< Wafilipi 4 >

1 Kwa hiyo, ndugu zangu, ninaowapenda na ambao ninawaonea shauku, ninyi mlio furaha yangu na taji yangu, hivi ndivyo iwapasavyo kusimama imara katika Bwana, ninyi wapenzi wangu.
Therefore, my brethren, dearly loved and longed for, my joy and crown, so stand firm in the Lord, my dearly-loved ones.
2 Nawasihi Euodia na Sintike wawe na nia moja katika Bwana.
I entreat Euodia, and I entreat Syntyche, to be of one mind, as sisters in Christ.
3 Naam, nakusihi wewe pia, mwenzangu mwaminifu, uwasaidie hawa wanawake, kwa sababu walijitaabisha katika kazi ya Injili pamoja nami bega kwa bega, wakiwa pamoja na Klementi na watendakazi wenzangu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima.
Yes, and I beg you also, my faithful yoke-fellow, to help these women who have shared my toil in connection with the Good News, together with Clement and the rest of my fellow labourers, whose names are recorded in the Book of Life.
4 Furahini katika Bwana siku zote, tena nasema furahini!
Always be glad in the Lord: I will repeat it, be glad.
5 Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu.
Let your forbearing spirit be known to every one--the Lord is near.
6 Msijisumbue kwa jambo lolote, bali katika kila jambo kwa kuomba na kusihi pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
Do not be over-anxious about anything, but by prayer and earnest pleading, together with thanksgiving, let your request be unreservedly made known in the presence of God.
7 Nayo amani ya Mungu, inayopita fahamu zote, itailinda mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.
And then the peace of God, which transcends all our powers of thought, will be a garrison to guard your hearts and minds in union with Christ Jesus.
8 Hatimaye, ndugu zangu, mambo yote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo na sifa njema, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote ya kupendeza, yoyote yenye staha, ukiwepo uzuri wowote, pakiwepo chochote kinachostahili kusifiwa, tafakarini mambo hayo.
Finally, brethren, whatever is true, whatever wins respect, whatever is just, whatever is pure, whatever is lovable, whatever is of good repute--if there is any virtue or anything deemed worthy of praise--cherish the thought of these things.
9 Mambo yote mliyojifunza au kuyapokea au kuyasikia kutoka kwangu, au kuyaona kwangu, yatendeni hayo. Naye Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.
The doctrines and the line of conduct which I taught you--both what you heard and what you saw in me-- hold fast to them; and God who gives peace will be with you.
10 Nina furaha kubwa katika Bwana kwamba hatimaye mmeanza upya kushughulika tena na maisha yangu. Kweli mmekuwa mkinifikiria lakini mlikuwa hamjapata nafasi ya kufanya hivyo.
But I rejoice with a deep and holy joy that now at length you have revived your thoughtfulness for my welfare. Indeed you have always been thoughtful for me, although opportunity failed you.
11 Sisemi hivyo kwa vile nina mahitaji, la! Kwa maana nimejifunza kuridhika katika hali yoyote.
I do not refer to this through fear of privation, for (for my part) I have learned, whatever be my outward experiences, to be content.
12 Ninajua kupungukiwa, pia ninajua kuwa na vingi. Nimejifunza siri ya kuridhika katika kila hali, wakati wa kushiba na wakati wa kuona njaa, wakati wa kuwa na vingi na wakati wa kupungukiwa.
I know both how to live in humble circumstances and how to live amid abundance. I am fully initiated into all the mysteries both of fulness and of hunger, of abundance and of want.
13 Naweza kuyafanya mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.
I have strength for anything through Him who gives me power.
14 Lakini, mlifanya vyema kushiriki nami katika taabu zangu.
Yet I thank you for taking your share in my troubles.
15 Zaidi ya hayo, ninyi Wafilipi mnajua kwamba siku za kwanza nilipoanza kuhubiri Injili, nilipoondoka Makedonia, hakuna kanisa jingine lililoshiriki nami katika masuala ya kutoa na kupokea isipokuwa ninyi.
And you men and women of Philippi also know that at the first preaching of the Good News, when I had left Macedonia, no other Church except yourselves held communication with me about giving and receiving;
16 Kwa maana hata nilipokuwa huko Thesalonike, mliniletea msaada kwa ajili ya mahitaji yangu zaidi ya mara moja.
because even in Thessalonica you sent several times to minister to my needs.
17 Si kwamba natafuta sana yale matoleo, bali natafuta sana ile faida itakayozidi sana kwa upande wenu.
Not that I crave for gifts from you, but I do want to see abundant fruit bring you honour.
18 Nimelipwa kikamilifu hata na zaidi; nimetoshelezwa kabisa sasa, kwa kuwa nimepokea kutoka kwa Epafrodito vile vitu mlivyonitumia, sadaka yenye harufu nzuri, dhabihu inayokubalika na ya kumpendeza Mungu.
I have enough of everything--and more than enough. My wants are fully satisfied now that I have received from the hands of Epaphroditus the generous gifts which you sent me--they are a fragrant odor, an acceptable sacrifice, truly pleasing to God.
19 Naye Mungu wangu atawajaza ninyi na kila mnachohitaji kwa kadiri ya utajiri wake katika utukufu ndani ya Kristo Yesu.
But my God--so great is His wealth of glory in Christ Jesus--will fully supply every need of yours.
20 Mungu wetu aliye Baba yetu apewe utukufu milele na milele. Amen. (aiōn g165)
And to our God and Father be the glory throughout the Ages of the Ages! Amen. (aiōn g165)
21 Msalimuni kila mtakatifu katika Kristo Yesu. Ndugu walioko pamoja nami wanawasalimu.
My Christian greetings to every one of God's people. The brethren who are with me send their greetings.
22 Watakatifu wote wanawasalimu, hasa wale watu wa nyumbani mwa Kaisari.
All God's people here greet you--especially the members of Caesar's household.
23 Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho zenu. Amen.
May the grace of our Lord Jesus Christ be with your spirits.

< Wafilipi 4 >