< 2 Nyakati 16 >

1 Katika mwaka wa thelathini na sita wa utawala wa Asa, Baasha, mfalme wa Israeli, akatenda kwa ukatili dhidi ya Yuda na akaujenga Rama, ili kwamba asimruhusu mtu yeyote kutoka wala kuingia katika nchi ya Asa, mfalme wa Yuda.
In the thirty and sixth year of the reign of Asa, come up hath Baasha king of Israel, against Judah, and buildeth Ramah, so as not to permit any going out and coming in to Asa king of Judah.
2 Kisha Asa akaitoa fedha na dhahabu nje ya vyumba vya kuhifadhia katika nyumba ya Yahwe na nje ya nyumba ya mfalme, na akaituma kwa Ben Hadadi mfalme wa Aramu, ambaye aliishi Dameski. Akasema, pawe na agano kati yako na mimi, kama palivyokuwa na agano kati ya baba yangu na baba yako. Angalia, nimekutumia fedha na dhahabu.
And Asa bringeth out silver and gold from the treasures of the house of Jehovah, and of the house of the king, and sendeth unto Ben-Hadad king of Aram, who is dwelling in Damascus, saying,
3 Livunje agano lako na Baasha, mfalme wa Israeli, ili kwamba aniache.”
'A covenant [is] between me and thee, and between my father and thy father, lo, I have sent to thee silver and gold; go, break thy covenant with Baasha king of Israel, and he doth go up from off me.'
4 Ben Hadadi akamsikiliza mfalme Asa na kutuma maakida wa majeshsi dhidi ya miji ya Israeli. Wakavamia Iyoni, Dani, Abelimaimu, na miji yoye ya kuhifadhia ya Naftali.
And Ben-Hadad hearkeneth unto king Asa, and sendeth the heads of the forces that he hath unto cities of Israel, and they smite Ijon, and Dan, and Abel-Maim, and all the stores, cities of Naphtali.
5 Ikawa kwamba Baasha aliposikia hili, akaacha kuujenga Rama, na akaistisha kazi yake.
And it cometh to pass, at Baasha's hearing, that he ceaseth from building Ramah, and letteth his work rest;
6 Kisha Asa mfalme akawachukua Yuda wote pamoja naye. Wakayabeba mawe na mbao za Rama ambazo Baasha alikuwa anajengea ule mji. Kisha Mfalme Asa alitumia vifaa hivyo vya ujenzi kwa ajili ya kuijenga Gaba na Mispa.
and Asa the king hath taken all Judah, and they bear away the stones of Ramah, and its wood, that Baasha hath built, and he buildeth with them Geba and Mizpah.
7 Wakati huo Hanani mwonaji akaenda kwa Asa, mfalme wa Yuda, na akamwambia, “Kwa sababu umemtegemea mfalme wa Aramu, na hukumtegemea Yahwe Mungu wako, jeshi la mfalme wa Aramu limetoroka nje ya mikono yako.
And at that time hath Hanani the seer come in unto Asa king of Judah, and saith unto him, 'Because of thy leaning on the king of Aram, and thou hast not leaned on Jehovah thy God, therefore hath the force of the king of Aram escaped from thy hand.
8 Waethiopia na Walubi hawakuwa jesi kubwa, wenye magari mengi na wapanda farasi wengi? Na bado, kwa sababau ulimtegemea Yahwe, alikupa ushindi juu yao.
Did not the Cushim and the Lubim become a very great force for multitude, for chariot, and for horsemen? and in thy leaning on Jehovah He gave them into thy hand,
9 Kwa maana macho ya Yahwe hukimbia kila mahali katika dunia yote, ili kwamba ajioneshe mwenyewe shujaa kwa niaba ya wale amabao mioyo yao ni mikamilifu kumwelekea yeye. Lakini umetenda kipumbavu katika jambo hili. Kwa maana tangu sasa na kuendelea, utakuwa na vita.” Kisha Asa akamkasirikia mwonaji, akamuweka gerezani, kwa maana alikuwa na hasira naye juu ya jambao
for Jehovah — His eyes go to and fro in all the earth, to show Himself strong [for] a people whose heart [is] perfect towards Him; thou hast been foolish concerning this, because — henceforth there are with thee wars.'
10 hili. Wakati huo huo, aliwagandamiza baadhi ya watu
And Asa is angry at the seer, and giveth him to the house of torture, for [he is] in a rage with him for this; and Asa oppresseth [some] of the people at that time.
11 Tazma, matendo ya Asa, kutoka mwanzo hadi mwisho, tazama, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
And lo, the matters of Asa, the first and the last, lo, they are written on the book of the kings of Judah and Israel.
12 Katika mwaka wa thelathini na tisa wa utawala wake, Asa alipata ugnjwa kwenye miguu yake; ugonjwa wake ulikuwa mkali sana. Hata hivyo, hakutafuta msaada kutoka kwa Yahwe, lakini kutoka kwa waganga tu.
And Asa is diseased — in the thirty and ninth year of his reign — in his feet, till his disease is excessive, and also in his disease he hath not sought Jehovah, but among physicians.
13 Asa akalala pamoja na babu zake; alikufa katika mwaka wa arobaiani na moja wa utawala wake. Wakamzika katika kaburi lake, ambalo alilichimba mwenyewe katika mji wa Daudi.
And Asa lieth with his fathers, and dieth in the forty and first year of his reign,
14 Walimlaza juu ya kitanda kilichokuwa kimewekewa manukato na aina mbali mbali ya dawa zilizotayarishwa na wale mafundi wa manukato. KIsha wakatengeneza moto kwa heshima yake.
and they bury him in [one of] his graves, that he had prepared for himself in the city of David, and they cause him to lie on a bed that [one] hath filled [with] spices, and divers kinds of mixtures, with perfumed work; and they burn for him a burning — very great.

< 2 Nyakati 16 >