< 1 Timotheo 6 >

1 Wale wote walio chini ya nira kama watumwa wawachukulie mabwana zao kama wenye heshima zote, wanatakiwa kufanya hivyo ili jina la Mungu na mafundisho yasitukanwe.
Que tous ceux qui sont esclaves sous le joug considèrent leurs propres maîtres comme dignes de tout honneur, afin que le nom de Dieu et la doctrine ne soient pas blasphémés.
2 Watumwa wenye mabwana waaminio wasiwadharau kwa sababu wao ni ndugu. Badala yake, wawatumikie zaidi. Kwa sababu mabwana wanaosaidiwa kazi zao ni waamini na wanapendwa. Fundisha na kuyatangaza mambo haya.
Quant à ceux qui ont des maîtres croyants, qu'ils ne les méprisent pas parce qu'ils sont frères, mais qu'ils les servent, parce que ceux qui participent au bienfait sont croyants et bien-aimés. Enseignez et exhortez ces choses.
3 Iwapo mtu fulani anafundisha kwa upotovu na hayapokei maelekezo yetu yenye kuaminika, ambayo ni maneno ya Bwana wetu Yesu Kristo, iwapo hawalikubali fundisho liongozalo kwenye utauwa.
Si quelqu'un enseigne une autre doctrine et ne se conforme pas aux paroles saines, aux paroles de notre Seigneur Jésus-Christ, et à la doctrine qui convient à la piété,
4 Mtu huyo anajivuna na hajui chochote. Badala yake, ana vurugu na mabishano juu ya maneno. Maneno haya huzaa wivu, ugomvi, matukano, shuku mbaya,
c'est un vaniteux, qui ne sait rien, mais qui est obsédé par les discussions, les disputes et les querelles de mots, d'où viennent l'envie, les querelles, les insultes, les mauvais soupçons,
5 na vurugu za mara kwa mara kati ya watu wenye akili zilizoharibika. Wanaiacha kweli. Wanafikiri kwamba utauwa ni njia ya kuwa matajiri”
les frictions constantes de gens à l'esprit corrompu et dépourvus de vérité, qui pensent que la piété est un moyen de gain. Retirez-vous de telles personnes.
6 Sasa utauwa na kuridhika ni faida kubwa.
Mais la piété avec le contentement est un grand gain.
7 Kwa maana hatukuja na chochote duniani. Wala hatuwezi kuchukua chochote kutoka duniani.
Car nous n'avons rien apporté dans le monde, et nous ne pouvons certainement rien emporter.
8 Badala yake, tutosheke na chakula na mavazi.
Mais si nous avons de la nourriture et des vêtements, nous nous en contenterons.
9 Sasa hao watakao kuwa na mali huanguka katika majaribu, katika mtego. Huanguka katika upumbavu mwingi na tamaa mbaya, na katika kitu chochote kinachowafanya watu wazame katika maangamizi na uharibifu.
Mais ceux qui veulent s'enrichir tombent dans une tentation, un piège et beaucoup de convoitises insensées et nuisibles, telles qu'elles noient les hommes dans la ruine et la perdition.
10 Kwa kuwa kupenda fedha ni chanzo cha aina zote za uovu. Watu ambao hutamani hiyo, wamepotoshwa mbali na imani na wamejichoma wenyewe kwa huzuni nyingi.
Car l'amour de l'argent est une racine de toutes sortes de maux. Certains se sont égarés de la foi par leur cupidité, et se sont percés de nombreuses peines.
11 Lakini wewe mtu wa Mungu, yakimbie mambo hayo. Fuata haki, utauwa, uaminifu, upendo, usitahimilivu, na upole.
Mais toi, homme de Dieu, fuis ces choses, et poursuis la justice, la piété, la foi, l'amour, la persévérance et la douceur.
12 Piga vita vizuri vya imani. Shikilia uzima wa milele ulioitiwa. Ilikuwa ni kwa sababu hii kwamba ulitoa ushuhuda mbele ya mashahidi wengi kwa kile kilicho chema. (aiōnios g166)
Combats le bon combat de la foi. Saisissez la vie éternelle à laquelle vous avez été appelés, et vous avez confessé la bonne confession devant de nombreux témoins. (aiōnios g166)
13 Nakupa amri hii mbele za Mungu, anayesababisha vitu vyote kuishi, na mbele ya Yesu Kristo, aliyenena iliyo kweli kwa Pontio Pilato:
Je vous ordonne, devant Dieu qui donne la vie à toutes choses, et devant le Christ Jésus qui a rendu témoignage de la bonne confession devant Ponce Pilate,
14 itunze amri kwa ukamilifu, pasipo mashaka, hadi ujio wa Bwana wetu Yesu Kristo.
de garder le commandement sans tache, sans reproche, jusqu'à l'apparition de notre Seigneur Jésus-Christ,
15 Mungu atadhihirisha ujio wake kwa wakati sahihi- Mungu, Mbarikiwa, nguvu pekee, Mfalme anayetawala, Bwana anayeongoza.
qu'il montrera au moment opportun, lui qui est le chef béni et unique, le roi des rois et le seigneur des seigneurs.
16 Peke yake anaishi milele na akaaye katika mwanga usiokaribiriwa. Hakuna mtu awezaye kumwona wala awezaye kumtazama. Kwake iwe heshima na uweza wa milele. Amina. (aiōnios g166)
Lui seul a l'immortalité, demeurant dans une lumière inaccessible, que nul homme n'a vu ni ne peut voir, à qui appartiennent l'honneur et la puissance éternelle. Amen. (aiōnios g166)
17 Waambie matajiri katika ulimwengu huu wasijivune, na wasitumaini katika utajiri, ambao siyo wa uhakika. Badala yake, wanapaswa kumtumaini Mungu. Ambaye hutupatia utajiri wote wa kweli ili tufurahie. (aiōn g165)
Demande à ceux qui sont riches dans le siècle présent de ne pas s'enfler d'orgueil et de ne pas fonder leur espérance sur l'incertitude des richesses, mais sur le Dieu vivant, qui nous procure avec abondance tout ce dont nous pouvons jouir; (aiōn g165)
18 Waambie watende mema, watajirike katika kazi njema, wawe wakarimu, na utayari wa kutoa.
qu'ils fassent le bien, qu'ils soient riches en bonnes œuvres, qu'ils soient prêts à distribuer, disposés à partager;
19 Katika njia hiyo watajiwekea msingi mzuri kwa mambo yajayo, ili kwamba waweze kushika maisha halisi.
qu'ils se constituent un bon fondement pour le temps à venir, afin de pouvoir saisir la vie éternelle.
20 Timotheo, linda kile ulichopewa. Jiepushe na majadiliano ya kipumbavu na mabishano yenye kujipinga ambayo kwa kwa uongo huitwamaarifa.
Timothée, garde ce qui t'a été confié, en te détournant des vains discours et des oppositions de ce qu'on appelle faussement la connaissance,
21 Baadhi ya watu huyatangaza mambo haya, na hivyo wameikosa imani. Neema na iwe pamoja nawe.
dont quelques-uns font profession, et qui se sont ainsi égarés loin de la foi. Que la grâce soit avec vous. Amen.

< 1 Timotheo 6 >