< 2 Nyakati 33 >

1 Manase alikuwa na umri wa miaka kumi na mbili alipoanza kutawala, alitawala miaka hamsini na tano katika Yerusalemu.
A son of twelve years is Manasseh in his reigning, and fifty and five years he hath reigned in Jerusalem;
2 Akafanya yalikuwa uovu katika macho ya Yahwe, kama yalivyo mambo ya machukizo ya mataifa ambao Yahwe alikuwa amewafukuza mbele ya watu wa Israeli.
and he doth the evil thing in the eyes of Jehovah, like the abominations of the nations that Jehovah dispossessed from the presence of the sons of Israel,
3 Kwa maana alizijenga tena sehemu za juu ambazo baba yake Hezekia alikuwa amezibomoa, na akajenga madhabahu kwa ajili ya mabaali, akatengeneza sanaamu za Maashera, na akaziinamia chini nyota zote za mbinguni na kuziabudu.
and he turneth and buildeth the high places that Hezekiah his father hath broken down, and raiseth altars for Baalim, and maketh shrines, and boweth himself to all the host of the heavens, and serveth them.
4 Manase akajenga madhbahu za kipagani katika nyumba ya Yahwe, ingawa Yahwe alikuwa amemwamuru, “Ni katika Yerusalemu ambamo jina langu litawekwa milele”.
And he hath built altars in the house of Jehovah of which Jehovah had said, 'In Jerusalem is My name to the age.'
5 Alijenga madhabahu kwa ajili ya nyota zote za mbinguni katika vile viwanja viwili vya nyumba ya Yahwe.
And he buildeth altars to all the host of the heavens in the two courts of the house of Jehovah.
6 Katika bonde la Beni Hinomu akawaweka wanaye katika moto. Akafanya misemo ya ubashiri, na uchawi, akassoma utabiri; akashauriana na wale waliozungumza na wafu na wale waliozungumza na na roho. Akafanaya maaovu mengi katika mcho ya Yahwe na alimfanya Mungu akasirike.
And he hath caused his sons to pass over through fire in the valley of the son of Hinnom, and observed clouds and used enchantments and witchcraft, and dealt with a familiar spirit, and a wizard; he hath multiplied to do the evil thing in the eyes of Jehovah, to provoke him to anger.
7 Ile sanamu ya Maashera aliyokuwa amefanya, akaipeleka katika nyumba ya Mungu. Ni kuhusu nyumba hii ambayo Mungu alikuwa amesema kwa Daudi na Selemani mwanaye; alikuwa amesema, “Ni katika nyumba hii na katika Yerusalemu, ambao nimeuchangua kutoka makabila yote ya Israeli, kwamba nitaliweka jina langu milele.
And he placeth the graven image of the idol that he made in the house of God, of which God said unto David, and unto Solomon his son, 'In this house, and in Jerusalem that I have chosen out of all the tribes of Israel, I put My name to the age,
8 Sitawaondoa tena watu wa Israeli katina nchi hii ambayo niliitoa kwa babu zao, ikiwa tu watakuwa makini katika kuyashika yote niliyowaamuru, kuzishika sheria zangu, amri zangu, na sheria zangu nilizowapa kupitia Musa.”
and I add not to turn aside the foot of Israel from off the ground that I appointed to your fathers, only, if they watch to do all that I have commanded them — to all the law, and the statutes, and the ordinances by the hand of Moses.'
9 Manase akawaongoza Yuda na wakaaji wa Yerusalemu hata kufanya uovu zaidi kuliko hata watu wa mataifa ambao Yahwe alikuwa amewateketeza mbele za Israeli.
And Manasseh maketh Judah and the inhabitants of Jerusalem to err, to do evil above the nations that Jehovah destroyed from the presence of the sons of Israel.
10 Yahwe akasema kwa Manase, na kwa watu wake wote, lakini hawakumsikiliza.
And Jehovah speaketh unto Manasseh and unto his people, and they have not attended,
11 Kwa hiyo Yahwe akaleta juu yao maamri jeshsi wa jeshi la Ashuru, ambao walimchukua Manase katika minyonyoro, wakamfunga kwa pingu, na wakampeleka Babeli.
and Jehovah bringeth in against them the heads of the host that the king of Asshur hath, and they capture Manasseh among the thickets, and bind him with brazen fetters, and cause him to go to Babylon.
12 Manase alipokuwa katika dhika, alimuomba Yahwe, Mungu wake, na akajinyenyekesha sana mbele za Mungu wa babu zake.
And when he is in distress he hath appeased the face of Jehovah his God, and is humbled exceedingly before the God of his fathers,
13 Akaomba kwake; na Mungu akamsikiliza, na Mungu akasikia kuomba kwake na akamrudisha Yerusalemu, katika ufalme wake. Kisha Manase akafahamu kwamba Yahwe alikuwa Mungu.
and prayeth unto Him, and He is entreated of him, and heareth his supplication, and bringeth him back to Jerusalem, to his kingdom, and Manasseh knoweth that Jehovah — He [is] God.
