< 1 Wafalme 6 >

1 Kwa hiyo Sulemani akaanza kulijenga hekalu. Hii ilikuwa mwaka wa 480 baada ya wana wa Israeli kutoka katika nchi ya Misri, katika mwaka wa nne wa utawala wa Sulemani huko Israeli, katika mwezi wa Ziv, ambao ndio mwezi wa pili.
And it was in eighty year and four hundred year of [the] coming out of [the] people of Israel from [the] land of Egypt in the year fourth in [the] month of Ziv that [was] the month second of [the] reigning of Solomon over Israel and he built the house for Yahweh.
2 Hekalu ambalo mfalme Sulemani alimjengea BWANA lilikuwa na urefu wa mita 27, na upana wa mita 9, na kimo cha mita 13. 5.
And the house which he built the king Solomon for Yahweh [was] sixty cubit[s] length its and [was] twenty breadth its and [was] thirty cubit[s] height its.
3 Na ukumbi uliokuwa mbele ya hekalu ulikuwa na urefu wa mita 9 na upana wa mita 4. 5 sawa na upana wa sehemu kuu ya hekalu.
And the porch on [the] face of [the] temple of the house [was] twenty cubit[s] length its on [the] face of [the] breadth of the house [was] ten by the cubit breadth its on [the] face of the house.
4 Lile hekalu alilitengenezea madirisha ambayo fremu zake kwa nje yalifanya yaonekane membamba kuliko ile sehemu ya ndani.
And he made for the house windows of frames shut.
5 Na ukuta wa nyumba aliuzungushia vyumba kuzunguka pande zake, kushikamana na vyumba vya nje na vya ndani ya hekalu. Akajenga vyumba katika pande zote.
And he built on [the] wall of the house (an extension *QK) all around [the] walls of the house around the temple and the innermost room and he made side-chambers all around.
6 Kile chumba cha chini kilikuwa na upana wa mita 2. 3, kile cha kati kilikuwa na upana wa mita 2. 8. na kile cha tatu kilikuwa na upana wa mita 3. 2. upande wa nje akaupunguza ukuta wa nyumba pande zote, ili boriti zisishikamane ukutani mwa nyumba.
(The extension *QK) lower [was] five by the cubit breadth its and the middle [extension] [was] six by the cubit breadth its and third [extension] [was] seven by the cubit breadth its for ledges he made for the house around [the] outside towards to not to have hold in [the] walls of the house.
7 Hekalu lilijengwa kwa mawe yaliyokuwa yamechongwa chimboni. Hakuna nyundo, wala shoka au chombo chochote cha chuma kilisikika wakati hekalu lilipokuwa likjengwa.
And the house when was built it stone perfect quarry it was built and hammers and axe any article of iron not it was heard in the house when was built it.
8 Upande wa kusini wa hekalu kulikuwa na lango la chini, ambalo mtu hupanda kwa madaraja mpaka juu kwenye chumba cha kati, na kutoka chumba cha kati hadi chumba cha tatu.
[the] entrance of The side-chamber middle [was] to [the] side of the house south and by stairs people went up to the middle and from the middle to the thirty.
9 Kwa hiyo Sulemani akalijenga hekalu mpaka akalimaliza, akalifunika hekalu kwa boriti na mbao za mwerezi.
And he built the house and he finished it and he covered the house beams and planks with cedar.
10 Akajenga vyumba vya pembeni mwa hekalu, kila upande mita 2. 3 kwenda juu. Navyo vikaunganishwa na hekalu kwa mbao za mierezi.
And he built (the extension *QK) on all the house [was] five cubits height its and he covered the house with wood of cedar.
11 Neno la BWANA likamjia Sulemani, likisema,
And it came [the] word of Yahweh to Solomon saying.
12 “Kuhusu hili hekalu ambalo unajenga, kama utatatembea katika maagizo yangu na kuhukumu kwa haki, na kutunza amri zangu na kuishi kwa hizo, ndipo ntakapozithibitisha ahadi zangu na wewe ambazo niliziahidi kwa baba yako Daudi.
