< 1 Wafalme 6 >

1 Kwa hiyo Sulemani akaanza kulijenga hekalu. Hii ilikuwa mwaka wa 480 baada ya wana wa Israeli kutoka katika nchi ya Misri, katika mwaka wa nne wa utawala wa Sulemani huko Israeli, katika mwezi wa Ziv, ambao ndio mwezi wa pili.
And it cometh to pass, in the four hundred and eightieth year of the going out of the sons of Israel from the land of Egypt, in the fourth year — in the month of Zif, it [is] the second month — of the reigning of Solomon over Israel, that he buildeth the house for Jehovah.
2 Hekalu ambalo mfalme Sulemani alimjengea BWANA lilikuwa na urefu wa mita 27, na upana wa mita 9, na kimo cha mita 13. 5.
As to the house that king Solomon hath built for Jehovah, sixty cubits [is] its length, and twenty its breadth, and thirty cubits its height.
3 Na ukumbi uliokuwa mbele ya hekalu ulikuwa na urefu wa mita 9 na upana wa mita 4. 5 sawa na upana wa sehemu kuu ya hekalu.
As to the porch on the front of the temple of the house, twenty cubits [is] its length on the front of the breadth of the house; ten by the cubit [is] its breadth on the front of the house;
4 Lile hekalu alilitengenezea madirisha ambayo fremu zake kwa nje yalifanya yaonekane membamba kuliko ile sehemu ya ndani.
and he maketh for the house windows of narrow lights.
5 Na ukuta wa nyumba aliuzungushia vyumba kuzunguka pande zake, kushikamana na vyumba vya nje na vya ndani ya hekalu. Akajenga vyumba katika pande zote.
And he buildeth against the wall of the house a couch round about, [even] the walls of the house round about, of the temple and of the oracle, and maketh sides round about.
6 Kile chumba cha chini kilikuwa na upana wa mita 2. 3, kile cha kati kilikuwa na upana wa mita 2. 8. na kile cha tatu kilikuwa na upana wa mita 3. 2. upande wa nje akaupunguza ukuta wa nyumba pande zote, ili boriti zisishikamane ukutani mwa nyumba.
The lowest couch, five by the cubit [is] its breadth; and the middle, six by the cubit [is] its breadth; and the third, seven by the cubit [is] its breadth, for withdrawings he hath put to the house round about, without — not to lay hold on the walls of the house.
7 Hekalu lilijengwa kwa mawe yaliyokuwa yamechongwa chimboni. Hakuna nyundo, wala shoka au chombo chochote cha chuma kilisikika wakati hekalu lilipokuwa likjengwa.
And the house, in its being built, of perfect stone brought [thither] hath been built, and hammer, and the axe — any instrument of iron — was not heard in the house, in its being built.
8 Upande wa kusini wa hekalu kulikuwa na lango la chini, ambalo mtu hupanda kwa madaraja mpaka juu kwenye chumba cha kati, na kutoka chumba cha kati hadi chumba cha tatu.
The opening of the middle side [is] at the right shoulder of the house, and with windings they go up on the middle one, and from the middle one unto the third.
9 Kwa hiyo Sulemani akalijenga hekalu mpaka akalimaliza, akalifunika hekalu kwa boriti na mbao za mwerezi.
And he buildeth the house, and completeth it, and covereth the house [with] beams and rows of cedars.
10 Akajenga vyumba vya pembeni mwa hekalu, kila upande mita 2. 3 kwenda juu. Navyo vikaunganishwa na hekalu kwa mbao za mierezi.
And he buildeth the couch against all the house, five cubits [is] its height, and it taketh hold of the house by cedar-wood.
11 Neno la BWANA likamjia Sulemani, likisema,
And the word of Jehovah is unto Solomon, saying,
12 “Kuhusu hili hekalu ambalo unajenga, kama utatatembea katika maagizo yangu na kuhukumu kwa haki, na kutunza amri zangu na kuishi kwa hizo, ndipo ntakapozithibitisha ahadi zangu na wewe ambazo niliziahidi kwa baba yako Daudi.
