< Matendo 27 >

1 Ilipoamuliwa kwamba tunatakiwa tusafiri kwa maji kwenda Italia, walimkabidhi Paulo na wafungwa wengine kwa afisa mmoja wa jeshi la Kiroma aliyeitwa Julio, wa Kikosi cha Agustani.
Lorsqu'il fut décidé que nous ferions voile vers l'Italie, ils livrèrent Paul et quelques autres prisonniers à un centurion nommé Julius, de la troupe d'Auguste.
2 Tukapanda meli kutoka Adramitamu, ambayo ilikuwa isafiri kandokando ya pwani ya Asia. Hivyo tukaingia baharini. Aristaka kutoka Thesolanike ya Makedonia akaenda pamoja nasi.
Nous nous embarquâmes sur un navire d'Adramyttium, qui allait faire voile vers des lieux situés sur la côte d'Asie, Aristarque, Macédonien de Thessalonique, étant avec nous.
3 Siku iliyofuata tukatua nanga katika mji wa Sidoni, ambapo Julio alimtendea Paulo kwa ukarimu na akamruhusu kwenda kwa rafiki zake kupokea ukarimu wao.
Le lendemain, nous abordâmes à Sidon. Julius traita Paul avec bonté, et lui donna la permission d'aller chez ses amis pour se rafraîchir.
4 Kutoka hapo tukaenda baharini tukasafiri kuzunguka kisiwa cha Kipro ambacho kilikuwa kimeukinga upepo, kwa sababu upepo ulikuwa ukitukabili.
De là, nous prîmes la mer, sous le vent de l'île de Chypre, car les vents étaient contraires.
5 Baada ya kuwa tumesafiri katika maji yaliyo karibu na Kilikia na Pamfilia, tukaja Mira, mji wa Lisia.
Après avoir traversé la mer qui est au large de la Cilicie et de la Pamphylie, nous arrivâmes à Myra, ville de Lycie.
6 Pale yule afisa wa jeshi la Kiroma, akaikuta meli kutoka Alexandria ambayo ilikuwa isafiri kuelekea Italia. Akatupandisha ndani yake.
Là, le centurion trouva un navire d'Alexandrie qui faisait route vers l'Italie, et il nous fit monter à bord.
7 Baada ya kuwa tumesafiri polepole kwa siku nyingi na hatimaye tukawa tumefika kwa taabu karibu na Kinidas, upepo haukuturuhusu tena kuelekea njia hiyo, hivyo tukasafiri kandokando ya kivuli cha Krete tukiukinga upepo, mkabala na Salmone.
Après avoir navigué lentement pendant plusieurs jours, et être arrivés avec peine en face de Cnide, le vent ne nous permettant pas d'aller plus loin, nous naviguâmes sous le vent de la Crète, en face de Salmone.
8 Tukasafiri kandokando ya pwani kwa ugumu, mpaka tukafika mahali palipoitwa Fari Haveni ambayo iko karibu na mji wa Lasi.
Nous le longeâmes avec peine, et nous arrivâmes à un endroit appelé Havres de plaisance, près de la ville de Lasea.
9 Tulikuwa tumechukua muda mwingi sana, na muda wa mfungo wa Kiyahudi ulikuwa umepita pia, na sasa ilikuwa ni hatari kuendelea kusafiri. Hivyo Paulo akatuonya,
Comme beaucoup de temps s'était écoulé et que le voyage était devenu dangereux, parce que le jeûne était déjà passé, Paul les avertit
10 na kusema, “Wanaume, naona safari ambayo tunataka tuichukue itakuwa na madhara na hasara nyingi, siyo tu ya mizigo na meli, lakini pia ya maisha yetu.”
et leur dit: « Messieurs, je vois que le voyage se fera avec des dommages et des pertes considérables, non seulement pour la cargaison et le navire, mais aussi pour nos vies. »
11 Lakini afisa wa jeshi la Kiroma akamsikiliza zaidi bwana wake na mmiliki wa meli, kuliko mambo yale ambayo yalizungumzwa na Paulo.
Mais le centurion prêta plus d'attention au capitaine et au propriétaire du navire qu'aux paroles de Paul.
12 Kwa sababu bandari haikuwa sehemu rahisi kukaa wakati wa baridi, mabaharia wengi wakashauri tusafiri kutoka pale, ili kwa namna yoyote tukiweza kuufikia mji wa Foinike, tukae pale wakati wa baridi. Foinike ni bandari huko Krete, na inatazama kaskazini mashariki na kusini mashariki.
Comme le port n'était pas propice à l'hivernage, la plupart des gens conseillèrent de prendre la mer à partir de là, si tant est qu'ils puissent atteindre Phœnix et y passer l'hiver, qui est un port de Crète, regardant vers le sud-ouest et le nord-ouest.
13 Upepo wa kusini ulipoanza kuvuma polepole, mabaharia wakafikiri wamepata kile ambacho walikuwa wanakihitaji. Wakang'oa nanga na kusafiri kandokando ya Krete karibu na pwani.
Lorsque le vent du sud souffla doucement, supposant qu'ils avaient atteint leur but, ils levèrent l'ancre et naviguèrent le long de la Crète, près du rivage.
