< Warumi 6 >

1 Tuseme nini basi? Je, tuendelee kutenda dhambi ili neema ipate kuongezeka?
To what conclusion, then, shall we come? Are we to persist in sinning in order that the grace extended to us may be the greater?
2 La hasha! Sisi tulioifia dhambi, tutawezaje kuendelea kuishi tena katika dhambi?
No, indeed; how shall we who have died to sin, live in it any longer?
3 Au hamjui ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake?
And do you not know that all of us who have been baptized into Christ Jesus were baptized into His death?
4 Kwa hiyo tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti, ili kama vile Kristo alivyofufuliwa kutoka kwa wafu kwa utukufu wa Baba, vivyo hivyo sisi nasi pia tupate kuenenda katika upya wa uzima.
Well, then, we by our baptism were buried with Him in death, in order that, just as Christ was raised from among the dead by the Father's glorious power, we also should live an entirely new life.
5 Kwa maana ikiwa tumeungana naye katika mauti yake, bila shaka tutaungana naye katika ufufuo wake.
For since we have become one with Him by sharing in His death, we shall also be one with Him by sharing in His resurrection.
6 Kwa maana twajua kwamba utu wetu wa kale ulisulubiwa pamoja naye ili ule mwili wa dhambi upate kuangamizwa, nasi tusiendelee kuwa tena watumwa wa dhambi.
This we know--that our old self was nailed to the cross with Him, in order that our sinful nature might be deprived of its power, so that we should no longer be the slaves of sin;
7 Kwa maana mtu yeyote aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi.
for he who has paid the penalty of death stands absolved from his sin.
8 Basi ikiwa tulikufa pamoja na Kristo, tunaamini kwamba pia tutaishi pamoja naye.
But, seeing that we have died with Christ, we believe that we shall also live with Him;
9 Kwa maana tunajua kwamba Kristo, kwa sababu alifufuliwa kutoka kwa wafu, hawezi kufa tena; mauti haina tena mamlaka juu yake.
because we know that Christ, having come back to life, is no longer liable to die.
10 Kifo alichokufa, aliifia dhambi mara moja tu, lakini uzima alio nao anamwishia Mungu.
Death has no longer any power over Him. For by the death which He died He became, once for all, dead in relation to sin; but by the life which He now lives He is alive in relation to God.
11 Vivyo hivyo, jihesabuni wafu katika dhambi lakini mlio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu.
In the same way you also must regard yourselves as dead in relation to sin, but as alive in relation to God, because you are in Christ Jesus.
12 Kwa hiyo, msiruhusu dhambi itawale ndani ya miili yenu, ipatikanayo na kufa, ili kuwafanya mzitii tamaa mbaya.
Let not Sin therefore reign as king in your mortal bodies, causing you to be in subjection to their cravings;
13 Wala msivitoe viungo vya miili yenu vitumike kama vyombo vya uovu vya kutenda dhambi, bali jitoeni kwa Mungu, kama watu waliotolewa kutoka mautini kuingia uzimani. Nanyi vitoeni viungo vya miili yenu kwake kama vyombo vya haki.
and no longer lend your faculties as unrighteous weapons for Sin to use. On the contrary surrender your very selves to God as living men who have risen from the dead, and surrender your several faculties to God, to be used as weapons to maintain the right.
14 Kwa maana dhambi haitakuwa na mamlaka juu yenu, kwa sababu hampo chini ya sheria, bali chini ya neema.
For Sin shall not be lord over you, since you are subjects not of Law, but of grace.
15 Ni nini basi? Je, tutende dhambi kwa kuwa hatuko chini ya sheria bali chini ya neema? La, hasha!
Are we therefore to sin because we are no longer under the authority of Law, but under grace? No, indeed!
16 Je, hamjui kwamba mnapojitoa kwa mtu yeyote kama watumwa watiifu, ninyi ni watumwa wa yule mnayemtii, aidha watumwa wa dhambi, ambayo matokeo yake ni mauti, au watumwa wa utii ambao matokeo yake ni haki?
Do you not know that if you surrender yourselves as bondservants to obey any one, you become the bondservants of him whom you obey, whether the bondservants of Sin (with death as the result) or of Duty (resulting in righteousness)?
17 Lakini Mungu ashukuriwe kwa kuwa ninyi ambao kwanza mlikuwa watumwa wa dhambi, mmekuwa watii kutoka moyoni kwa mafundisho mliyopewa.
But thanks be to God that though you were once in thraldom to Sin, you have now yielded a hearty obedience to that system of truth in which you have been instructed.
18 Nanyi, mkiisha kuwekwa huru mbali na dhambi, mmekuwa watumwa wa haki.
You were set free from the tyranny of Sin, and became the bondservants of Righteousness--
19 Ninasema kwa namna ya kibinadamu kwa sababu ya udhaifu wenu wa hali ya asili. Kama vile mlivyokuwa mkivitoa viungo vya miili yenu kama watumwa wa mambo machafu na uovu uliokuwa ukiongezeka zaidi, hivyo sasa vitoeni viungo vyenu kama watumwa wa haki inayowaelekeza mpate kutakaswa.
your human infirmity leads me to employ these familiar figures--and just as you once surrendered your faculties into bondage to Impurity and ever-increasing disregard of Law, so you must now surrender them into bondage to Righteousness ever advancing towards perfect holiness.
20 Mlipokuwa watumwa wa dhambi, mlikuwa hamtawaliwi na haki.
For when you were the bondservants of sin, you were under no sort of subjection to Righteousness.
21 Lakini mlipata faida gani kwa mambo hayo ambayo sasa mnayaonea aibu? Mwisho wa mambo hayo ni mauti.
At that time, then, what benefit did you get from conduct which you now regard with shame? Why, such things finally result in death.
22 Lakini sasa kwa kuwa mmewekwa huru mbali na dhambi na mmekuwa watumwa wa Mungu, faida mnayopata ni utakatifu, ambao mwisho wake ni uzima wa milele. (aiōnios g166)
But now that you have been set free from the tyranny of Sin, and have become the bondservants of God, you have your reward in being made holy, and you have the Life of the Ages as the final result. (aiōnios g166)
23 Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti, bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu. (aiōnios g166)
For the wages paid by Sin are death; but God's free gift is the Life of the Ages bestowed upon us in Christ Jesus our Lord. (aiōnios g166)

< Warumi 6 >