< Warumi 5 >

1 Kwa hiyo, kwa kuwa tumekwisha kuhesabiwa haki kwa imani, tuna amani na Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
Standing then acquitted as the result of faith, let us enjoy peace with God through our Lord Jesus Christ,
2 ambaye kwa kupitia kwake tumepata kwa njia ya imani kuifikia neema hii ambayo ndani yake sasa tunasimama, nasi twafurahia katika tumaini letu la kushiriki utukufu wa Mungu.
through whom also, as the result of faith, we have obtained an introduction into that state of favour with God in which we stand, and we exult in hope of some day sharing in God's glory.
3 Si hivyo tu, bali twafurahi pia katika mateso, kwa sababu tunajua kuwa mateso huleta saburi,
And not only so: we also exult in our sufferings, knowing as we do, that suffering produces fortitude;
4 nayo saburi huleta uthabiti wa moyo, na uthabiti wa moyo huleta tumaini,
fortitude, ripeness of character; and ripeness of character, hope;
5 wala tumaini halitukatishi tamaa, kwa sababu Mungu amekwisha kumimina pendo lake mioyoni mwetu kwa njia ya Roho Mtakatifu ambaye ametupatia.
and that this hope never disappoints, because God's love for us floods our hearts through the Holy Spirit who has been given to us.
6 Kwa maana hata tulipokuwa dhaifu, wakati ulipowadia, Kristo alikufa kwa ajili yetu sisi wenye dhambi.
For already, while we were still helpless, Christ at the right moment died for the ungodly.
7 Hakika, ni vigumu mtu yeyote kufa kwa ajili ya mwenye haki, ingawa inawezekana mtu akathubutu kufa kwa ajili ya mtu mwema.
Why, it is scarcely conceivable that any one would die for a simply just man, although for a good and lovable man perhaps some one, here and there, will have the courage even to lay down his life.
8 Lakini Mungu anaudhihirisha upendo wake kwetu kwamba: Tulipokuwa tungali wenye dhambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.
But God gives proof of His love to us in Christ's dying for us while we were still sinners.
9 Basi, kwa kuwa sasa tumehesabiwa haki kwa damu yake, si zaidi sana tutaokolewa kutoka ghadhabu ya Mungu kupitia kwake!
If therefore we have now been pronounced free from guilt through His blood, much more shall we be delivered from God's anger through Him.
10 Kwa kuwa kama tulipokuwa adui wa Mungu tulipatanishwa naye kwa njia ya kifo cha Mwanawe, si zaidi sana tukiisha kupatanishwa, tutaokolewa kwa uzima wake.
For if while we were hostile to God we were reconciled to Him through the death of His Son, it is still more certain that now that we are reconciled, we shall obtain salvation through Christ's life.
11 Lakini zaidi ya hayo, pia tunafurahi katika Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kupitia kwake tumepata upatanisho.
And not only so, but we also exult in God through our Lord Jesus Christ, through whom we have now obtained that reconciliation.
12 Kwa hiyo kama vile dhambi ilivyoingia ulimwenguni kupitia kwa mtu mmoja, na kupitia dhambi hii mauti ikawafikia watu wote, kwa sababu wote wamefanya dhambi:
What follows? This comparison. Through one man sin entered into the world, and through sin death, and so death passed to all mankind in turn, in that all sinned.
13 kwa maana kabla sheria haijatolewa, dhambi ilikuwepo ulimwenguni. Lakini dhambi haihesabiwi wakati hakuna sheria.
For prior to the Law sin was already in the world; only it is not entered in the account against us when no Law exists.
14 Hata hivyo, tangu wakati wa Adamu hadi wakati wa Mose, mauti ilitawala watu wote, hata wale ambao hawakutenda dhambi kwa kuvunja amri, kama alivyofanya Adamu, ambaye alikuwa mfano wa yule atakayekuja.
Yet Death reigned as king from Adam to Moses even over those who had not sinned, as Adam did, against Law. And in Adam we have a type of Him whose coming was still future.
15 Lakini ile karama iliyotolewa haikuwa kama lile kosa. Kwa maana ikiwa watu wengi walikufa kwa sababu ya kosa la mtu mmoja, zaidi sana neema ya Mungu na ile karama iliyokuja kwa neema ya mtu mmoja, yaani, Yesu Kristo, imezidi kuwa nyingi kwa ajili ya wengi.
But God's free gift immeasurably outweighs the transgression. For if through the transgression of the one individual the mass of mankind have died, infinitely greater is the generosity with which God's grace, and the gift given in His grace which found expression in the one man Jesus Christ, have been bestowed on the mass of mankind.
16 Tena, ile karama ya Mungu si kama matokeo ya ile dhambi. Hukumu ilikuja kwa njia ya mtu mmoja, ikaleta adhabu, bali karama ya neema ya Mungu ilikuja kwa njia ya makosa mengi, ikaleta kuhesabiwa haki.
And it is not with the gift as it was with the results of one individual's sin; for the judgement which one individual provoked resulted in condemnation, whereas the free gift after a multitude of transgressions results in acquittal.
17 Kwa maana ikiwa kutokana na kosa la mtu mmoja, mauti ilitawala kupitia huyo mtu mmoja, zaidi sana wale wanaopokea wingi wa neema ya Mungu na karama yake ya kuhesabiwa haki, watatawala katika uzima kwa njia ya huyo mtu mmoja, yaani, Yesu Kristo.
For if, through the transgression of the one individual, Death made use of the one individual to seize the sovereignty, all the more shall those who receive God's overflowing grace and gift of righteousness reign as kings in Life through the one individual, Jesus Christ.
18 Kwa hiyo, kama vile kosa la mtu mmoja lilivyoleta adhabu kwa watu wote, vivyo hivyo pia kwa tendo la haki la mtu mmoja lilileta kuhesabiwa haki ambako huleta uzima kwa wote.
It follows then that just as the result of a single transgression is a condemnation which extends to the whole race, so also the result of a single decree of righteousness is a life-giving acquittal which extends to the whole race.
19 Kwa maana kama vile kwa kutokutii kwa yule mtu mmoja wengi walifanywa wenye dhambi, vivyo hivyo kwa kutii kwa mtu mmoja wengi watafanywa wenye haki.
For as through the disobedience of the one individual the mass of mankind were constituted sinners, so also through the obedience of the One the mass of mankind will be constituted righteous.
20 Zaidi ya hayo, sheria ilikuja, ili uvunjaji wa sheria uongezeke. Lakini dhambi ilipoongezeka, neema iliongezeka zaidi,
Now Law was brought in later on, so that transgression might increase. But where sin increased, grace has overflowed;
21 ili kwamba kama vile dhambi ilivyotawala kwa njia ya mauti, vivyo hivyo neema iweze kutawala kwa njia ya kuhesabiwa haki hata kuleta uzima wa milele katika Yesu Kristo Bwana wetu. (aiōnios g166)
in order that as sin has exercised kingly sway in inflicting death, so grace, too, may exercise kingly sway in bestowing a righteousness which results in the Life of the Ages through Jesus Christ our Lord. (aiōnios g166)

< Warumi 5 >