14 Lakini baada ya muda mfupi upepo mkali, ulioitwa Wa kaskazini mashariki, ukaanza kutupiga kutoka ng'ambo ya kisiwa.
Mais bientôt, un vent de tempête s'abattit sur le rivage, qu'on appelle Euroclydon.
15 Wakati meli ilipolemewa na kushindwa kuukabili upepo, tukakubaliana na hali hiyo, tukasafirishwa nao.
Le navire étant pris et ne pouvant faire face au vent, nous lui cédâmes et fûmes entraînés.
16 Tukakimbia kupitia ule upande uliokuwa unaukinga upepo wa kisiwa kiitwacho Kauda; na kwa taabu sana tulifanikiwa kuuokoa mtumbwi.
Courant sous le vent d'une petite île appelée Clauda, nous avons pu, avec difficulté, arrimer le bateau.
17 Baada ya kuwa wameivuta, walitumia kamba kuifunga meli. Waliogopa kwamba tungeweza kwenda kwenye eneo la mchanga mwingi la Syiti, hivyo wakashusha nanga na waliendeshwa kandokando.
Après l'avoir hissé, ils ont utilisé des câbles pour aider à renforcer le navire. Craignant de s'échouer sur les bancs de sable de Syrtis, ils abaissèrent l'ancre de mer et se laissèrent ainsi entraîner.
18 Tulipigwa kwa nguvu sana na dhoruba, hivyo siku iliyofuata mabaharia wakaanza kutupa mizigo kutoka melini.
Comme nous étions très éprouvés par la tempête, le lendemain, ils commencèrent à jeter des objets par-dessus bord.
19 Siku ya tatu, mabaharia wakaanza kuyatoa maji kwa mikono yao wenyewe.
Le troisième jour, ils jetèrent de leurs propres mains les agrès du navire.
20 Wakati ambapo jua na nyota hazikutuangazia kwa siku nyingi, bado dhoruba kubwa ilitupiga, na matumaini kwamba tungeokolewa yalitoweka.
Alors que, pendant plusieurs jours, ni le soleil ni les étoiles n'avaient brillé sur nous, et qu'aucune petite tempête ne nous pressait, tout espoir d'être sauvés s'envolait.
21 Baada ya kuwa wameenda muda mrefu bila chakula, hapo Paulo akasimama katikati ya mabaharia akasema, “Wanaume, mlipaswa mnisikilize, na tusingengo'a nanga kutoka Krete, ili kupata haya madhara na hasara.
Après qu'ils eurent été longtemps sans manger, Paul se leva au milieu d'eux et dit: « Messieurs, vous auriez dû m'écouter, et ne pas partir de Crète, pour avoir cette blessure et cette perte.
22 Na sasa nawafariji mjitie moyo, kwa sababu hakutakuwa upotevu maisha kati yenu, isipokuwa hasara ya meli tu.
Maintenant je vous exhorte à reprendre courage, car il n'y aura pas de perte de vie parmi vous, mais seulement celle du navire.
23 Kwa sababu usiku uliopita malaika wa Mungu, ambaye huyo Mungu mimi ni wake, na ambaye ninamwabudu pia - malaika wake alisimama pembeni mwangu
Car cette nuit s'est tenu près de moi un ange, appartenant au Dieu dont je suis et que je sers,
24 na kusema, “Usiogope Paulo. Lazima usimame mbele ya Kaisari, na tazama, Mungu katika wema wake amekupa hawa wote ambao wanasafiri pamoja nawe.
et qui m'a dit: « Ne crains pas, Paul. Tu dois te présenter devant César. Et voici que Dieu t'a accordé tous ceux qui naviguent avec toi.
25 Hivyo, wanaume, jipeni moyo, kwa sababu namwamini Mungu, kwamba itakuwa kama nilivyoambiwa.
C'est pourquoi, messieurs, réjouissez-vous! Car je crois en Dieu, et il en sera comme il m'a été dit.
26 Lakini lazima tuumie kwa kupigwa katika baadhi ya visiwa.”
Mais il faut que nous échouions sur une île. »
27 Ulipofika usiku wa kumi na nne, tulipokuwa tukiendeshwa huko na huko kwenye bahari ya Adratik, kama usiku wa manane hivi, mabaharia walifikiri kwamba wamekaribia nchi kavu.
Mais la quatorzième nuit étant arrivée, comme nous étions ballottés dans la mer Adriatique, vers minuit les marins supposèrent qu'ils approchaient de quelque terre.
28 Walitumia milio kupima kina cha maji na wakapata mita thelathini na sita, baada ya muda mfupi wakapima tena wakapata mita ishirini na saba.
Ils sondèrent et trouvèrent vingt brasses. Un peu plus tard, ils sondèrent de nouveau et trouvèrent quinze brasses.
29 Waliogopa kwanza tunaweza kugonga miamba, hivyo wakashusha nanga nne kutoka katika sehemu ya kuwekea nanga na wakaomba kwamba asubuhi ingekuja mapema.
