< 2 Nyakati 8 >

1 Ikawa karibu ya mwisho wa miaka ishirini, kipindi ambacho Selemani alikuwa ameijenga nyumba ya Yahwe na ya kwake mwenye,
Después de 20 años, durante los cuales Salomón construyó la Casa de Yavé y su propio palacio,
2 kwamba Selemani akaiajenga miji ambayo Hiramu alikuwa amempa, na ndani yake akawaweka watu wa Israeli.
Salomón reedificó las ciudades que Hiram le entregó, y estableció en ellas a los hijos de Israel.
3 Selemani akauavamia Hamathzoba, akaushinda.
Después Salomón fue a Hamat de Soba y se apoderó de ella.
4 Akaijenga Tadmori katika nyika, na miji yote ya hazina, ambayo aliijenga katika Hamathi.
Reedificó también Tadmor en la región despoblada, y todas las ciudades de almacenamiento que edificó en Hamat.
5 Pia akaujenga Beth-horoni wa juu, na Beth-horoni wa chini, miji iliyozungushiwa kwa ukuta, malango, na makomeo.
Además reedificó la Bet-horón de arriba y la Bet-horón de abajo, ciudades fortificadas, con muros, puertas y barras.
6 Akaujenga Baalathi na miji yote ya hazina aliyoimiliki, na miji yote kwa ajili ya magari yake na miji kwa ajili ya wapanda farasi wake, na chochote alichotamani kujenga kwa ajili ya starehe zake katika Yerusalemu, katika Lebanoni, na katika nchi zote zilizokuwa chini ya utawala wake.
[Reedificó] Baalat, todas las ciudades de almacenamiento que Salomón tenía, todas las de los carruajes, las de los jinetes, todo lo que Salomón se propuso edificar en Jerusalén, el Líbano y toda la tierra que estaba bajo su dominio.
7 Kuhusu watu wengine wote ambao walikuwa wamesalia wa Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi, Wayebusi, ambao hawakuwa wa Israeli,
De todo el pueblo que quedó de los heteos, amorreos, ferezeos, heveos y jebuseos, quienes no eran de Israel,
8 watoto wao ambao waliachwa baada yao katika nchi, ambaoa watu wa Israeli hawakuwaangamiza—Selemani akawafanyisha kazi kwa nguvu, ndivyo walivyo hata leo.
cuyos descendientes quedaron después de ellos en la tierra, a quienes los hijos de Israel no expulsaron totalmente, Salomón los sometió a trabajos forzados hasta hoy.
9 Vile vile, Selemani hakuwafanyisha kazi kwa nguvu watu wa Israeli. Badala yake, wakawa wanajeshsi wake, maakida wake, wakuu wake, na maakida wa magari ya majeshi yake na wapanda farasi wake.
Pero Salomón no sometió a alguno de los hijos de Israel a servidumbre para su obra. Ellos eran hombres de guerra, sus capitanes escogidos, los comandantes de sus carruajes y jinetes.
10 Pia hawa walikuwa wakuu wa wakuu wakisimamia wasimamizi waliokuwa wa mfalme Selemani, walikuwa 250, waliowasimamia watu walioifanya kazi.
Estos eran los principales oficiales del rey Salomón. Eran 250 quienes ejercían autoridad sobre la gente.
11 Selemani akamleta binti Farao nje ya mji wa Daudi kwenye nyumba aaliyokuwa amemjengea, kwa maana alisema, “Mke wangu lazima asiishi kataika nyumba ya Daudi mfalme wa Israeli, kwa sababu kila linapokuja sanduku la Yahwe ni takatifu”.
Salomón llevó a la hija de Faraón de la Ciudad de David al palacio que construyó para ella, pues dijo: Mi esposa no vivirá en la Casa de David, rey de Israel, porque aquellas habitaciones en las que entró el Arca de Yavé son sagradas.
12 Kisha Selemani akatoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu yake ambayo alikuwa ametengeza mbele ya ukumbi.
Entonces Salomón ofreció holocaustos a Yavé sobre el altar de Yavé que edificó en el patio,
13 Akatoa sadaka kama ilivyohitaka katika ratiba ya kila siku; akazitoa, kwa kufuata maelekezo yaliyokuwa katika amari ya Musa, katika siku za Sabato, miezi mipya, na katika siku zilizopangwa mara tatu kila mwaka: Sikukuu ya mikate isiyochachwa, sikukuu ya majuma, na sikuku ya vibanda.
según lo prescrito para cada día por mandato de Moisés, para ofrecerlos los sábados, en las lunas nuevas y los tiempos señalados, y tres veces al año: en la fiesta de los Panes sin Levadura, la fiesta de Las Semanas y la fiesta de Las Cabañas.
14 Katika kuyatunza maagizo ya baba yake Daudi, Selemani akayapanga makundi ya makuhani kwenye kazi yao, na Walawi kwenye nafasi zao, ili kumsisfu Mungu na kuhudumu mbele za makuhani, kama ilivyotakiwa katika ratiba ya kila siku. Pia akawateua walinda lango kwa zamu zao kwa kila lango, kwa maana Daudi, mtu wa Mungu, alikuwa ameagiza hivyo pia.
También estableció las clases sacerdotales en sus servicios según la ordenanza de su padre David, a los levitas en sus funciones para alabar y ministrar ante los sacerdotes según lo prescrito para cada día, y los porteros para cada puerta según sus grupos, porque así lo ordenó David, varón de ʼElohim.
15 Watu hawa hawakupotea kutoka kwenye amri ya mfalme kwa makuhani na Walawi kuhusu jambo lolote, au kuhusu vyumba vya hazina.
No se apartaron del mandato del rey en cuanto a los sacerdotes y a los levitas en ningún asunto, incluso en el de los tesoros.
16 Kazi yote aliyoagizwa na Selemani ikakamilika, kutoka siku msingi wa nyumba ya Yahwe ulipowekwa hadi ilipokamilika. Nyumba ya Yahwe ikamalizika.
Toda la obra de Salomón fue ejecutada desde el día cuando los cimientos de la Casa de Yavé fueron puestos hasta acabarla. Y quedó terminada la Casa de Yavé.
17 Kisha Selemani akaenda Esion geberi, na Elothi, juu ya pwani katika nchi ya Edomu.
Entonces Salomón fue a Ezión-geber y Eilat, a la costa del mar en la tierra de Edom,
18 Hiramu akatuma meli zake kupitia watumishi wake ambao walikuwa wana maji wenye uzoefu. Wakasafiri na Selemani na watumishi wa Semani hadi Ofiri. Wakachukua kutoka huko talanta 450 za dhahabu ambazo walimletea Selemani.
porque Hiram envió por medio de sus esclavos naves y marineros diestros en el mar, quienes fueron con los esclavos de Salomón a Ofir. Tomaron de allá 14,8 toneladas de oro y los llevaron al rey Salomón.

< 2 Nyakati 8 >