< Amosi 6 >

1 Ole wao wanaostarehe katika Sayuni, na kwa wale ambao wameokoka katika nchi ya mlima wa Samaria, watu mashuhuri bora wa mataifa, ambao nyumba ya Israeli huja kwa ajili ya msaada!
Sorrow awaits who are carefree in Zion, overconfident on the mountain of Samaria! The elite of this, the best of nations, on whom the people of Israel rest their hopes!
2 Viongozi wenu husema, “Pita kwenda Kalne na mkatazame; kutoka huko nendeni hadi Hamathi, mji mkubwa; kisha nendeni chini hata Gathi ya Wapelestina. Je ni wabora kuliko falme zenu mbili? Je kuna mpaka mkubwa kuliko mpaka wenu?”
You say to the people: Cross over to Calneh and see, go from there to Hamath the great, then go down to Gath of the Philistines: Are they better than these kingdoms? Is their territory larger than yours?
3 Ole wao wale waiwekao siku ya majanga na kufanya ufalme kuwa kinyume kusogea karibu.
You push away all thoughts of the evil day, yet have instituted a rule of violence.
4 Wamelala juu ya vitanda vya pembe na kupumzika juu ya viti vyao. Wakala wana kondoo kutoka kwenye kundi na ndama kutoka kwenye zizi.
They lie on ivory couches, sprawl on their divans, eat choice lambs from the flock, and fattened calves from the stall.
5 Wanaimba nyimbo za kijinga kwenye muziki wa kinubi; wanatunga kwenye vyombo kama vya Daudi.
They idly sing to the sound of the lyre, thinking themselves songwriters like David,
6 Wanakunywa mvinyo kutoka kwenye bakuli na kujipaka mafuta wenyewe kwa mafuta ya marahamu, lakini hawahuzuniki juu ya mateso ya Yusufu.
they drink bowlfuls of wine, and anoint themselves with the finest of oil. But they do not grieve over the ruin of Joseph.
7 Hivyo sasa watakwenda utumwani pamoja na watumwa wakwanza, na kelele za hao waliojinyoosha zitapita.
Therefore now they must go into exile at the head of the captives, and hushed will be the revelry of the sprawlers.
8 “Mimi Bwana Yahwe, nimeapa kwa nafsi yangu -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo, Mungu wa majeshi, naizira fahari ya Yakobo; nachukia boma zake. Kwa hiyo nitautoa huo mji pamoja vyote vilivyomo humo.”
The Lord God, the Lord, the God of hosts, has sworn by himself: I abhor the pride of Jacob, I hate his palaces, therefore I will deliver up the city and all that is in it to their enemies.
9 Itakuja kuhusu kwamba kama kuna wanaume kumi waliobakia kwenye nyumba moja, watakufa.
If ten people remain in one house, then they will die.
10 Wakati ndugu wa mtu huyo atakapokuja kuchukua miili yao-yule ambaye awachomaye baada ya kuleta maiti katika nyumba-kama akisema kwa mtu katika nyumba, “Je kuna mtu yuko pamoja nawe?” Vipi kama yule akisema, “Hapana.” Kisha atasema, “Kaa kimya, kwa kuwa hatulitaja jina la Yahwe.”
When the uncle and another member of the family of a dead man come to carry the body out of the house for burial, they will call to someone in a corner of the house, ‘Any more there?’ and he will answer, ‘No’, and then he will add, ‘Be quiet!’ – for the name of the Lord must not be mentioned.
11 Tazama, Yahwe atatoa amri, na nyumba kubwa itapigwa kuwa vipande vipande, na nyumba ndogo kuwa na nyufa.
Look! The Lord is giving the command! He will smash the large house to bits, the small house into fragments.
12 Je farasi watakimbia juu ya mteremko wa miamba? Je mtu atalima huko na ng'ome? Bado mmegeuza haki kuwa sumu na tunda la haki kuwa uchungu.
Do horses gallop on crags? Does one plow the sea with oxen? Yet you turn justice into poison weed, and the fruit of righteousness into bitter wormwood.
13 Ninyi mnaofurahia juu ya Lo Debari, msemao, “Je hatukuchukua Karnaimu kwa nguvu zetu wenyewe?”
You who are so proud of capturing Lo-debar, who say, ‘Have we not by our own strength taken Karnaim for ourselves?’
14 Lakini tazama, nitainua juu yenu taifa, nyumba ya Israeli-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe, Mungu wa majeshi. Watawatesa ninyi kutoka Lebo Hamathi hata kijito cha Araba.”
I am now raising up against you, Israel, a nation, says the Lord, the God of hosts. They will oppress you, from the entrance of Hamath to the brook of the Arabah.

< Amosi 6 >