< 1 Nyakati 23 >

1 Daudi alipo kuwa mzee na kukaribia mwisho wa maisha yake, alimfanya Sulemani mwanae mfalme juu ya Israeli.
大衛年紀老邁,日子滿足,就立他兒子所羅門作以色列的王。
2 Aliwakusanya pamoja viongozi wote wa Israeli, na makuhani na Walawi.
大衛招聚以色列的眾首領和祭司利未人。
3 Walawi walio kuwa miaka thelathini na zaidi walihesabiwa. Idadi ya elfu thelathini na nane.
利未人從三十歲以外的都被數點,他們男丁的數目共有三萬八千;
4 Kwa hawa, elfu ishirini na nne walikuwa kusimamia kazi ya nyumba ya Yahweh, na elfu sita walikuwa maaskari na waamuzi.
其中有二萬四千人管理耶和華殿的事,有六千人作官長和士師,
5 Elfu nne walikuwa walinzi wa lango, na elfu nne walikuwa wamsifu Yahweh na vyombo nilivyo vitengeneza vya kusifu.” Daudi akasema.
有四千人作守門的,又有四千人用大衛所做的樂器頌讚耶和華。
6 Akawatenganisha kwenye vikundi kulingana na wana wa Levi: Gerishoni, Kohathi, na Merari.
大衛將利未人革順、哥轄、米拉利的子孫分了班次。
7 Kwa koo za uzao wa Gerishoni, kulilkuwa na Ladani na Shimei.
革順的子孫有拉但和示每。
8 Palikuwa na watatu wa wana wa Ladani: Yehieli kiongozi, Zethami, na Yoeli.
拉但的長子是耶歇,還有細坦和約珥,共三人。
9 Palikuwa na watatu wa wana wa Shimei: Shelomothi, Hazieli, na Harani. Hawa walikuwa viongozi wa koo ya Ladani.
示每的兒子是示羅密、哈薛、哈蘭三人。這是拉但族的族長。
10 Palikuwa na wanne wa wana wa Shimei: Yahathi, Ziza, Yeushi, na Beria.
示每的兒子是雅哈、細拿、耶烏施、比利亞共四人。
11 Yahathi alikuwa mkubwa, Ziza wapili, lakini Yeushi na Beria hawakuwa na wana wengi, hivyo walihesabiwa kama ukoo mmoja na kupangiwa kazi sawa.
雅哈是長子,細撒是次子。但耶烏施和比利亞的子孫不多,所以算為一族。
12 Palikuwa na wanne wa wana wa Kohathi: Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
哥轄的兒子是暗蘭、以斯哈、希伯倫、烏薛共四人。
13 Hawa walikuwa wana wa Amramu: Aruni na Musa. Aruni alichaguliwa kuandaa vitu vitakatifu, yeye na uzao wake watatoa uvumba kwa Yahweh, kumtumikia na kumpa baraka kwa jina lake.
暗蘭的兒子是亞倫、摩西。亞倫和他的子孫分出來,好分別至聖的物,在耶和華面前燒香、事奉他,奉他的名祝福,直到永遠。
14 Lakini kwa Musa mtu wa Mungu, wana wake walihesabiwa kuwa Walawi.
至於神人摩西,他的子孫名字記在利未支派的冊上。
15 Wana wa Musa walikuwa Gerishomu na Eliezeri.
摩西的兒子是革舜和以利以謝。
16 Uzao wa Gerishomu ulikuwa Shebueli mkubwa.
革舜的長子是細布業;
17 Uzao wa Eliezeri alikuwa Rehabia. Eliezeri hakuwa na wana wengine, lakini Rehabia alikuwa na uzao mkubwa.
以利以謝的兒子是利哈比雅。以利以謝沒有別的兒子,但利哈比雅的子孫甚多。
18 Mwana wa Izihari alikuwa Shelomithi kiongonzi.
以斯哈的長子是示羅密。
19 Uzao wa Hebroni ulikuwa Yeria, mkubwa, Amaria wapili, Yahazieli watatu, na Yekameamu wanne.
希伯倫的長子是耶利雅,次子是亞瑪利亞,三子是雅哈悉,四子是耶加面。
20 Wana wa Uzieli walikuwa Mika mkubwa, na Ishia wapili.
烏薛的長子是米迦,次子是耶西雅。
21 Wana wa Merari walikuwa Mahili na Mushi. Wana wa Mahili walikuwa Eleazari na Kishi.
米拉利的兒子是抹利、母示。抹利的兒子是以利亞撒、基士。
22 Eleazari alikufa bila mtoto wa kiume. Alikuwa na mabinti tu. Wana wa Kishi waliwaoa.
以利亞撒死了,沒有兒子,只有女兒,他們本族基士的兒子娶了她們為妻。
23 Wana wa Mushi watatu walikuwa Mahili, Ederi, na Yeremothi.
母示的兒子是末力、以得、耶利摩共三人。
24 Hawa walikuwa uzao wa Lawi kuligana na koo zao. Walikuwa viongozi, wamehesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, kuanzia koo zilizo fanya kazi katika nyumba ya Yahweh, kutoka miaka ishirini na zaidi.
以上利未子孫作族長的,照着男丁的數目,從二十歲以外,都辦耶和華殿的事務。
25 Kwa kuwa Daudi alisema, “Yahweh, Mungu wa Israeli, amewapa pumziko watu wake. Anafanya makao yake Yerusalemu milele.
大衛說:「耶和華-以色列的上帝已經使他的百姓平安,他永遠住在耶路撒冷。
26 Walawi hawataitaji kubeba hema la kuabuadia na vifaa vyake vinavyo tumika kwenye utumishi wake.”
利未人不必再抬帳幕和其中所用的一切器皿了。」
27 Kwa maneno ya Daudi ya mwisho Walawi walihesabiwa, miaka ishirini na kuendelea.
照着大衛臨終所吩咐的,利未人從二十歲以外的都被數點。
28 Wajibu wao ulikuwa kuwasaidia wazao wa Aruni katika utumishi wa nyumba ya Yahweh. Walikuwa washughulikie nyuani, vyumbani, utakasaji wa vitu vyote vya Yahweh, na kazi zingine katika utumishi wa nyumba ya Mungu.
他們的職任是服事亞倫的子孫,在耶和華的殿和院子,並屋中辦事,潔淨一切聖物,就是辦上帝殿的事務,
29 Pia walishughulikia mkate wa uwepo, unga safi wa mbegu za sadaka, maandazi ya siotiwa chachu, sadaka za ngano, sadaka ziliochanganywa na mafuta, na vipimo vyote vya idadi n a ukubwa wa vitu.
並管理陳設餅,素祭的細麵,或無酵薄餅,或用盤烤,或用油調和的物,又管理各樣的升斗尺度;
30 Pia walisimama kila asubui kumshukuru na kumsifu Yahweh. Pia walifanya hivi jioni
每日早晚,站立稱謝讚美耶和華,
31 na kila wakati sadaka ya kuteketezwa ilipo tolewa kwa Yahweh, siku ya Sabato na sherehe za mwezi mpya na siku za maakuli. Idadi iliyo pangwa, iliyo tolewa kwa amri, ilipaswa kuwa mbele ya Yahweh.
又在安息日、月朔,並節期,按數照例,將燔祭常常獻給耶和華;
32 Walikuwa viongozi wa hema la kukutania, patakatifu, na kuwasaidia ndugu zao wa uzao wa Aruni katika utumishi wa nyumba ya Yahweh.
又看守會幕和聖所,並守耶和華吩咐他們弟兄亞倫子孫的,辦耶和華殿的事。

< 1 Nyakati 23 >