Craignant que nous ne nous échouions sur un terrain rocheux, ils lâchèrent quatre ancres de la poupe, et souhaitèrent qu'il fasse jour.
30 Wale mabaharia walikuwa wanatafuta namna ya kuitelekeza ile meli na walizishusha majini boti ndogo ndogo za kuokolea maisha, na wakajifanya kwamba wanatupa nanga kutoka sehemu ya mbele ya boti.
Comme les matelots cherchaient à s'enfuir du navire et qu'ils avaient descendu la barque dans la mer, en prétendant qu'ils allaient jeter des ancres par la proue,
31 Lakini Paulo akamwambia yule askari wa jeshi la Kiroma na wale askari, “Hamuwezi kuokoka isipokuwa hawa watu wanabaki kwenye meli”.
Paul dit au centenier et aux soldats: « Si ceux-ci ne restent pas dans le navire, vous ne pouvez pas être sauvés. »
32 Kisha wale askari wakakata kamba za ile boti na ikaachwa ichukuliwe na maji.
Alors les soldats coupèrent les cordages de la barque et la laissèrent tomber.
33 Wakati mwanga wa asubuhi ulipokuwa unajitokeza, Paulo akawasihi wote angalau wale kidogo. Akasema, “Hii ni siku ya kumi na nne mnasuburi bila kula, hamjala kitu.
Comme le jour approchait, Paul les pria de prendre de la nourriture, en disant: « C'est aujourd'hui le quatorzième jour que vous attendez et que vous jeûnez, sans avoir rien pris.
34 Hivyo nawasihi mchukue chakula kidogo, kwa sababu hii ni kwa ajili ya kuishi kwenu; na hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea.
C'est pourquoi je vous prie de prendre de la nourriture, car c'est pour votre salut, car il ne périra pas un cheveu de vos têtes. »
35 Alipokwisha kusema hayo, akachukua mkate akamshukuru Mungu mbele ya macho ya kila mtu. Kisha akaumega mkate akaanza kula.
Lorsqu'il eut dit cela et pris du pain, il rendit grâces à Dieu en présence de tous; puis il le rompit et se mit à manger.
36 Kisha wote wakatiwa moyo na wao wakachukua chakula.
Alors tous se réjouirent, et ils prirent aussi de la nourriture.
37 Tulikuwa watu 276 ndani ya meli.
En tout, nous étions deux cent soixante-seize personnes sur le navire.
38 Walipokwisha kula vya kutosha, waliifanya meli nyepesi kwa kutupa ngano ndani ya bahari.
Lorsqu'ils eurent suffisamment mangé, ils allégèrent le navire et jetèrent le blé à la mer.
39 Ilipokuwa mchana, hawakuitambua nchi kavu, lakini wakaona sehemu ya nchi kavu iliyoingia majini iliyokuwa na mchanga mwingi. wakajadiliana kama wanaweza kuiendesha meli kuelekea hapo.
Le jour venu, ils ne reconnurent pas la terre, mais ils remarquèrent une certaine baie avec une plage, et ils décidèrent d'essayer d'y conduire le navire.
40 Hivyo wakazilegeza nanga wakaziacha baharini. Katika muda huo huo wakazilegeza kamba za tanga na wakaiinua sehemu ya mbele kuelekea kwenye upepo, hivyo wakaelekea kwenye hiyo sehemu ya mchanga mwingi.
Jetant les ancres, ils les laissèrent dans la mer, en même temps qu'ils détachaient les cordes du gouvernail. Ils hissent la voile d'avant au vent et se dirigent vers la plage.
41 Lakini wakaja mahali ambapo mikondo miwili ya maji inakutana, na meli ikaelekea mchangani. Na ile sehemu ya mbele ya meli ikakwama pale na haikuweza kutoka, lakini sehemu ya mbele ya meli ikaanza kuvunjika kwa sababu ya ukali wa mawimbi.
Mais arrivant à un endroit où deux mers se rencontraient, ils firent échouer le navire. La proue frappa et resta immobile, mais la poupe commença à se briser par la violence des vagues.
42 Mpango wa wale askari ulikuwa ni kuwaua wafungwa, ili kwamba hakuna ambaye angeogelea na kutoroka.
Le conseil des soldats était de tuer les prisonniers, afin qu'aucun d'eux ne pût se sauver à la nage.
43 Lakini yule askari wa jeshi la Kiroma alitaka kumwokoa Paulo, hivyo akausimamisha mpango wao; na akawaamuru wale ambao wanaweza kuogelea, waruke kutoka melini kwanza na waende nchi kavu.
Mais le centurion, voulant sauver Paul, les détourna de leur dessein, et ordonna que ceux qui savaient nager se jetassent les premiers par-dessus bord pour gagner la terre ferme;
44 Kisha wanaume wengine watafuata, wengine juu ya vipande vya mbao na wengine juu ya vitu vingine kutoka kwenye meli. Kwa njia hii ikatokea kwamba wote tutafika salama nchi kavu.
et que les autres suivissent, les uns sur des planches et les autres sur d'autres objets du navire. Tous se sauvèrent ainsi jusqu'à la terre ferme.

< Matendo 27 >