< Torati 6 >

1 Sasa haya ni maagizo, amri, na sheria ambazo Yahwe Mungu wetu ameniamuru mimi kuwafundisha ninyi, ili kwamba muweze kuzishika katika nchi ambayo mnaenda ng'ambo ya pili ya Yordani kumiliki,
Now this is the commandment, the statutes, and the ordinances, which Jehovah your God commanded to teach you, that you might do them in the land where you go over to possess it;
2 ili kwamba mpate kumheshimu Yahwe wenu, ili muzishike amri zake zote na maagizo ninayowaamuru-ninyi, wana wenu na wana wa wana wenu, siku zenu zote za maisha, ili kwamba siku zenu ziongezeke.
that you might fear Jehovah your God, to keep all his statutes and his commandments, which I command you, you, and your son, and your son's son, all the days of your life; and that your days may be prolonged.
3 Kwa hiyo wasikilizeni, Israeli, na kuzishika ili kwamba iweze kuwa vizuri kwenu, ili kusudi muweze kuzidi mno kwenye nchi itiririkayo maziwa na asali, kama Yahwe Mungu wa Baba zenu, amewaahidi atafanya.
Hear therefore, Israel, and observe to do it; that it may be well with you, and that you may increase mightily, as Jehovah, the God of your fathers, has promised to you, in a land flowing with milk and honey.
4 Sikiliza, Israel: Yahwe Mungu wetu ni mmoja.
Hear, Israel: Jehovah is our God, Jehovah is one.
5 Mtampenda Yahwe Mungu wenu kwa moyo wenu wote, kwa roho zenu zote, na kwa akili zenu zote.
And you shall love Jehovah your God with all your heart, and with all your soul, and with all your might.
6 Maneno ninayowaamuru ninyi leo yatakuwa katika moyo wenu;
These words, which I command you this day, shall be on your heart;
7 na mtayafundisha kwa bidii kwa watoto wenu, mtayazungumza wakati mkaapo katika nyumba zenu, wakati mlalapo, na wakati mwinukapo.
and you shall teach them diligently to your children, and shall talk of them when you sit in your house, and when you walk by the way, and when you lie down, and when you rise up.
8 Utazifunga kama ishara juu ya mkono wako, nayo yatakuwa utepe kati ya macho yako.
You shall bind them for a sign on your hand, and they shall be for symbols between your eyes.
9 Utaziandika kwenye miimo ya mlango ya nyumba yako na kwenye malango.
You shall write them on the door posts of your house, and on your gates.
10 Wakati Yahwe Mungu wako akuleta kwenye nchi ambayo aliaapa kwa baba zako, Ibrahimu, Isaka, na Yakobo, kwamba angekupa, pamoja na miji mikubwa na mizuri ambayo hamkuijenga,
It shall be, when Jehovah your God shall bring you into the land which he swore to your fathers, to Abraham, to Isaac, and to Jacob, to give you, great and goodly cities, which you did not build,
11 na nyumba zilizojaa kila aina ya vitu vizuri ambavyo hamkuzifanya, visima ambavyo hamkuvichimba, mashamba na miti ya mizeituni ambayo hamkuipanda, mtakula na kutosheka-
and houses full of all good things, which you did not fill, and cisterns dug out, which you did not dig, vineyards and olive trees, which you did not plant, and you shall eat and be full;
12 basi iweni makini ili kwamba msije kumsahau Yahwe, aliyewaleta toka nchi ya Misri, toka nyumba ya utumwa.
then beware lest you forget Jehovah, who brought you forth out of the land of Egypt, out of the house of bondage.
13 Mtamheshimu Yahwe Mungu wenu, yeye mtamwabudu, na mtaapa kwa jina lake.
You shall fear Jehovah your God; and you shall serve him only, and you shall cling to him, and take oaths by his name.
14 Hamtawaendea miungu mingine, miungu ya watu wanaowazunguka wote-
You shall not go after other gods, of the gods of the peoples who are around you;
15 kwa kuwa Yahwe Mungu wenu katikati yenu ni Mungu wa wivu- kama mtafanya, hasira ya Yahwe Mungu wenu atawasha dhidi yenu na atawaangamiza kutoka kwenye uso wa dunia.
for Jehovah your God in the midst of you is a jealous God; lest the anger of Jehovah your God be kindled against you, and he destroy you from off the face of the earth.
16 Hamtamjaribu Yahwe Mungu wenu kama mlivyomjaribu huko Massah.
Do not test Jehovah your God, as you tested him at Massah.
17 Kwa bidii mtayashika maagizo ya Yahwe Mungu wenu, maagizo yake makini, na amri ambazo amewaamuru.
You shall diligently keep the commandments of Jehovah your God, and his testimonies, and his statutes, which he has commanded you.
18 Mtafanya kile kilicho sahihi na kizuri katika macho ya Yahwe, kwamba iwe vizuri kwenu, na kwamba muweze kuingia na kumiliki nchi nzuri ambayo Yahwe aliaapa kwa baba zenu,
You shall do that which is right and good in the sight of Jehovah; that it may be well with you, and that you may go in and possess the good land which Jehovah swore to your fathers,
19 kuwaondoa maadui zenu wote mbele zenu, kama Yahwe alivyosema.
to thrust out all your enemies from before you, as Jehovah has spoken.
20 Wakati mwana wako auliza kwa wakati unaokuja, kusema,”Ni zipi amri za gano, sheria, na amri zingine ambazo Yahwe Mungu wetu alituamuru?
When your son asks you in time to come, saying, "What do the testimonies, the statutes, and the ordinances, which Jehovah our God has commanded you mean?"
21 Basi utasema kwa mwana wako, tulikuwa watumwa wa Farao huko Misri, Yahwe alitutoa Misri kwa mkono wa uweza,
then you shall tell your son, "We were Pharaoh's bondservants in Egypt: and Jehovah brought us out of Egypt with a mighty hand;
22 na alionesha ishara na maajabu, makuu na makali, Misri kwa Farao, na kwa nyumba yake yote, mbele ya macho yenu,
and Jehovah showed great and awesome signs and wonders on Egypt, on Pharaoh, and on all his house, before our eyes;
23 na alitutoa kutoka huko, ili kwamba atulete ndani, kutupa nchi ambayo aliaapa kwa baba zetu.
and he brought us out from there, that he might bring us in, to give us the land which he swore to our fathers.
24 Yahwe alituamuru daima kuzishika amri hizi, kumuogopa Yahwe Mungu wetu kwa uzuri wetu, ili kwamba atuweke hai, kama tulivyo leo.
Jehovah commanded us to do all these statutes, to fear Jehovah our God, for our good always, that he might preserve us alive, as at this day.
25 Kama tutashika maagizo haya yote mbele ya Yahwe Mungu wetu kama alivyotuamuru, hii itakuwa haki yetu.
It shall be righteousness to us, if we observe to do all this commandment before Jehovah our God, as he has commanded us."

< Torati 6 >