< Zaburi 149 >

1 Msifuni Bwana. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.
Alleluja. Śpiewajcie PANU nową pieśń; niech jego chwała zabrzmi w zgromadzeniu świętych.
2 Israeli na washangilie katika Muumba wao, watu wa Sayuni na wafurahi katika Mfalme wao.
Niech Izrael cieszy się swoim Stwórcą; niech synowie Syjonu radują się swoim Królem.
3 Na walisifu jina lake kwa kucheza na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
Niech chwalą jego imię tańcem; niech grają mu na bębnie i na harfie.
4 Kwa maana Bwana anapendezwa na watu wake, anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.
PAN bowiem swój lud upodobał sobie; zdobi pokornych zbawieniem.
5 Watakatifu washangilie katika heshima hii, na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.
Niech święci się radują w chwale [Bożej], niech śpiewają na swych posłaniach.
6 Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao na upanga ukatao kuwili mikononi mwao,
Niech chwała Boża będzie na ich ustach, a miecz obosieczny w ich rękach;
7 ili walipize mataifa kisasi na adhabu juu ya mataifa,
Aby dokonali zemsty na poganach i ukarali narody;
8 wawafunge wafalme wao kwa minyororo, wakuu wao kwa pingu za chuma,
Aby zakuli ich królów w kajdany, a ich dostojników w żelazne okowy;
9 ili kuwafanyia hukumu iliyoandikwa dhidi yao. Huu ndio utukufu wa watakatifu wake wote. Msifuni Bwana.
Aby wykonali na nich zapisany wyrok. Taka jest chwała wszystkich jego świętych. Alleluja.

< Zaburi 149 >