'This house that thou art building — if thou dost walk in My statutes, and My judgments dost do, yea, hast done all My commands, to walk in them, then I have established My word with thee, which I spake unto David thy father,
13 Nitaishi kati ya watu wa Israeli nami sitawatupa.”
and have tabernacled in the midst of the sons of Israel, and do not forsake My people Israel.'
14 Kwa hiyo Sulemani akalijenga hekalu mpaka akalimaliza.
And Solomon buildeth the house and completeth it;
15 Kisha akajenga kuta za ndani za hekalu kwa mbao za mwerezi. Kuanzia sakafu ya hekalu hadi boriti za juu, kwa ndani akazifunika kwa miti, na akaifunika sakafu kwa mbao za miberoshi.
and he buildeth the walls of the house within with beams of cedar, from the floor of the house unto the walls of the ceiling; he hath overlaid with wood the inside, and covereth the floor of the house with ribs of fir.
16 Alijenga mita 9 ndani ya hekalu kwa mbao za miberoshi kutoka sakafuni hadi juu. Hiki ni chumba cha ndani, cha patakatifu sana.
And he buildeth the twenty cubits on the sides of the house with ribs of cedar, from the floor unto the walls; and he buildeth for it within, for the oracle, for the holy of holies.
17 Ule ukumbu mkuu, ulikuwa mahali pakatifu amabao ulikuwa mbele ya patakatifu sana, ulikuwa wa mita 18. hapo kulikwa na mbao za mwerezi ndani ya hekalu, zilizokuwa zimechongwa kwa sura ya vibuyu na maua yaliyochanua.
And forty by the cubit was the house, it [is] the temple before [it].
18 Zote zilikuwa za mierezi kwa ndani. Hapakuonekana chochote ndani kilichokuwa kimetengenezwa kwa mawe.
And the cedar for the house within [is] carvings of knobs and openings of flowers; the whole [is] cedar, there is not a stone seen.
19 Sulemani alitengeneza kile chumba cha ndani kwa lengo la kuweka sanduku la agano la BWANA.
And the oracle in the midst of the house within he hath prepared, to put there the ark of the covenant of Jehovah.
20 Kile chumba cha ndani kilikuwa na upana wa mita 9, na kimo cha mita 9. Sulemani alizifunika kuta kwa dhabahu na madhabahu aliifunika kwa mbao za mierezi.
And before the oracle [is] twenty cubits in length, and twenty cubits in breadth, and twenty cubits [is] its height; and he overlayeth it with gold refined, and overlayeth the altar with cedar.
21 Sulemani alifunika ndani ya hekalu kwa dhahabu safi na akaweka mikufu ya dhahabu iliyopita mbele ya chumba cha ndani, na kulifunika eneo la mbele kwa dhabahu.
And Solomon overlayeth the house within with gold refined, and causeth [it] to pass over in chains of gold before the oracle, and overlayeth it with gold.
22 Akalisakafia kwa dhahabu eneo lote la ndani mpaka akamaliza hekalu lote. Pia akalisakafia kwa dhahabu madhahabu yote ya chumba cha ndani.
And the whole of the house he hath overlaid with gold, till the completion of all the house; and the whole of the altar that the oracle hath, he hath overlaid with gold.
23 Sulemani akatengeneza makerubi mawili kwa mbao za mizeituni, kila moja lilikuwa na kimo cha mita 4. 5 kwa ajili ya chumba cha ndani.
