< Zaburi 146 >

1 Msifuni Bwana! Ee nafsi yangu, umsifu Bwana,
Alleluja. Chwal, duszo moja, PANA.
2 Nitamsifu Bwana maisha yangu yote; nitamwimbia Mungu wangu sifa wakati wote niishipo.
Będę chwalić PANA, póki żyję; będę śpiewał memu Bogu, póki będę istniał.
3 Usiweke tumaini lako kwa wakuu, kwa wanadamu ambao hufa, ambao hawawezi kuokoa.
Nie pokładajcie ufności we władcach [ani w żadnym] synu ludzkim, u którego nie ma wybawienia.
4 Roho yao itokapo hurudi mavumbini, siku hiyo hiyo mipango yao yote hukoma.
Opuszcza go duch i wraca do swojej ziemi; w tymże dniu zginą [wszystkie] jego myśli.
5 Heri yeye ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake ni katika Bwana, Mungu wake,
Błogosławiony ten, kogo pomocą jest Bóg Jakuba, kto nadzieję pokłada w PANU, jego Bogu;
6 Muumba wa mbingu na nchi, na bahari na vyote vilivyomo ndani yake: Bwana anayedumu kuwa mwaminifu milele na milele.
Który uczynił niebo i ziemię, morze i wszystko, co w nich [jest]; który dochowuje prawdy na wieki;
7 Naye huwapatia haki walioonewa na kuwapa wenye njaa chakula. Bwana huwaweka wafungwa huru,
Który oddaje sprawiedliwość pokrzywdzonym [i] daje chleb głodnym; PAN uwalnia więźniów.
8 Bwana huwafumbua vipofu macho, Bwana huwainua waliolemewa na mizigo yao, Bwana huwapenda wenye haki.
PAN otwiera [oczy] ślepych; PAN podnosi przygnębionych; PAN miłuje sprawiedliwych.
9 Bwana huwalinda wageni na kuwategemeza yatima na wajane, lakini hupinga njia za waovu.
PAN strzeże przychodniów, wspomaga sierotę i wdowę, ale krzyżuje drogę niegodziwych.
10 Bwana atamiliki milele, Mungu wako, ee Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Bwana.
PAN będzie królował na wieki, twój Bóg, o Syjonie, z pokolenia na pokolenie. Alleluja.

< Zaburi 146 >