< Matendo 2 >

1 Ilipofika siku ya Pentekoste, wote walikuwa pamoja sehemu moja.
Le jour de la Pentecôte, ils étaient tous ensemble dans le même lieu.
2 Ghafla ikatokea muungurumo kutoka mbinguni kama upepo mkali. ukaijaza nyumba yote walimokuwa wameketi.
Tout à coup, il vint du ciel un bruit semblable au souffle d'un grand vent, et il remplit toute la maison où ils étaient assis.
3 Hapo zikawatokea ndimi, kama ndimi za moto zimegawanyika, zikawa juu yao kila mmoja wao.
Des langues semblables à des langues de feu apparurent et leur furent distribuées, et il y en eut une sur chacun d'eux.
4 Wao wote wakajazwa na Roho Mtakatifu na wakaanza kusema kwa lugha zingine, kama vile Roho alivyowajalia kusema.
Ils furent tous remplis de l'Esprit Saint et se mirent à parler d'autres langues, selon que l'Esprit leur donnait la faculté de parler.
5 Sasa walikuwapo wayahudi waliokuwa wanaishi Yerusalemu, wacha Mungu, kutoka kila taifa chini ya mbingu.
Or, il y avait à Jérusalem des Juifs, des hommes pieux, de toutes les nations qui sont sous le ciel.
6 Ngurumo hizi ziliposikiwa, kundi la watu likaja pamoja na wakiwa na wasiwasi kwa sababu kila mtu aliwasikia wakiongea kwa lugha yake mwenyewe.
Lorsque ce bruit se fit entendre, la foule s'assembla et fut déconcertée, car chacun les entendait parler dans sa propre langue.
7 waliduwaa na kushangazwa, wao walisema, “Kweli, hawa wote wanaoongea siyo Wagalilaya?
Ils étaient tous stupéfaits et s'étonnaient, se disant les uns aux autres: « Voici, tous ceux qui parlent ne sont-ils pas Galiléens?
8 Kwa nini sisi tunawasikia, kila mmoja katika lugha tulizozaliwa nazo?
Comment entendons-nous, chacun dans sa langue maternelle?
9 Waparthia na Wamedi na Waelamu, na hao waishio Mesopotamia, Uyahudi, na Kapadokia, na katika Ponto na Asia,
Parthes, Mèdes, Élamites, gens de Mésopotamie, de Judée, de Cappadoce, du Pont, d'Asie,
10 katika Frigia, Pamfilia, katika Misri, na sehemu ya Libya hata Kirene, na wageni kutoka Rumi,
de Phrygie, de Pamphylie, d'Égypte, des environs de Cyrène en Libye, des visiteurs de Rome, Juifs et prosélytes,
11 Wayahudi na waongofu, Wakrete na Waarabu, tunawasikia wakizungumza katika lugha zetu kuhusu kazi za uweza wa Mungu.”
Crétois et Arabes, nous les entendons parler dans nos langues des merveilles de Dieu. »
12 Wote walikuwa wameduwaa na kutatanishwa; walisemezana wao kwa wao, “Hii ina maana gani?”
Ils étaient tous stupéfaits et perplexes, se disant les uns aux autres: « Que signifie ceci? »
13 Lakini wengine walidhihaki wakisema, “Hawa wamejazwa kwa mvinyo mpya.”
D'autres, se moquant, disaient: « Ils sont remplis de vin nouveau. »
14 Lakini Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti, akawaambia, “Watu wa Yudea na wote mnaoishi hapa Yerusalemu, hili lijulikane kwenu, sikilizeni kwa makini maneno yangu.
Mais Pierre, debout avec les onze, éleva la voix et leur dit: « Hommes de Judée et vous tous qui habitez à Jérusalem, sachez ceci et écoutez mes paroles.
15 Watu hawa hawajalewa kama mnavyodhani, sababu saa hizi ni asubuhi saa tatu.
Car ceux-ci ne sont pas ivres, comme vous le supposez, puisque ce n'est que la troisième heure du jour.
16 Lakini hili lilikuwa limesemwa kupitia kwa nabii Yoeli:
Mais voici ce qui a été annoncé par le prophète Joël:
17 Itakuwa katika siku za mwisho; Mungu asema, nitamwaga Roho wangu kwa watu wote. Wana wenu na binti zenu watatoa unabii, vijana wenu wataona maono, na wazee wenu wataota ndoto.
« Il en sera ainsi dans les derniers jours, dit Dieu, que je répandrai mon Esprit sur toute chair. Vos fils et vos filles prophétiseront. Vos jeunes hommes auront des visions. Vos vieux hommes feront des rêves.
