest you forget Adonai, who brought you out of the land of Egypt [Abode of slavery], out of the house of bondage.
13 Mtamheshimu Yahwe Mungu wenu, yeye mtamwabudu, na mtaapa kwa jina lake.
You shall fear Adonai your God; and you shall abad ·serve· him, and shall swear by his name.
14 Hamtawaendea miungu mingine, miungu ya watu wanaowazunguka wote-
You shall not go after other deities, of the deities of the peoples who are around you;
15 kwa kuwa Yahwe Mungu wenu katikati yenu ni Mungu wa wivu- kama mtafanya, hasira ya Yahwe Mungu wenu atawasha dhidi yenu na atawaangamiza kutoka kwenye uso wa dunia.
for Adonai your God among you is a jealous God; lest the anger of Adonai your God be kindled against you, and he destroy you from off the face of the earth.
16 Hamtamjaribu Yahwe Mungu wenu kama mlivyomjaribu huko Massah.
You shall not tempt Adonai your God, as you tempted him in Massah [Testing].
17 Kwa bidii mtayashika maagizo ya Yahwe Mungu wenu, maagizo yake makini, na amri ambazo amewaamuru.
You shall diligently keep the mitzvot ·instructions· of Adonai your God, and his testimonies, and his statutes, which he has enjoined you.
18 Mtafanya kile kilicho sahihi na kizuri katika macho ya Yahwe, kwamba iwe vizuri kwenu, na kwamba muweze kuingia na kumiliki nchi nzuri ambayo Yahwe aliaapa kwa baba zenu,
You shall do that which is right and good in Adonai’s sight; that it may be well with you, and that you may go in and possess the good land which Adonai swore to your fathers,
19 kuwaondoa maadui zenu wote mbele zenu, kama Yahwe alivyosema.
to thrust out all your enemies from before you, as Adonai has spoken.
20 Wakati mwana wako auliza kwa wakati unaokuja, kusema,”Ni zipi amri za gano, sheria, na amri zingine ambazo Yahwe Mungu wetu alituamuru?
Some day when your child asks you in time to come, saying, “What do the testimonies, the statutes, and the judgments, which Yahweh Eloheikhem [Yahweh our God] has enjoined you mean?”
21 Basi utasema kwa mwana wako, tulikuwa watumwa wa Farao huko Misri, Yahwe alitutoa Misri kwa mkono wa uweza,
then you shall tell your child, “We were Pharaoh’s slaves in Egypt [Abode of slavery]. Adonai brought us out of Egypt [Abode of slavery] with a mighty hand;
22 na alionesha ishara na maajabu, makuu na makali, Misri kwa Farao, na kwa nyumba yake yote, mbele ya macho yenu,
and Adonai showed great and awesome signs and wonders on Egypt [Abode of slavery], on Pharaoh, and on all his house, before our eyes;
23 na alitutoa kutoka huko, ili kwamba atulete ndani, kutupa nchi ambayo aliaapa kwa baba zetu.
and he brought us out from there, that he might bring us in, to give us the land which he swore to our fathers.
24 Yahwe alituamuru daima kuzishika amri hizi, kumuogopa Yahwe Mungu wetu kwa uzuri wetu, ili kwamba atuweke hai, kama tulivyo leo.
Adonai enjoined us to do all these statutes, to fear Yahweh Eloheikhem [Yahweh our God], for our good always, that he might preserve us alive, as we are today.
25 Kama tutashika maagizo haya yote mbele ya Yahwe Mungu wetu kama alivyotuamuru, hii itakuwa haki yetu.
It shall be righteousness to us, if we observe to do all this mitzvot ·instructions· before Yahweh Eloheikhem [Yahweh our God], as he has enjoined us.”

< Torati 6 >