< Amosi 8 >

1 Hiki ndicho ambacho bwana Yahwe amenionyesha. Tazama, kikapu cha matunda ya hari!
The Lord God showed me this: a basket of summer fruit.
2 Akasema, “Unaona nini, Amosi?” Nikasema, “Kikapu cha matunda ya hari.” Kisha Yahwe akanambia, “Mwisho umefika kwa watu wangu Israeli; sintowaumiza tena.
“What do you see, Amos?” he asked. I replied, “A basket of ripe summer fruit.” Then the Lord said to me: The time is ripe for my people Israel, I will no longer overlook their crimes.
3 Nyimbo za kwenye hekalu zitakuwa vilio. Katika siku hiyo-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe. Mizoga itakuwa mingi, katika kila sehemu wataitupa katika ukimya!”
The singing women in the palace will howl on that day, says the Lord: Corpses everywhere, thrown out in silence.
4 Lisikilizeni hili, ninyi mkanyagao maskini na kumuondoa fukara wa nchi.
Listen to this, you who trample on the needy, who oppress the poor of the earth,
5 wakisema, “Wakati mwezi mpya utakapoisha, hivyo tunaweza kuuza mazao tena? Wakati siku ya Sabato itakapoisha, ili kwamba tuuze ngano? Tutafanya kipimo kidogo na kuongeza bei, tukidanganya kwa mizani za udanganyifu.
saying: When will the feast of the new moon be over so that we may sell grain? And the sabbath ended so that we may offer wheat for sale? Reducing the measure and increasing the price, cheating with false scales,
6 Hivi ndivyo ambavyo tunaweza kuuza ngano mbaya, kununua fukara kwa fedha, na masikini kwa jozi moja ya kubadhi.”
mixing the sweepings in with the wheat. Then we can buy the poor for money, the needy for a pair of shoes.
7 Yahwe ameapa kwa fahari ya Yakobo, “Hakika sintoweza kusahau kazi zao hata moja.”
Now the Lord has taken an oath by the Pride of Jacob: I will never forget all their deeds!
8 Je nchi haitatetemeka kwa hili, na kila mmoja aishiye kuombolezea? Yote hayo yatainuka kama Mto Naili, nayo itataabika juu na kupwa tena, kama mto wa Misri.
Because of this won’t the land quake, and all its inhabitants mourn? Won’t the whole of it rise like the Nile, churn and subside like the Nile in Egypt?
9 “Itakuja siku ambayo -huu ndio usemi wa Bwana Yahwe- kwamba nitafanya jua litue wakati wa mchana, na nitaiweka giza dunia wakati wa mchana.
On that day, says the Lord God, I will make the sun set at noon and darken the earth in broad daylight.
10 Nitazigeuza sikukuu zenu kuwa maombolezo na nyimbo zenu zote kuwa masikitiko. Nitawafanya wote kuvaa nguo za magunia na kipara juu ya kila kichwa. Nitayafanya haya kama maombolezo kwa mwana pekee, na siku ya uchungu mwisho wake.
I will turn your feasts into mourning, all your songs into dirges. I will cause you to dress in sackcloth, every head shaved. I will make you mourn like you have lost your only son, all that happens will end in bitterness.
11 Tazama, siku zinakuja -asema Bwana Yahwe- wakati nitakapoleta njaa katika nchi, sio njaa ya mkate, wala kiu ya maji, ila kusikia maneno ya Yahwe.
The day is coming, says the Lord God, when I will send hunger in the land. Not a famine of bread or thirst for water, but for hearing the message of the Lord.
12 watatangatanga kutoka bahari hata bahari; watakimbia kutoka kaskazini kwenda magharibi kutafuta neno la Yahwe, lakini hawatalipata.
Then they will wander from sea to sea, from the north to the east, to seek a message from the Lord, but they will not find it.
13 Katika siku hiyo wanawali wazuri na wavulana watazimia kutokana na njaa.
In that day beautiful girls and strong young men will faint from thirst.
14 Wale waapao kwa dhambi ya Samaria wataanguka na hawatainuka tena.”
Those who take oaths by the shameful idol of Samaria, who swear, ‘As surely as your God lives, O Dan!’ and, ‘By the sacred way to Beer-sheba!’ – they will fall and never rise again.

< Amosi 8 >