< Mithali 10 >

1 Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
Przysłowia Salomona. Mądry syn sprawia ojcu radość, a głupi syn [jest] zgryzotą swojej matki.
2 Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
Skarby niegodziwości nie przynoszą pożytku, lecz sprawiedliwość uwalnia od śmierci.
3 Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
PAN nie pozwoli, by dusza sprawiedliwego cierpiała głód, a rozproszy majątek niegodziwych.
4 Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
Leniwa ręka prowadzi do nędzy, a ręka pracowita ubogaca.
5 Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
Kto zbiera w lecie, jest synem roztropnym; syn, który śpi w czasie żniwa, przynosi hańbę.
6 Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
Błogosławieństwa [są] na głowie sprawiedliwego, a usta niegodziwych kryją nieprawość.
7 Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
Pamięć sprawiedliwego jest błogosławiona, a imię niegodziwych zgnije.
8 Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
[Człowiek] mądrego serca przyjmuje przykazania, a gadatliwy głupiec upadnie.
9 Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
Kto postępuje uczciwie, postępuje bezpiecznie, a kto jest przewrotny w swoich drogach, zostanie ujawniony.
10 Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
Kto mruga okiem, przynosi cierpienie, a gadatliwy głupiec upadnie.
11 Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
Usta sprawiedliwego są źródłem życia, a usta niegodziwych kryją nieprawość.
12 Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
Nienawiść wznieca kłótnie, a miłość zakrywa wszystkie grzechy.
13 Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
Na wargach rozumnego znajduje się mądrość, a kij na grzbiecie nierozumnego.
14 Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
Mądrzy gromadzą wiedzę, a usta głupiego grożą zniszczeniem.
15 Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
Majątek bogacza [jest] jego warownym miastem, a zniszczeniem ubogich jest ich nędza.
16 Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
Praca sprawiedliwego [prowadzi] do życia, a dochód niegodziwych do grzechu.
17 Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
Kto przestrzega karności, [idzie] ścieżką życia, a kto gardzi upomnieniem, błądzi.
18 Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
Kto kryje nienawiść kłamliwymi wargami i kto rozgłasza oszczerstwo, jest głupcem.
19 Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
Wielomówność nie bywa bez grzechu, a kto powściąga swoje wargi, jest roztropny.
20 Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
Język sprawiedliwego jest wybornym srebrem, [a] serce niegodziwych jest mało warte.
21 Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
Wargi sprawiedliwego żywią wielu, a głupi umierają przez brak rozumu.
22 Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
Błogosławieństwo PANA wzbogaca i nie przynosi z sobą zmartwień.
23 Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
Dla głupiego popełnić haniebny czyn to zabawa, a człowiek roztropny [trzyma się] mądrości.
24 Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
Niegodziwego spotka to, czego się boi, a sprawiedliwym [Bóg] daje to, czego pragną.
25 Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
Jak wicher przemija, [tak] niegodziwy [nie przetrwa], a sprawiedliwy [ma] wieczny fundament.
26 Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
Czym ocet dla zębów i dym dla oczu, tym [jest] leniwy dla tych, którzy go posyłają.
27 Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
Bojaźń PANA przedłuża dni, a lata niegodziwego będą skrócone.
28 Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
Oczekiwanie sprawiedliwych przynosi radość, a nadzieja niegodziwych zginie.
29 Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
Droga PANA jest mocą dla prawego, a zgubą dla czyniących nieprawość.
30 Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
Sprawiedliwy nigdy się nie zachwieje, a niegodziwi nie będą mieszkać na ziemi.
31 Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
Usta sprawiedliwego wydają mądrość, a język przewrotny będzie wycięty.
32 Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.
Wargi sprawiedliwego wiedzą, co wypada, a usta niegodziwych są przewrotne.

< Mithali 10 >