< Torati 17 >

1 Haupaswi kumtolea dhabihu Yahwe Mungu wako ng'ombe au kondoo aliye na kasoro au kitu chochote kibaya, kwa kuwa hiyo itakuwa chukizo kwa Yahwe Mungu wako.
گاو یا گوسفندی که در آن عیب یا هیچ چیز بد باشد، برای یهوه خدای خودذبح منما، چونکه آن، نزد یهوه خدایت مکروه است.۱
2 Kama kunapatikana miongoni mwenu, ndani ya malango ya mji wowote ambao Yahwe Mungu wenu anawapatia, mwanaume yoyote au mwanamke ambaye anafanya uovu mbele ya Yahwe Mungu wenu kuiharibu agano lake -
اگر در میان تو، در یکی از دروازه هایت که یهوه خدایت به تو می‌دهد، مرد یا زنی پیدا شودکه در نظر یهوه، خدایت، کار ناشایسته نموده، ازعهد او تجاوز کند،۲
3 yoyote ambaye ameenda na kuabudu miungu mingine na kuisujudia, wala jua, mwezi, au kati ya jeshi la mbinguni- hakuna chochote nimekuamuru,
و رفته خدایان غیر را عبادت کرده، سجده نماید، خواه آفتاب یا ماه یا هر یک از جنود آسمان که من امر نفرموده‌ام،۳
4 na kama ungeambiwa kuhusu hiki, au kama una mifugo- basi unapaswa kufanya uchunguzi wa makini. Kama ni kweli na hakika kwamba chukizo kama hilo limefanyika Israeli-
و از آن اطلاع یافته، بشنوی، پس نیکو تفحص کن. واینک اگر راست و یقین باشد که این رجاست دراسرائیل واقع شده است،۴
5 -basi utamleta huyo mwanaume au mwanamke, aliyefanya uovu huu, katika malango ya mji, kwamba mwanaume kabisa au mwanamke, na umponde huyo mtu mpaka kufa.
آنگاه آن مرد یا زن راکه این کار بد را در دروازه هایت کرده است، بیرون آور، و آن مرد یا زن را با سنگها سنگسار کن تابمیرند.۵
6 Kwa kinywa cha mashahidi wawili, au mashahidi watatu, itakuwa yeye anayepaswa kuuwawa; lakini kwa kinywa cha shahidi mmoja peke hatauwawa.
از گواهی دو یا سه شاهد، آن شخصی که مستوجب مرگ است کشته شود؛ از گواهی یک نفر کشته نشود.۶
7 Mkono wa mashahidi unapaswa kuwa wa kwanza kumuuwa, na badae mkono wa watu wote; na mtamuondoa muovu miongoni mwenu.
اولا دست شاهدان به جهت کشتنش بر او افراشته شود، و بعد از آن، دست تمامی قوم، پس بدی را از میان خود دورکرده‌ای.۷
8 Kama jambo linatokea ambalo ni gumu kwenu kufanya maamuzi- pengine swali la mauaji au kifo cha ajali, haki ya mtu mmoja na haki ya mtu mwingine, au swali moja la aina ya kuzulu kufanyika, au aina nyingine ya jambo-mambo ya utata ndani ya malango yenu, basi utapaswa kwenda kwenye eneo ambalo Yahwe Mungu wako atachagua kama patakatifu pake.
اگر در میان تو امری که حکم بر آن مشکل شود به ظهور آید، در میان خون و خون، و درمیان دعوی و دعوی، و در میان ضرب و ضرب، از مرافعه هایی که در دروازه هایت واقع شود، آنگاه برخاسته، به مکانی که یهوه، خدایت، برگزیند، برو.۸
9 Utapaswa kwenda kwa makuhani, wazao wa Lawi, na kwa mwamuzi atakayetumika kwa wakati huo; mtatafuta ushauri wao, na watawapa ninyi maamuzi.
و نزد لاویان کهنه و نزد داوری که در آن روزها باشد رفته، مسالت نما و ایشان تو رااز فتوای قضا مخبر خواهند ساخت.۹
10 Mnapaswa kufuata sheria mliyopewa, katika eneo Yahwe atachagua kama patakatifu pake. Mtakuwa makini kufanya kila kitu ambacho wanawaelekeza kufanya.
وبرحسب فتوایی که ایشان از مکانی که خداوندبرگزیند، برای تو بیان می‌کنند، عمل نما. وهوشیار باش تا موافق هر‌آنچه به تو تعلیم دهند، عمل نمایی.۱۰
11 Fuata sheria wanayowafundisha, na kufanya kulingana na maamuzi wanawapa. Msigeuke kutoka kwa kile wanawambia, kwa kulia au kushoto.
