< 1 Nyakati 18 >

1 Baada ya haya Daudi akawashambulia Wafilisti na kuwashinda. Alichukuwa Gathi na vijiji vyake katika utawala wa Wafilisti.
And it cometh to pass after this, that David smiteth the Philistines, and humbleth them, and taketh Gath and its small towns out of the hand of the Philistines;
2 Kisha akamshinda Moabu, na Wamoabu wakawa watumishi wa Daudi na wakamlipa ushuru maalumu.
and he smiteth Moab, and the Moabites are servants to David, bringing a present.
3 Daudi kisha akamshinda Hadadezeri, mfalme wa Zoba huko Hamathi, wakati Hadadezeri alipo kuwa akisafiri kuimarisha utawala wake kwa Mto wa Frati.
And David smiteth Hadarezer king of Zobah, at Hamath, in his going to establish his power by the river Phrat,
4 Daudi akateka magari ya farasi elfu, wanaume wa farasi elfu saba, na wanajeshi wa miguu elfu ishirini. Daudi aliwajeruhi farasi wote wagari, lakini akahifadhi baadhi kwa ajili ya magari ya farasi mia moja.
and David captureth from him a thousand chariots, and seven thousand horsemen, and twenty thousand footmen, and David destroyeth utterly all the chariots, and leaveth of them a hundred chariots [only].
5 Waaramia wa Damasko walipo kuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Zoba, Daudi aliua wanaume elfu ishirini na mbili wa Kiaramia.
And Aram of Damascus cometh in to give help to Hadarezer king of Zobah, and David smiteth in Aram twenty and two thousand men,
6 Kisha Daudi akaweka vikosi huko Aramu ya Damasko, na Waaramia wakawa watumishi wake na wakamletea ushuru maalaumu. Yahweh alimpatia Daudi ushindi popote alipoenda.
and David putteth [garrisons] in Aram of Damascus, and the Aramaeans are to David for servants, bearing a present, and Jehovah giveth salvation to David whithersoever he hath gone.
7 Daudi alichukua ngao za dhahabu zilizo kuwa kwa watumishi wa Hadadezeri na kuleta Yerusalemu.
And David taketh the shields of gold that have been on the servants of Hadarezer, and bringeth them in to Jerusalem;
8 Kutoka Tibhathi na Kuni, miji ya Hadadezeri, Daudi alichukuwa shaba nyingi sana. Ilikuwa shaba hii ambayo baadae Sulemani alifanya saani ya shaba, nguzo, na vifaa vya shaba.
and from Tibhath, and from Chun, cities of Hadarezer, hath David taken very much brass; with it hath Solomon made the brazen sea, and the pillars, and the vessels of brass.
9 Wakati Toi, mfalme wa Hamathi, alipo sikia kuwa Daudi ameshinda majeshi yote ya Hadadezeri mfalme wa Zoba,
And Tou king of Hamath heareth that David hath smitten the whole force of Hadarezer king of Zobah,
10 Toi akamtuma Hadoramu mwanae kwa Mfalme Daudi kumsalimia na kumbariki, kwasababu Daudi amepigana na Hadadezeri na kumshinda, na kwasababu Hadadezeri alifanya vita na Toi. Hadoramu alipeleka vifaa vya fedha, dhahabu, na shaba.
and he sendeth Hadoram his son unto king David, to ask of him of peace, and to bless him (because that he hath fought against Hadarezer, and smiteth him, for a man of wars with Tou had Hadarezer been, ) and all kinds of vessels, of gold, and silver, and brass;
11 Mfalme Daudi alivitenga hivi vitu kwa ajili ya Yahweh, pamoja na fedha na dhahabu aliyo ibeba kutoka kwa mataifa yote: Edomu, Moabu, watu wa Amoni, Wafilisti, na Waamaleki.
also them hath king David sanctified to Jehovah with the silver and the gold that he hath taken from all the nations, from Edom, and from Moab, and from the sons of Ammon, and from the Philistines, and from Amalek.
12 Abishai mwana wa Zeruia akawaua Waedomi elfu kumi na nane katika Bonde la Chumvi.
And Abishai son of Zeruiah hath smitten Edom in the valley of salt — eighteen thousand,
13 Alieka vikosi huko Edomu, na Waedomi wote wakawa watumishi wa Daudi. Yahweh alimpa Daudi ushindi pote alipoenda.
and he putteth in Edom garrisons, and all the Edomites are servants to David; and Jehovah saveth David whithersoever he hath gone.
14 Daudi alitawala Israeli yote, na alitenda haki na utaua kwa watu wote.
And David reigneth over all Israel, and he is doing judgment and righteousness to all his people,
15 Yoabu mwana wa Zeruia walikuwa mkuu wa jeshi, na Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mtunza kumbukumbu.
and Joab son of Zeruiah [is] over the host, and Jehoshaphat son of Ahilud [is] remembrancer,
16 Zadoki mwana wa Ahitubi na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani, na Shavisha alikuwa mwandishi.
and Zadok son of Ahitub, and Abimelech son of Abiathar, [are] priests, and Shavsha [is] scribe,
17 Benaia mwana wa Yehoiada alikuwa mwangalizi wa Wakerethi na Wapelethi, na wana wa Daudi walikuwa washauri wakuu wa mfalme.
and Benaiah son of Jehoiada [is] over the Cherethite and the Pelethite, and the elder sons of David [are] at the hand of the king.

< 1 Nyakati 18 >