The house this which you [are] building if you will walk in statutes my and judgments my you will observe and you will keep all commandments my to walk in them and I will establish word my with you which I spoke to David father your.
13 Nitaishi kati ya watu wa Israeli nami sitawatupa.”
And I will dwell in among [the] people of Israel and not I will abandon people my Israel.
14 Kwa hiyo Sulemani akalijenga hekalu mpaka akalimaliza.
And he built Solomon the house and he finished it.
15 Kisha akajenga kuta za ndani za hekalu kwa mbao za mwerezi. Kuanzia sakafu ya hekalu hadi boriti za juu, kwa ndani akazifunika kwa miti, na akaifunika sakafu kwa mbao za miberoshi.
And he built [the] walls of the house from inside with boards of cedar from [the] floor of the house to [the] walls of the ceiling he overlaid wood from inside and he overlaid [the] floor of the house with boards of cypresses.
16 Alijenga mita 9 ndani ya hekalu kwa mbao za miberoshi kutoka sakafuni hadi juu. Hiki ni chumba cha ndani, cha patakatifu sana.
And he built twenty cubit[s] (from [the] innermost parts of *Qk) the house with boards of cedar from the floor to the walls and he built for it from inside to an innermost room to [the] holy place of the holy places.
17 Ule ukumbu mkuu, ulikuwa mahali pakatifu amabao ulikuwa mbele ya patakatifu sana, ulikuwa wa mita 18. hapo kulikwa na mbao za mwerezi ndani ya hekalu, zilizokuwa zimechongwa kwa sura ya vibuyu na maua yaliyochanua.
And forty by the cubit it was the house that [is] the temple before me.
18 Zote zilikuwa za mierezi kwa ndani. Hapakuonekana chochote ndani kilichokuwa kimetengenezwa kwa mawe.
And cedar [was] to the house within carving of gourds and spread out [things] of flowers everything [was] cedar not stone [was] visible.
19 Sulemani alitengeneza kile chumba cha ndani kwa lengo la kuweka sanduku la agano la BWANA.
And an innermost room in [the] middle of the house from within he prepared to put there [the] ark of [the] covenant of Yahweh.
20 Kile chumba cha ndani kilikuwa na upana wa mita 9, na kimo cha mita 9. Sulemani alizifunika kuta kwa dhabahu na madhabahu aliifunika kwa mbao za mierezi.
And before the innermost room [was] twenty cubit[s] length and [was] twenty cubit[s] breadth and [was] twenty cubit[s] height its and he overlaid it gold gold plate and he overlaid an altar cedar.
21 Sulemani alifunika ndani ya hekalu kwa dhahabu safi na akaweka mikufu ya dhahabu iliyopita mbele ya chumba cha ndani, na kulifunika eneo la mbele kwa dhabahu.
And he overlaid Solomon the house from within gold gold plate and he made pass (with chains of *QK) gold before the innermost room and he overlaid it gold.
22 Akalisakafia kwa dhahabu eneo lote la ndani mpaka akamaliza hekalu lote. Pia akalisakafia kwa dhahabu madhahabu yote ya chumba cha ndani.
And all the house he overlaid gold until was finished all the house and all the altar which [belonged] to the innermost room he overlaid gold.
23 Sulemani akatengeneza makerubi mawili kwa mbao za mizeituni, kila moja lilikuwa na kimo cha mita 4. 5 kwa ajili ya chumba cha ndani.
And he made in the innermost room two cherubim wood of olive [was] ten cubits height its.
24 Bawa moja la kerubi wa kwanza lilikuwa na urefu wa mita 2. 3. Kwa hiyo kutoka ncha ya bawa moja hadi ncha ya bawa lingine kulikuwa na umbali wa mita 4. 5. Yule
And [was] five cubits [the] wing of the cherub one and [was] five cubits [the] wing of the cherub second [was] ten cubits from [the] ends of wings its and to [the] ends of wings its.
