< Torati 10 >

1 Kwa wakati ule Yahwe alisema kwangu, 'Chonga mbao mbili za mawe kama zile za kwanza, na njoo kwangu huku juu ya mlima, na utengeneze sanduku la mbao.
At that time Jehovah said to me, "Cut two tablets of stone like the first, and come up to me onto the mountain, and make an ark of wood.
2 Nitaandika kwenye mbao maneno ambayo yalikuwa kwenye mbao za kwanza ulizozivunja, na utaziweka ndani ya sanduku.
I will write on the tables the words that were on the first tables which you broke, and you shall put them in the ark."
3 Basi nilitengeneza sanduku la mbao za mikaratusi, na nikachonga mbao mbili za mawe kwa zile za kwanza, na nikaenda juu ya mlima, nikiwa na mbao mbili mkononi mwangu.
So I made an ark of acacia wood, and cut two tablets of stone like the first, and went up onto the mountain, having the two tablets in my hand.
4 Aliandika kwenye mbao, kama maandishi ya kwanza, amri kumi ambazo Yahwe amesema nanyi kwenye mlima kutoka katikati mwa moto katika siku ya kusanyiko; ndipo Yahwe alilinipa mimi.
He wrote on the tables, according to the first writing, the ten commandments, which Jehovah spoke to you on the mountain out of the midst of the fire in the day of the assembly: and Jehovah gave them to me.
5 Niligeuka na kushuka chini kutoka mlimani, na kuweka mbao ndani ya sanduku nililokuwa nimetengeneza; hapo zilikaa, kama Yahwe alivyoniamuru.”
I turned and came down from the mountain, and put the tables in the ark which I had made; and there they are as Jehovah commanded me.
6 (Watu wa Israeli walisafiri kutoka Beerothi ya Bene Jaakan kwenda Moserathi. Huko Aaroni alikufa, na huko alizikwa; Eleazar, mwana wake, alitumika katika ofisi ya ukuhani kwenye nafasi yake.
(The children of Israel traveled from Beeroth Bene Jaakan to Moserah. There Aaron died, and there he was buried; and Eleazar his son ministered in the priest's office in his place.
7 Kutokea huko walisafiri kwenda Gudgodah, na kutoka Gudgodah kwenda Jotbathah, nchi yenye mikondo ya maji.
From there they traveled to Gudgodah; and from Gudgodah to Jotbathah, a land of brooks of water.
8 Kwa wakati huo Yahwe alichagua kabila la Lawi kubeba sanduku la agano la Yahwe, kusimama mbele ya Yahwe kumtumikia na kubariki watu kwa jina lake, kama ilivyo leo.
At that time Jehovah set apart the tribe of Levi, to bear the ark of the covenant of Jehovah, to stand before Jehovah to minister to him, and to bless in his name, to this day.
9 Kwa hiyo Lawi hawana sehemu wala urithi wa nchi pamoja na ndugu zake; Yahwe ni urithi wao, kama Yahwe Mungu wenu alizungumza naye)
Therefore Levi has no portion nor inheritance with his brothers; Jehovah is his inheritance, according as Jehovah your God spoke to him.)
10 “Nilibaki kwenye mlima kama ilivyokuwa mara ya kwanza, siku arobaini na usiku arobaini. Yahwe alinisikiliza wakati huo pia; Yahwe hakutaka kukuangamiza.
I stayed on the mountain, as at the first time, forty days and forty nights: and Jehovah listened to me that time also, and Jehovah would not destroy you.
11 Yahwe alisema nami, “Inuka, nenda mbele ya watu uwaongoze katika safari yao; wataingia na kumiliki nchi ambayo niliapa kwa mababu zao kuwapa.'
Jehovah said to me, "Arise, take your journey before the people; and they shall go in and possess the land, which I swore to their fathers to give to them."
12 Sasa, Israeli, Yahwe Mungu wenu ataka nini kwenu, isipokuwa hofu ya Yahwe Mungu wenu, kutembea katika njia zake zote, kumpenda yeye, na kumwabudu Yahwe Mungu wenu kwa moyo wenu wote na roho yenu yote.
Now, Israel, what does Jehovah your God require of you, but to fear Jehovah your God, to walk in all his ways, and to love him, and to serve Jehovah your God with all your heart and with all your soul,
13 Kuzishika amri za Yahwe, na maagizo ambayo ninawaamuru ninyi leo kwa ajili ya uzuri wenu?
to keep the commandments of Jehovah, and his statutes, which I command you this day for your good?
14 Tazama, kwa Yahwe Mungu wenu mbingu ni zake na mbingu za mbingu, dunia, vyote vilivyomo.
Look, to Jehovah your God belongs heaven and the heaven of heavens, the earth, with all that is in it.
15 Yahwe peke alichukua furaha kwa baba zenu ili kwamba awapende, na aliwachagua ninyi, wazao wao, baada yao, zaidi kuliko ya watu wengine wowote, kama afanyavyo leo.
Only Jehovah had a delight in your fathers to love them, and he chose their descendants after them, even you above all peoples, as at this day.
16 Kwa hiyo basi wataili govi la mioyo yao, na msiwe wakaidi tena.
Circumcise therefore the foreskin of your heart, and be no more stiff-necked.
17 Kwa kuwa Yahwe Mungu wenu, ni Mungu wa miungu na Bwana wa bwana, Mungu mkuu, mwenye nguvu na wakutisha, ambaye hapendelei yeyote na hapokei rushwa-
For Jehovah your God, he is God of gods, and Lord of lords, the great God, the mighty, and the awesome, who doesn't respect persons, nor takes reward.
18 Hutekeleza haki kwa yatima na wajane, na huonesha upendo kwa mgeni kwa kumpa chakula na mavazi.
He does execute justice for the fatherless and widow, and loves the foreigner, in giving him food and clothing.
19 Kwa hiyo basi mpende mgeni; kwa kuwa mlikuwa wageni kutoka nchi ya Misri.
Therefore love the foreigner; for you were foreigners in the land of Egypt.
20 Mtamche Yahwe Mungu wenu yeye mtamwabudu. Mtashikamana kwake, na kwa jina lake mtaapa.
You shall fear Jehovah your God; you shall serve him; and you shall cling to him, and you shall swear by his name.
21 Yeye ni sifa yenu, ni Mungu wenu, ambaye amefanya kwa ajili yenu haya mambo makuu na kutisha, ambayo macho yenu yameyaona.
He is your praise, and he is your God, who has done for you these great and awesome things, which your eyes have seen.
22 Baba zako walienda Misri kama watu sabini; sasa Yahwe Mungu wako amekufanya wewe kuwa wengi kama nyota za mbinguni.
Your fathers went down into Egypt with seventy persons; and now Jehovah your God has made you as the stars of the sky for multitude.

< Torati 10 >