< Zaburi 12 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa sheminithi. Zaburi ya Daudi. Bwana tusaidie, kwa kuwa wacha Mungu wametoweka; waaminifu wametoweka miongoni mwa wanadamu.
Przewodnikowi chóru, na Seminit. Psalm Dawida. Ratuj, PANIE, bo [już] nie ma pobożnego, zniknęli wierni spośród synów ludzkich.
2 Kila mmoja humwambia jirani yake uongo; midomo yao ya hila huzungumza kwa udanganyifu.
Wszyscy mówią kłamliwie do bliźniego, mówią schlebiającymi wargami i z obłudnym sercem.
3 Bwana na akatilie mbali midomo yote ya hila na kila ulimi uliojaa majivuno,
Niech PAN wytępi wszystkie wargi schlebiające [i] język mówiący przechwałki.
4 ule unaosema, “Kwa ndimi zetu tutashinda; midomo ni mali yetu, bwana wetu ni nani?”
Oni mówią: Swoim językiem zwyciężymy, nasze wargi należą do nas, któż jest naszym panem?
5 “Kwa sababu ya uonevu wa wanyonge na kulia kwa uchungu kwa wahitaji, nitainuka sasa,” asema Bwana. “Nitawalinda kutokana na wale wenye nia mbaya juu yao.”
Ze względu na ucisk ubogich [i] jęk nędzarzy teraz powstanę – mówi PAN – zapewnię bezpieczeństwo [temu], na kogo zastawiają sidła.
6 Maneno ya Bwana ni safi, kama fedha iliyosafishwa katika tanuru, iliyosafishwa mara saba.
Słowa PANA to słowa czyste jak srebro wypróbowane w ziemnym tyglu, siedmiokrotnie oczyszczone.
7 Ee Bwana, utatuweka salama na kutulinda na kizazi hiki milele.
Ty, PANIE, zachowasz ich, będziesz ich strzegł od tego pokolenia aż na wieki.
8 Watu waovu huenda wakiringa kila mahali wakati ambapo yule aliye mbaya sana ndiye anayeheshimiwa miongoni mwa watu.
Niegodziwi krążą wokoło, gdy najpodlejsi z ludzi zostają wywyższeni.

< Zaburi 12 >