< Wafilipi 3 >

1 Hatimaye, ndugu zangu, furahini katika Bwana! Mimi kuwaandikia mambo yale yale hakuniudhi, kwa maana ni kinga kwa ajili yenu.
In conclusion, my brethren, be joyful in the Lord. For me to give you the same warnings as before is not irksome to me, while so far as you are concerned it is a safe precaution.
2 Jihadharini na mbwa, wale watenda maovu, jihadharini na wale wajikatao miili yao, wasemao ili kuokoka ni lazima kutahiriwa.
Beware of 'the dogs,' the bad workmen, the self-mutilators.
3 Kwa maana sisi ndio tulio tohara, sisi tumwabuduo Mungu katika Roho, tunaona fahari katika Kristo Yesu, ambao hatuweki tumaini letu katika mwili,
For we are the true circumcision--we who render to God a spiritual worship and make our boast in Christ Jesus and have no confidence in outward ceremonies:
4 ingawa mimi mwenyewe ninazo sababu za kuutumainia mwili. Kama mtu yeyote akidhani anazo sababu za kuutumainia mwili, mimi zaidi.
although I myself might have some excuse for confidence in outward ceremonies. If any one else claims a right to trust in them, far more may I:
5 Nilitahiriwa siku ya nane, mimi ni Mwisraeli wa kabila la Benyamini, Mwebrania wa Waebrania. Kwa habari ya sheria, ni Farisayo,
circumcised, as I was, on the eighth day, a member of the race of Israel and of the tribe of Benjamin, a Hebrew sprung from Hebrews; as to the Law a Pharisee;
6 kwa habari ya juhudi, nilikuwa nalitesa kanisa, kuhusu haki ipatikanayo kwa sheria, mimi nilikuwa sina hatia.
as to zeal, a persecutor of the Church; as to the righteousness which comes through Law, blameless.
7 Lakini mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, sasa nayahesabu kuwa hasara kwa ajili ya Kristo.
Yet all that was gain to me--for Christ's sake I have reckoned it loss.
8 Zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara tupu nikiyalinganisha na faida kubwa ipitayo kiasi cha kumjua Kristo Yesu Bwana wangu, ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote, nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nimpate Kristo.
Nay, I even reckon all things as pure loss because of the priceless privilege of knowing Christ Jesus my Lord. And for His sake I have suffered the loss of everything, and reckon it all as mere refuse, in order that I may win Christ and be found in union with Him,
9 Nami nionekane mbele zake bila kuwa na haki yangu mwenyewe ipatikanayo kwa sheria, bali ile ipatikanayo kwa imani katika Kristo, haki ile itokayo kwa Mungu kwa njia ya imani.
not having a righteousness of my own, derived from the Law, but that which arises from faith in Christ--the righteousness which comes from God through faith.
10 Nataka nimjue Kristo na uweza wa kufufuka kwake na ushirika wa mateso yake, ili nifanane naye katika mauti yake,
I long to know Christ and the power which is in His resurrection, and to share in His sufferings and die even as He died;
11 ili kwa njia yoyote niweze kufikia ufufuo wa wafu.
in the hope that I may attain to the resurrection from among the dead.
12 Si kwamba nimekwisha kufikia, au kwamba nimekwisha kuwa mkamilifu, la hasha! Bali nakaza mwendo ili nipate kile ambacho kwa ajili yake, nimeshikwa na Kristo Yesu.
I do not say that I have already won the race or have already reached perfection. But I am pressing on, striving to lay hold of the prize for which also Christ has laid hold of me.
13 Ndugu zangu, sijihesabu kuwa nimekwisha kushika. Lakini ninafanya jambo moja: Ninasahau mambo yale yaliyopita, nakaza mwendo kufikia yale yaliyo mbele.
Brethren, I do not imagine that I have yet laid hold of it. But this one thing I do--forgetting everything which is past and stretching forward to what lies in front of me,
14 Nakaza mwendo nifikie ile alama ya ushindi iliyowekwa ili nipate tuzo ya mwito mkuu wa Mungu ambao nimeitiwa huko juu mbinguni katika Kristo Yesu.
with my eyes fixed on the goal I push on to secure the prize of God's heavenward call in Christ Jesus.
15 Hivyo sisi sote tuliokuwa kiroho tuwaze jambo hili, hata mkiwaza mengine katika jambo lolote, Mungu ataliweka wazi hilo nalo.
Therefore let all of us who are mature believers cherish these thoughts; and if in any respect you think differently, that also God will make clear to you.
16 Lakini na tushike sana lile ambalo tumekwisha kulifikia.
But whatever be the point that we have already reached, let us persevere in the same course.
17 Ndugu zangu, kwa pamoja fuateni mfano wangu na kuwatazama wale wanaofuata kielelezo tulichowawekea.
Brethren, vie with one another in imitating me, and carefully observe those who follow the example which we have set you.
18 Kwa maana, kama nilivyokwisha kuwaambia mara nyingi kabla, nami sasa nasema tena hata kwa machozi, watu wengi wanaishi kama adui wa msalaba wa Kristo.
For there are many whom I have often described to you, and I now even with tears describe them, as being enemies to the Cross of Christ.
19 Mwisho wa watu hao ni maangamizi, Mungu wao ni tumbo, na utukufu wao ni aibu, na mawazo yao yamo katika mambo ya dunia.
Their end is destruction, their bellies are their God, their glory is in their shame, and their minds are devoted to earthly things.
20 Lakini uenyeji wetu uko mbinguni. Nasi tunamngoja kwa shauku Mwokozi kutoka huko, yaani, Bwana Yesu Kristo,
We, however, are free citizens of Heaven, and we are waiting with longing expectation for the coming from Heaven of a Saviour, the Lord Jesus Christ,
21 atakayeubadili mwili wetu wa unyonge, ili upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uweza ule ambao kwa huo aweza hata kuvitiisha vitu vyote chini yake.
who, in the exercise of the power which He has even to subject all things to Himself, will transform this body of our humiliation until it resembles His own glorious body.

< Wafilipi 3 >