18 Vilevile juu ya watumishi wangu na watumishi wangu wa kike katika siku hizo, nitamwaga Roho wangu, nao watatabiri.
Oui, et sur mes serviteurs et sur mes servantes en ces jours-là, Je répandrai mon Esprit, et ils prophétiseront.
19 Nitaonesha maajabu juu angani na ishara chini duniani, damu, moto, na mafusho ya moshi.
Je ferai apparaître des merveilles dans le ciel en haut, et des signes sur la terre en dessous: du sang, du feu et des nuages de fumée.
20 Na jua litabadilishwa kuwa giza na mwezi kuwa damu, kabla haijaja siku kuu na ya ajabu ya Bwana.
Le soleil se changera en ténèbres, et la lune en sang, avant que le grand et glorieux jour du Seigneur n'arrive.
21 itakuwa ya kwamba kila mmoja ambaye huliitia jina la Bwana ataokoka.'
Quiconque invoquera le nom du Seigneur sera sauvé.
22 Watu wa Israeli, sikieni maneno haya: Yesu wa Nazareti, mwanadamu aliyethibitishwa na Mungu kwenu kwa matendo ya uweza na maajabu, na ishara ambazo Mungu kupitia Yeye katikati yenu, kama ninyi wenyewe mnavyojua-
« Hommes d'Israël, écoutez ces paroles! Jésus de Nazareth, homme approuvé par Dieu à vos yeux, par les miracles, les prodiges et les signes que Dieu a faits par lui au milieu de vous, comme vous le savez vous-mêmes,
23 Kwa sababu ya mpango uliokusudiwa tangu mwanzo, na maarifa ya Mungu, alitolewa, na ninyi, kwa mikono ya watu wahalifu, mlimsulibisha na kumuua,
lui qui, livré selon le dessein arrêté et la prescience de Dieu, a été pris par la main d'hommes sans loi, crucifié et tué,
24 ambaye Mungu alimwinua, akauondoa uchungu wa mauti kwake, kwasababu haikuwezekana kwake kumilikiwa na huo.
lui que Dieu a ressuscité, le délivrant du supplice de la mort, parce qu'il n'était pas possible qu'il fût retenu par elle.
25 Hivyo Daudi anasema kuhusu yeye, 'Nilimwona Bwana daima mbele ya uso wangu, yeye yuko mkono wangu wa kulia hivyo basi sitasogezwa.
Car David dit de lui, Je voyais le Seigneur toujours devant moi, car il est à ma droite, afin que je ne sois pas ébranlé.
26 Kwa hiyo moyo wangu ulikuwa na furaha na ulimi wangu ulifurahishwa. Pia mwili wangu utaishi katika ujasiri.
C'est pourquoi mon cœur s'est réjoui, et ma langue s'est réjouie. De plus, ma chair aussi habitera dans l'espérance,
27 Hutaiacha nafsi yangu iende kuzimu, wala hutaruhusu Mtakatifu wako kuona uozo. (Hadēs g86)
car tu ne laisseras pas mon âme dans le séjour des morts, vous ne permettrez pas non plus à votre Saint de voir la pourriture. (Hadēs g86)
28 Wewe umedhihirisha kwangu njia za uzima; utanifanya nijae furaha mbele ya uso wako.'
Tu m'as fait connaître les chemins de la vie. Tu me rempliras d'allégresse par ta présence ».
29 Ndugu, ninaweza kuzungumza kwenu kwa ujasiri kuhusu baba yetu Daudi: yeye alikufa na akazikwa, na kaburi lake liko pamoja nasi hata hivi leo.
« Frères, je peux vous dire librement du patriarche David, qu'il est mort et qu'il a été enseveli, et que son tombeau est encore parmi nous aujourd'hui.
30 Hivyo, alikuwa nabii na alijua kuwa Mungu alishaapa kwa kiapo kwake, kwamba ataweka mmoja katika uzao wake kwenye kiti cha enzi.
C'est pourquoi, étant prophète, et sachant que Dieu lui avait juré par serment que, du fruit de son corps, selon la chair, il susciterait le Christ pour qu'il s'asseye sur son trône,
31 Aliliona hili mapema, na akasema kuhusu ufufuo wa Kristo, 'wala alikuwa hakuachwa kuzimu, wala mwili wake haukuoza.' (Hadēs g86)
il a, prévoyant cela, parlé de la résurrection du Christ, afin que son âme ne restât pas dans le séjour des morts et que sa chair ne vît pas la pourriture. (Hadēs g86)
32 Huyu Yesu - Mungu alimfufua, ambaye sisi wote ni mashahidi.
Ce Jésus, Dieu l'a ressuscité, ce dont nous sommes tous témoins.