And he maketh within the oracle two cherubs, of the oil-tree, ten cubits [is] their height;
24 Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa mita 2. 3. Kwa hiyo kutoka ncha ya bawa moja hadi ncha ya bawa lingine kulikuwa na umbali wa mita 4. 5. Yule
and five cubits [is] the one wing of the cherub, and five cubits the second wing of the cherub, ten cubits from the ends of its wings even unto the ends of its wings;
25 kerubi mwingine naye alikuwa na bawa lenye kipimo cha mita 4. 5 Makerubi hawa walikuwa wanafanana kwa umbo na kwa vipimo.
and ten by the cubit [is] the second cherub, one measure and one form [are] to the two cherubs,
26 Kimo cha kerubi mmoja kilikuwa mita 4. 5 na yule wa pili alikuwa hivyo hivyo.
the height of the one cherub [is] ten by the cubit, and so [is] the second cherub;
27 Sulemani aliwaweka hao kerubi kwenye chumba cha patakatifu sana. Bawa moja la kerubi lilikuwa limeenea kiasi kwamba bawa moja liligusa ukuta huu na bawa la yule wa pili nalo liligusa ukuta wa upande mwingine. Hayo mabawa yalikuwa yanakutana katikati ya chumba cha patakatifu sana.
and he setteth the cherubs in the midst of the inner house, and they spread out the wings of the cherubs, and a wing of the one cometh against the wall, and a wing of the second cherub is coming against the second wall, and their wings [are] unto the midst of the house, coming wing against wing;
28 Sulemani aliwafunika hao kerubi kwa dhahabu.
and he overlayeth the cherubs with gold,
29 Akazinakshi kuta zote kwa sura za makerubi, miti ya mitende, na maua yaliyochanua, kwa vyumba vya nje na vya ndani.
and all the walls of the house round about he hath carved with openings of carvings, cherubs, and palm trees, and openings of flowers, within and without.
30 Sulemani akalisakafia hekalu kwa dhahabu, kwa vyumba vyote vya ndani na vya nje.
And the floor of the house he hath overlaid with gold, within and without;
31 Sulemani akatengeneza milango ya mbao za mizeituni kwenye lango la kuingia ndani. Aliweka vizingiti na miimo kwenye pande tano.
as to the opening of the oracle, he made doors of the oil-tree; the lintel, side-posts, a fifth.
32 Kwa hiyo akatengeneza na milango miwili ya mizeituni, na akainakshi kwa makerubi, na mitende, na maua yaliyochanua. Akasakafia kwa dhahabu na akatandaza dhahabu kwenye makerubi na kwenye mitende.
And the two doors [are] of the oil-tree, and he hath carved upon them carvings of cherubs, and palm-trees, and openings of flowers, and overlaid with gold, and he causeth the gold to go down on the cherubs and on the palm-trees.
33 Kwa njia hii, akalitengenezea hekalu miimo miwili ya mbao za mizeituni yenye pande nne
And so he hath made for the opening of the temple, side-posts of the oil-tree, from the fourth.
34 na milango miwili ya mbao za mierezi. Zile mbao mbili za mlango mmoja zilikuwa zikijikunja na mbao mbili za mlango wa pili nazo zilikuwa zikijikunja pia.
And the two doors [are] of fir-tree, the two sides of the one door are revolving, and the two hangings of the second door are revolving.
35 Akazinakshi kwa makerubi, mitende, na maua yaliyochanua, na pia akazisakafia kwa dhahabu juu ya zile nakshi.
And he hath carved cherubs, and palms, and openings of flowers, and overlaid with straightened gold the graved work.
36 Akalijengs Korido la ndani kwa safu tatu za mawe ya kuchongwa na safu moja ya mhimili wa mierezi.
And he buildeth the inner court, three rows of hewn work, and a row of beams of cedar.
37 Msingi wa hekalu ulijengwa katika mwaka wa nne, wa mwezi wa Ziv.
In the fourth year hath the house of Jehovah been founded, in the month Zif,
38 Mwaka wa kumi na moja mwezi wa Buli, ambao ndio mwezi wa nane, sehemu zote za hekalu zilimalizika na sharti zake zote. Sulemani alilijenga hekalu kwa miaka saba.
and in the eleventh year, in the month Bul — [that is] the eighth month — hath the house been finished in all its matters, and in all its ordinances, and he buildeth it seven years.

< 1 Wafalme 6 >