14 Baada ya hayo, manase akajenga ukuta wa nje ya mji wa Daudi, upande wa magharibi wa Gihoni, katika bonde, hadi kwenye lango la Samaki. Akauzungushia mlima wa Ofeli na akaupandisha ukuta hadi usawa mrefu sana. Akaweka maamri jeshi jasiri katika ngome zote za miji ya Yuda.
And after this he hath built an outer wall to the city of David, on the west of Gihon, in the valley, and at the entering in at the fish-gate, and it hath gone round to the tower, and he maketh it exceeding high, and he putteth heads of the force in all the cities of the bulwarks in Judah.
15 Akaipeleka mbali miungu yote ya kigeni, akaondoa sanamu zote kwenye nyumba ya Yahwe, na madhabahu zote ambazo alikuwa amejenga juu ya mlima wa nyumba ya Yahwe na katika Yerusalemu, na kuvitupa nje ya mji.
And he turneth aside the gods of the stranger, and the idol, out of the house of Jehovah, and all the altars that he had built in the mount of the house of Jehovah and in Jerusalem, and casteth [them] to the outside of the city.
16 Akaijenga tena madhabahu ya Yahwe na juu yake akatoa sadaka za amani na sadaka za shukrani; akamwamuru Yuda amtumikie Yahwe, Mungu wa Israeli.
And he buildeth the altar of Jehovah, and sacrificeth upon it sacrifices of peace-offerings and thank-offering, and saith to Judah to serve Jehovah, God of Israel;
17 Hata hivyo watu bado walitoa sadaka mahali pa sehemu za juu, lakini kwa Yahwe, Mungu wao pekee.
but still the people are sacrificing in high places, only — to Jehovah their God.
18 Katika mambo mengine kuhusu Manase, maombi yake kwa Mungu wake, na maneno ya waonaji ambao walisema kwake katika jina la Yahwe, Mungu wa Israeli, tazama, yameandikwa miongoni mwa matendo ya wafalme wa Israeli.
And the rest of the matters of Manasseh, and his prayer unto his God, and the matters of the seers, those speaking unto him in the name of Jehovah, God of Israel, lo, they are [on the book of] the matters of the kings of Israel;
19 Katika matukio hayo kuna historia ya maombi yake, na jinsi Mungu alivyoguswa na maomabi hayo. Pia kuna kumbu kumbu ya dhambi zake zote na makosa yake, na sehemu ambako alikuwa amejenga sehemu za juu na kuzisimamisha Maashera na sanamu za kuchonga, kambla ya kujinyenyekesha mwenyewe — na imeandikwa kuhusu hayo katika tarehe ya waonaji. (Maandishi ya kale yanasema hivi, “tarehe ya Hozai,” ambayo ni maandishi ya kifungu asili. Lakini matoleo mengi ya kisasa yamesahihisha na kusomeka “tarehe ya waonaj” Pia, matoleo machache ya kisasa yanasema “tarehe ya waonaji”.).
and his prayer, and his entreaty, and all his sin, and his trespass, and the places in which he had built high places, and established the shrines and the graven images before his being humbled, lo, they are written beside the matters of Hozai.
20 Kwa hiyo Manase akalala na babu zake, na wakamzika katika nyumba yake mwenyewe. Amoni, mwaye, akawa mfalme katika nafasi yake.
And Manasseh lieth with his fathers, and they bury him in his own house, and reign doth Amon his son in his stead.
21 Amoni alikuwa na umri wa miaka ishirini na mbili alipoanza kutawala; alitawala miaka miwili katika Yerusalemu.
A son of twenty and two years [is] Amon in his reigning, and two years he hath reigned in Jerusalem,
22 Akafanya yaliyokuwa uovu katika macho ya Yaahwe, kama Manase, baba yake, alivyofanya. Amoni alitoa sadaka katika sanamau zote za kuchonga ambazo alitengeneza Manase baba yake, na aliziabudu.
and he doth the evil thing in the eyes of Jehovah, as did Manasseh his father, and to all the graven images that Manasseh his father had made hath Amon sacrificed, and serveth them,
23 Hakujinyenyekesha mbele za Yahwe, kama baba yake Manase alivyokuwa amefanya. Badala yake, Amoni huyu huyu alifanya makosa zaidi na zaidi.
and hath not been humbled before Jehovah, like the humbling of Manasseh his father, for Amon himself hath multiplied guilt.
24 Watumishi wake wakapanga njama wa zidi yake na wakamua katika nyumba yake mwenyewe.
And his servants conspire against him, and put him to death in his own house,
25 Lakini watu wa nchi wakawaua wote waliofanya njama zidi ya Mfalme Amoni, na wakamfanya Yosia, mwanaye, mfalme katika nafasi yake.
and the people of the land smite all those conspiring against king Amon, and the people of the land cause Josiah his son to reign in his stead.

< 2 Nyakati 33 >