< 1 Nyakati 24 >

1 Makundi vya kazi kulingana na uzao wa Aroni yalikuwa haya: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
Ahora, los hijos de Aarón fueron distribuidos en grupos. Los hijos de Aarón fueron Nadab, Abiú, Eleazar e Itamar.
2 Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao kufa. Walikuwa hawana watoto, kwahiyo Eleazari na Ithamari walitumika kama makuhani.
Pero como Nadab y Abiú murieron antes que su padre, y no tuvieron hijos, Eleazar e Itamar ejercieron el sacerdocio.
3 Daudi pamoja na Zadoki, uzao wa Eleazari, na Ahimeleki, uzao wa Ithamari, waliwagawanya katika makundi yao ya kazi kama makuhani.
David y Sadoc repartieron a los hijos de Eleazar, los hijos de Ahimelec y los hijos de Itamar por turnos en el ministerio.
4 Kulikuwa na wanaume viongozi zaidi kati ya uzao wa Eleazari kuliko kati ya uzao wa Ithamari, kwahiyo waligawanya uzao wa Eleazari katika makundi kumi na sita. Walifanya hivyo na viongozi wa ukoo na uzao wa Ithamari. Magawanyo haya yalikuwa nane kwa idadi, sambamba na koo zao.
Pero como había más varones jefes de los hijos de Eleazar que de los hijos de Itamar, los repartieron así: De los hijos de Eleazar, 16 jefes de casas paternas, y de los hijos de Itamar ocho jefes de casas paternas.
5 Waliwagawanya bila upendeleo kwa kura, kwa kuwa walikuwa waamuzi watakatifu na waamuzi wa Mungu, kutoka pande zote uzao wa Eleazari na uzao wa Ithamari.
De esta manera fueron repartidos por sorteo los unos y los otros, porque tanto de los hijos de Eleazar como de los hijos de Itamar hubo funcionarios del Santuario y funcionarios de ʼElohim.
6 Shemaia mwana wa Nethaneli mwandishi, Mlawi, aliandika majina yao mbele ya mfalme, muamuzi, kuhani Zadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa makuhani na familia za Walawi. Ukoo mmoja ulichaguliwa kwa kura kutoka uzao wa Eleazari, na kisha uliofata utachaguliwa kutoka uzao wa Ithhamari.
El escriba Semaías, hijo de Natanael, de los levitas, escribió sus nombres en presencia del rey y de los jefes, delante de Sadoc el sacerdote, de Ahimelec, hijo de Abiatar, y de los jefes de las casas paternas de los sacerdotes y levitas. Designaron por sorteo una casa paterna para Eleazar y otra para Itamar.
7 Kura ya kwanza ilienda kwa Yehoiaribu, ya pili kwa Yedaia,
La primera suerte tocó a Joiarib, la segunda a Jedaías,
8 ya tatu kwa Harimu, ya nne kwa Seorimu,
la tercera a Harim, la cuarta a Seorim,
9 ya tano kwa Malikija, ya sita kwa Mijamini,
la quinta a Malquías, la sexta a Mijamín,
10 ya saba kwa Hakozi, ya nane kwa Abija,
la séptima a Cos, la octava a Abías,
11 ya tisa kwa Yeshua, ya kumi kwa Shekania,
la novena a Jesúa, la décima a Secanías,
12 ya kumi na moja kwa Eliashibu, ya kumi na mbili kwa Yakimu,
la undécima a Eliasib, la duodécimma a Jaquim,
13 ya kumi na tatu kwa Hupa, ya kumi na nne kwa Yesheheabu,
la decimotercera a Hupa, la decimocuarta a Jesebeab,
14 ya kumi na tano kwa Biliga, ya kumi na sita kwa Imma,
la decimoquinta a Bilga, la decimosexta a Imer,
15 ya kumi na saba kwa Heziri, ya kumi na nane kwa Hapizezi,
la decimoséptima a Hezir, la decimoctava a Afses,
16 ya kumi na tisa kwa Pethaia, ya ishirini kwa Yehezikeli,
la decimonovena a Petaías, la vigésima a Hezequiel,
17 ya ishirini na moja kwa Yakini, ya ishirini na mbili kwa Gamuli,
la vigesimoprimera a Jaquín, la vigesimosegunda a Gamul,
18 ya ishirini na tatu kwa Delaia, na ya ishirini na nne kwa Maazia.
la vigesimotercera a Delaía, la vigesimocuarta a Maazías.
19 Hii ilikuwa taratibu ya utumishi wao, walipo kuja kwenye nyumba ya Yahweh, wakifuata utaratibu waliopewa na Aruni babu yao, kama Yahweh, Mungu wa Israeli, alivyo waagiza.
Éstos fueron distribuidos para su ministerio, para que entraran en la Casa de Yavé, según les fue ordenado por su padre Aarón, de la manera como Yavé ʼElohim de Israel le mandó.
20 Hawa walikuwa Walawi waliobakia: Wana wa Amiramu, Shebueli; wana wa Shebaeli, Yedeia.
De los hijos de Leví que quedaron fueron designados: Subael, de los hijos de Amram y Jehedías, de los hijos de Subael.
21 Wana wa Rehabia: wana wa Rehabia, Ishia kiongozi.
De los hijos de Rehabías, Isías el primero.
22 Wa Waizari, Shelomothi; mwana wa Shelomothi, Yahathi.
De los izharitas, Selomot. De los hijos de Selomot, Jahat.
23 Wana wa Hebroni: Yeria kiongozi, Amaria wapili, Yahazieli watatu, na Yekameamu wanne.
De los hijos de Hebrón, Jerías el primero, Amarías el segundo, Jahaziel el tercero, Jecamán el cuarto.
24 Wana wa uzao wa Uzieli ulimjumuisha Mika. Uzao wa Mika ulimjumuisha Shamiri.
De los hijo de Uziel, Micaía. De los hijos de Micaía, Samir.
25 Kaka wa Mika alikuwa Ishia. Wana wa Ishia akijumuishwa Zakaria.
El hermano de Micaía, Isías. De los hijos de Isías, Zacarías.
26 Wana na Merari: Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia, Beno.
De los hijos de Merari: Mahli y Musi. De los hijos de Jaazías, Beno.
27 Wana wa Merari: Yaazia, Beno, Shohamu, Zakuri, na Ibrri.
Los hijos de Merari por medio de Jaazías fueron: Beno, Soham, Zacur e Ibri.
28 Wana wa Mahili: eleazari, ambaye alikuwa hana wana.
De Mahli, Eleazar, quien no tuvo hijos.
29 Wana wa Kishi: Yerameli
De Cis, hijo de Cis, Jerameel.
30 wana wa Mushi: Mahli, Eda, na yerimothi. Walikuwa walawi, walio orodheshwa na familia zao.
Los hijos de Musi: Mahli, Edar y Jerimot. Éstos fueron los hijos de los levitas según sus casas paternas.
31 Wanaume hawa ambao walikuwa vichwa katika nyumba za baba zao na kila wadogo zao, walipiga kura katika uwepo wa Mfalme Daudi, na Zadoki na Ahimeleki, pamoja na viongozi wa familia wa makuhani na Walawi. Walirusha kura kama uzao wa Aroni walivyofanya.
Éstos también echaron suertes, como sus hermanos, los hijos de Aarón, en presencia del rey David, Sadoc, Ahimelec y los jefes de las casas paternas, tanto de los sacerdotes como de los levitas, las casas paternas de los jefes y el menor de sus hermanos por igual.

< 1 Nyakati 24 >