< 2 Timotheo 1 >

1 Paulo mtume wa Yesu Kristo kwa mapenzi ya Mungu, sawasawa na ahadi ya uzima ulio ndani ya Kristo Yesu,
Paul, apôtre de Jésus-Christ par la volonté de Dieu, selon la promesse de la vie qui est en Jésus-Christ,
2 kwa Timotheo mwana mpendwa: Neema, rehema na amani toka kwa Mungu Baba na Kristo Yesu Bwana wetu.
à Timothée, mon enfant bien-aimé: Grâce, miséricorde et paix, de la part de Dieu le Père et de Jésus-Christ notre Seigneur.
3 Ninamshukuru Mungu, ambaye ninamtumikia kwa nia njema kama walivyofanya baba zangu, ninapokumbuka daima katika maombi yangu. Usiku na
Je rends grâce à Dieu, que je sers comme mes ancêtres, avec une conscience pure. Comme je me souviens sans cesse de vous dans mes requêtes, nuit et jour
4 mchana ninatamani kukuona, ili kwamba nijawe na furaha. Ninayakumbuka machozi yako.
désirant vous voir, me souvenant de vos larmes, afin d'être rempli de joie;
5 Nimekuwa nikikumbushwa kuhusu imani yako halisi, ambayo hapo kwanza ilikaa kwa bibi yako Loisi na mama yako Yunisi. Na nina hakika ya kwamba imani hiyo inakaa ndani yako pia.
m'étant rappelé la foi sincère qui est en vous, qui a vécu d'abord en votre grand-mère Loïs et en votre mère Eunice et, j'en suis persuadé, en vous aussi.
6 Hii ndiyo sababu nakukumbusha kuchochea karama ya Mungu iliyomo ndani yako kwa njia ya kuwekewa mikono yangu.
C'est pourquoi je vous rappelle que vous devez stimuler le don de Dieu qui est en vous par l'imposition de mes mains.
7 Kwa kuwa Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na upendo na nidhamu.
Car Dieu ne nous a pas donné un esprit de crainte, mais de puissance, d'amour et de maîtrise de soi.
8 Kwa hiyo usiuonee haya ushuhuda kuhusu Bwana wetu, wala wangu mimi Paulo mfungwa wake. Bali ushiriki mateso kwa ajili ya injili sawasawa na uweza wa Mungu.
N'ayez donc pas honte du témoignage de notre Seigneur, ni de moi, son prisonnier, mais supportez la souffrance pour la Bonne Nouvelle, selon la puissance de Dieu,
9 Ni Mungu aliyetuokoa na kutuita kwa wito mtakatifu. Hakufanya hivi kulingana na kazi zetu bali kulingana na neema na mpango wake mwenyewe. Alitupatia mambo haya katika Kristo Yesu kabla ya nyakati kuanza. (aiōnios g166)
qui nous a sauvés et appelés par une vocation sainte, non selon nos œuvres, mais selon son dessein et sa grâce, qui nous ont été accordés en Jésus-Christ avant les temps éternels, (aiōnios g166)
10 Lakini sasa wokovu wa Mungu umekwishafunuliwa kwa kuja kwa mwokozi wetu Kristo Yesu. Ni Kristo aliyeikomesha mauti na kuleta uzima usiokoma kwa nuru ya injili.
mais qui ont été révélés maintenant par l'apparition de notre Sauveur, Jésus-Christ, qui a aboli la mort et mis en lumière la vie et l'immortalité par la Bonne Nouvelle.
11 Kwa sababu hiyo nilichaguliwa kuwa mhubiri, mtume na mwalimu.
C'est pour cela que j'ai été établi prédicateur, apôtre et docteur des païens.
12 Kwa sababu hii nateseka pia, lakini sioni haya kwa kuwa namjua yeye niliyekwisha kumuamini. Nina hakika kuwa yeye anaweza kukitunza kile nilichokikabidhi kwake hata siku ile.
C'est pourquoi je souffre aussi ces choses. Mais je n'ai pas honte, car je connais celui en qui j'ai cru, et je suis persuadé qu'il est capable de garder ce que je lui ai confié pour ce jour-là.
13 Ukumbuke mfano wa ujumbe wa uaminifu uliousikia toka kwangu, pamoja na imani na upendo ulio ndani ya Kristo Yesu.
Gardez le modèle des saines paroles que vous avez entendues de moi, dans la foi et la charité qui est en Jésus-Christ.
14 Yatunze Mambo mazuri aliyokukabidhi Mungu kupitia Roho Mtakatifu aishiye ndani yetu.
Ce bien qui vous a été confié, gardez-le par le Saint-Esprit qui habite en nous.
15 Unajua ya kuwa, wote waishio katika Asia waliniacha. Kwenye kundi hili wamo Figelo na Hemogene.
Vous savez que tous ceux qui sont en Asie se sont détournés de moi, dont Phygelus et Hermogène.
16 Bwana airehemu nyumba ya Onesiforo kwa kuwa mara nyingi aliniburudisha na hakuionea aibu minyororo yangu.
Que le Seigneur fasse miséricorde à la maison d'Onésiphore, car il m'a souvent rafraîchi, et n'a pas eu honte de ma chaîne,
17 Badala yake, alipokuwa Roma alinitafuta kwa bidii na akanipata.
mais, lorsqu'il était à Rome, il m'a cherché diligemment et m'a trouvé
18 Mungu amjalie kupata rehema kutoka kwake siku ile. Kama alivyonisaidia nilipokuwa Efeso, wewe wajua vyema.
(que le Seigneur lui accorde de trouver la miséricorde du Seigneur en ce jour); et en combien de choses il a servi à Éphèse, vous le savez très bien.

< 2 Timotheo 1 >