25 kerubi mwingine naye alikuwa na bawa lenye kipimo cha mita 4. 5 Makerubi hawa walikuwa wanafanana kwa umbo na kwa vipimo.
And [was] ten by the cubit the cherub second a measurement one and a shape one [belonged] to [the] two the cherubim.
26 Kimo cha kerubi mmoja kilikuwa mita 4. 5 na yule wa pili alikuwa hivyo hivyo.
[the] height of The cherub one [was] ten by the cubit and thus the cherub second.
27 Sulemani aliwaweka hao kerubi kwenye chumba cha patakatifu sana. Bawa moja la kerubi lilikuwa limeenea kiasi kwamba bawa moja liligusa ukuta huu na bawa la yule wa pili nalo liligusa ukuta wa upande mwingine. Hayo mabawa yalikuwa yanakutana katikati ya chumba cha patakatifu sana.
And he put the cherubim in [the] middle of - the house inner and they spread out [the] wings of the cherubim and it touched [the] wing of the one [cherub] the wall and [the] wing of the cherub second [was] touching the wall second and wings their to [the] middle of the house [were] touching wing to wing.
28 Sulemani aliwafunika hao kerubi kwa dhahabu.
And he overlaid the cherubim gold.
29 Akazinakshi kuta zote kwa sura za makerubi, miti ya mitende, na maua yaliyochanua, kwa vyumba vya nje na vya ndani.
And all [the] walls of the house round about - he carved engravings of carvings of cherubim and palm trees and spread out [things] of flowers from to faces and to the outer.
30 Sulemani akalisakafia hekalu kwa dhahabu, kwa vyumba vyote vya ndani na vya nje.
And [the] floor of the house he overlaid gold to within and to the outer.
31 Sulemani akatengeneza milango ya mbao za mizeituni kwenye lango la kuingia ndani. Aliweka vizingiti na miimo kwenye pande tano.
And [the] entrance of the innermost room he made doors of wood of olive the pillar doorposts of fifth.
32 Kwa hiyo akatengeneza na milango miwili ya mizeituni, na akainakshi kwa makerubi, na mitende, na maua yaliyochanua. Akasakafia kwa dhahabu na akatandaza dhahabu kwenye makerubi na kwenye mitende.
And two doors of wood of olive and he carved on them carvings of cherubim and palm trees and spread out [things] of flowers and he overlaid [them] gold and he hammered out on the cherubim and on the palm trees the gold.
33 Kwa njia hii, akalitengenezea hekalu miimo miwili ya mbao za mizeituni yenye pande nne
And thus he made for [the] entrance of the temple doorposts of wood of olive from with a fourth.
34 na milango miwili ya mbao za mierezi. Zile mbao mbili za mlango mmoja zilikuwa zikijikunja na mbao mbili za mlango wa pili nazo zilikuwa zikijikunja pia.
And two doors of wood of cypresses two sides the door one [were] revolving and two curtains the door second [were] revolving.
35 Akazinakshi kwa makerubi, mitende, na maua yaliyochanua, na pia akazisakafia kwa dhahabu juu ya zile nakshi.
And he carved cherubim and palm trees and spread out [things] of flowers and he overlaid gold made smooth on the carved [work].
36 Akalijengs Korido la ndani kwa safu tatu za mawe ya kuchongwa na safu moja ya mhimili wa mierezi.
And he built the court inner three rows of hewn [stone] and a row of beams of cedar.
37 Msingi wa hekalu ulijengwa katika mwaka wa nne, wa mwezi wa Ziv.
In the year fourth it was founded [the] house of Yahweh in [the] month of Ziv.
38 Mwaka wa kumi na moja mwezi wa Buli, ambao ndio mwezi wa nane, sehemu zote za hekalu zilimalizika na sharti zake zote. Sulemani alilijenga hekalu kwa miaka saba.
And in the year one plus ten in [the] month of Bul that [was] the month eighth it was complete the house to all parts its and to all (plans its *QK) and he built it seven years.

< 1 Wafalme 6 >