33 Kwa hiyo, akiwa ameinuliwa katika mkono wa kuume wa Mungu, na akiwa amepokea ahadi ya Roho Mtakatifu kutoka kwa Baba, yeye amemimina hii ahadi, ambaye ninyi mnaona na kusikia.
Étant donc élevé par la droite de Dieu, et ayant reçu du Père la promesse du Saint-Esprit, il a répandu ce que vous voyez et entendez maintenant.
34 Kwani Daudi hakupaa kwenda mbinguni, lakini anasema, 'BWANA alisema kwa Bwana wangu,
Car David n'est pas monté aux cieux, mais il dit lui-même, Le Seigneur a dit à mon Seigneur: « Assieds-toi à ma droite ».
35 “keti mkono wangu wa kulia, mpaka nitakapowafanya adui zako kigoda kwa ajili ya miguu yako.
jusqu'à ce que je fasse de vos ennemis un marchepied pour vos pieds. »
36 Kwa hiyo nyumba yote ya Israeli na ijue kwa hakika kwamba Mungu amemfanya Yeye kuwa Bwana na Kristo, huyu Yesu ambaye mlimsulibisha.”
« Que toute la maison d'Israël sache donc avec certitude que Dieu l'a fait à la fois Seigneur et Christ, ce Jésus que vous avez crucifié. »
37 Sasa waliposikia hivyo, wakachomwa katika mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, “Ndugu, tufanyeje?”
Ayant entendu cela, ils eurent le cœur brisé et dirent à Pierre et aux autres apôtres: « Frères, que ferons-nous? »
38 Na Petro akawaambia, “Tubuni na Mbatizwe, kila mmoja wenu, katika jina la Yesu Kristo kwa ajili ya msamaha wa dhambi zenu, na mtapokea zawadi ya Roho Mtakatifu.
Pierre leur dit: « Repentez-vous et soyez baptisés, chacun de vous, au nom de Jésus-Christ, pour le pardon des péchés, et vous recevrez le don du Saint-Esprit.
39 Kwani kwenu ni ahadi na kwa watoto wenu na kwa wale wote walioko mbali, watu wengi kwa kadri Bwana Mungu wetu atakavyowaita.”
Car la promesse est pour vous, pour vos enfants, et pour tous ceux qui sont au loin, en aussi grand nombre que le Seigneur notre Dieu voudra appeler à lui. »
40 Kwa maneno mengi alishuhudia na kuwasihi; alisema, “Jiokoeni mtoke katika kizazi hiki kiovu.”
Avec beaucoup d'autres paroles, il leur rendait témoignage et les exhortait en disant: « Sauvez-vous de cette génération perverse! »
41 Ndipo wakayapokea maneno yake na wakabatizwa, hapo wakaongezeka katika siku hiyo kama nafsi elfu tatu.
Alors ceux qui reçurent avec joie sa parole furent baptisés. En ce jour-là, il y eut environ trois mille âmes de plus.
42 Wakaendelea katika mafundisho ya mitume na ushirikiano, katika kuumega mkate na katika maombi.
Ils persévéraient dans l'enseignement des apôtres et dans la communion fraternelle, dans la fraction du pain et dans la prière.
43 Hofu ikaja juu ya kila nafsi, na maajabu mengi na ishara zikafanyika kupitia mitume.
La crainte s'empara de tous, et il se fit beaucoup de prodiges et de miracles par les apôtres.
44 Wote walioamini walikuwa pamoja na kuwa na vitu vyao kwa pamoja,
Tous ceux qui croyaient étaient ensemble, et avaient tout en commun.
45 na waliuza vitu na milki zao na kugawanya kwa wote kulingana na hitaji la kila mmoja.
Ils vendaient leurs biens et leurs propriétés, et les distribuaient à tous, selon les besoins de chacun.
46 Hivyo siku baada ya siku waliendelea wakiwa na lengo moja katika hekalu, na walimega mkate kwenye kaya, na walishiriki chakula kwa furaha na unyenyekevu wa moyo;
Chaque jour, persévérant d'un commun accord dans le temple, et rompant le pain dans les maisons, ils prenaient leur nourriture avec joie et simplicité de cœur,
47 walimsifu Mungu na wakiwa na kibali na watu wote. Bwana aliwaongeza siku kwa siku ambao walikuwa wakiokolewa.
louaient Dieu et avaient la faveur de tout le peuple. Le Seigneur ajoutait chaque jour à l'assemblée ceux qui étaient sauvés.

< Matendo 2 >