موافق مضمون شریعتی که به توتعلیم دهند، و مطابق حکمی که به تو گویند، عمل نما، و از فتوایی که برای تو بیان می‌کنند به طرف راست یا چپ تجاوز مکن.۱۱
12 Yeyote anayefanya kwa kiburi, kwa kutomsikiliza kuhani anayesimama kutumika mbele ya Yahwe Mungu wako, au kwa kutomsikiliza mwamuzi- huyu mtu atakufa; mtaweka mbali uovu kutoka Israeli.
و شخصی که از روی تکبر رفتار نماید، و کاهنی را که به حضوریهوه، خدایت، به جهت خدمت در آنجامی ایستد یا داور را گوش نگیرد، آن شخص کشته شود. پس بدی را از میان اسرائیل دور کرده‌ای.۱۲
13 Watu wote wanapaswa kusikia na kuogopa, na kutofanya kwa kiburi tena.
و تمامی قوم چون این را بشنوند، خواهندترسید و بار دیگر از روی تکبر رفتار نخواهندنمود.۱۳
14 Wakati mlipokuja kwenye nchi ambayo Yahwe Mungu anawapa, na wakati mnamiliki na kuanza kuishi ndani yake, na halafu unasema, 'Nitajiwekea mfalme juu yangu, kama mataifa yote yanayonizunguka mimi,'
چون به زمینی که یهوه، خدایت، به تومی دهد، داخل شوی و در آن تصرف نموده، ساکن شوی و بگویی مثل جمیع امتهایی که به اطراف منند پادشاهی بر خود نصب نمایم،۱۴
15 basi unapaswa kwa hakika kujiwekea mfalme juu yako mtu yeyote ambaye Yahwe atachagua. Unapaswa kujiweka kama mfalme juu yako mtu yeyote kutoka miongoni mwa ndugu zenu. Haupaswi kuweka mgeni, ambaye si ndugu yenu, juu yenu.
البته پادشاهی را که یهوه خدایت برگزیند برخود نصب نما. یکی از برادرانت را بر خود پادشاه بساز، و مرد بیگانه‌ای را که از برادرانت نباشد، نمی توانی بر خود مسلط نمایی.۱۵
16 Lakini hapaswi kuzidisha farasi kwa ajili yake, wala kusababisha watu kurudi Misri ili kwamba aweze kuzidisha farasi, kwa kuwa Yahwe alikwisha sema kwako, 'Unapaswa kuanzia sasa usirudi njia hiyo tena.'
لکن او برای خود اسبهای بسیار نگیرد، و قوم را به مصر پس نفرستد، تا اسبهای بسیار برای خود بگیرد، چونکه خداوند به شما گفته است بار دیگر به آن راه برنگردید.۱۶
17 Na hapaswi kuzidisha wake kwa ajili yake, ili kwamba moyo wake usigeuke kotoka kwa Yahwe; wala hapaswi sana kuzidisha kwa ajili yake fedha au dhahabu.
و برای خود زنان بسیار نگیرد، مبادا دلش منحرف شود، و نقره و طلا برای خودبسیار زیاده نیندوزد.۱۷
18 Wakati aketipo kwenye kiti cha enzi cha ufalme wake, anapaswa kuandika kwenye kitabu kwa ajili yake nakala ya sheria hii, kutoka kwenye sheria ambayo iko mbele ya makuhani, ambao ni Walawi.
و چون بر تخت مملکت خود بنشیند، نسخه این شریعت را از آنچه از آن، نزد لاویان کهنه است برای خود در طوماری بنویسد.۱۸
19 Kitabu kinapaswa kuwa na yeye, na anapaswa kusoma ndani yake kwa siku zake zote, ili kwamba aweze kujifunza kumheshimu Yahwe Mungu wako, ili kwamba ashike maneno yote ya sheria hii na amri hizi, kuzishika.
و آن نزد او باشد و همه روزهای عمرش آن را بخواند، تا بیاموزد که از یهوه خدای خود بترسد، و همه کلمات این شریعت و این فرایض را نگاه داشته، به عمل آورد.۱۹
20 Anapaswa kufanya hivi ili kwamba moyo wake usiinuliwe zaidi ya ndugu zake, na ili kwamba asigeuke mbali na amri, kwa kulia au kwa kushoto' kwa kusudi kwamba aweze kuzidisha siku zake katika ufalme wake, yeye na watoto wake, miongoni mwa Israel.
مبادا دل او بر برادرانش افراشته شود، و از این اوامر به طرف چپ یا راست منحرف شود، تا آنکه او وپسرانش در مملکت او در میان اسرائیل روزهای طویل داشته باشند.۲۰

< Torati 17 >