< Mathayo 7 >

1 “Usihukumu ili usije ukahukumiwa.
"Judge not, that you may not be judged;
2 Kwa maana jinsi unavyowahukumu wengine, ndivyo utakavyohukumiwa, na kwa kipimo kile upimiacho, ndicho utakachopimiwa.
for your own judgement will be dealt--and your own measure meted--to yourselves.
3 “Mbona unatazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na wala huoni boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe?
And why do you look at the splinter in your brother's eye, and not notice the beam which is in your own eye?
4 Au unawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Acha nitoe kibanzi kwenye jicho lako,’ wakati kuna boriti kwenye jicho lako mwenyewe?
Or how say to your brother, 'Allow me to take the splinter out of your eye,' while the beam is in your own eye?
5 Ewe mnafiki, ondoa boriti ndani ya jicho lako kwanza, ndipo utaweza kuona dhahiri jinsi ya kuondoa kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako.
Hypocrite, first take the beam out of your own eye, and then you will see clearly how to remove the splinter from your brother's eye.
6 “Msiwape mbwa vitu vilivyo vitakatifu; wala msitupie nguruwe lulu zenu. Kama mkifanya hivyo, watazikanyagakanyaga na kisha watawageukia na kuwararua vipande vipande.
"Give not that which is holy to the dogs, nor throw your pearls to the swine; otherwise they will trample them under their feet and then turn and attack you.
7 “Ombeni nanyi mtapewa; tafuteni nanyi mtapata; bisheni nanyi mtafunguliwa mlango.
"Ask, and it will be given to you; seek, and you will find; knock, and the door will be opened to you.
8 Kwa kuwa kila aombaye hupewa; naye kila atafutaye hupata; na kila abishaye hufunguliwa mlango.
For it is always he who asks that receives, he who seeks that finds, and he who knocks that has the door opened to him.
9 “Au ni nani miongoni mwenu ambaye mwanawe akimwomba mkate atampa jiwe?
What man is there among you, who if his son shall ask him for bread will offer him a stone?
10 Au mwanawe akimwomba samaki atampa nyoka?
Or if the son shall ask him for a fish will offer him a snake?
11 Ikiwa ninyi basi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa vitu vizuri wale wamwombao?
If you then, imperfect as you are, know how to give good gifts to your children, how much more will your Father in Heaven give good things to those who ask Him!
12 Kwa hiyo chochote mnachotaka mtendewe na watu, ninyi nanyi watendeeni vivyo hivyo. Kwa kuwa hii ndiyo Sheria na Manabii.
Everything, therefore, be it what it may, that you would have men do to you, do you also the same to them; for in this the Law and the Prophets are summed up.
13 “Ingieni kupitia mlango mwembamba, kwa maana lango ni pana na njia ni pana ielekeayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa kupitia lango hilo.
"Enter by the narrow gate; for wide is the gate and broad the road which leads to ruin, and many there are who enter by it;
14 Lakini mlango ni mwembamba na njia ni finyu ielekeayo kwenye uzima, nao ni wachache tu waionao.
because narrow is the gate and contracted the road which leads to Life, and few are those who find it.
15 “Jihadharini na manabii wa uongo, wanaowajia wakiwa wamevaa mavazi ya kondoo, lakini ndani ni mbwa mwitu wakali.
"Beware of the false teachers--men who come to you in sheep's fleeces, but beneath that disguise they are ravenous wolves.
16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je, watu huchuma zabibu kwenye miiba, au tini kwenye michongoma?
By their fruits you will easily recognize them. Are grapes gathered from thorns or figs from brambles?
17 Vivyo hivyo, mti mwema huzaa matunda mazuri, na mti mbaya huzaa matunda mabaya.
Just so every good tree produces good fruit, but a poisonous tree produces bad fruit.
18 Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mazuri.
A good tree cannot bear bad fruit, nor a poisonous tree good fruit.
19 Kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.
Every tree which does not yield good fruit is cut down and thrown aside for burning.
20 Hivyo, mtawatambua kwa matunda yao.
So by their fruits at any rate, you will easily recognize them.
21 “Si kila mtu aniambiaye, ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika Ufalme wa Mbinguni, bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
"Not every one who says to me, 'Master, Master,' will enter the Kingdom of the Heavens, but only those who are obedient to my Father who is in Heaven.
22 Wengi wataniambia siku ile, ‘Bwana, Bwana, hatukutoa unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo wachafu na kufanya miujiza mingi?’
Many will say to me on that day, "'Master, Master, have we not prophesied in Thy name, and in Thy name expelled demons, and in Thy name performed many mighty works?'
23 Ndipo nitakapowaambia wazi, ‘Sikuwajua kamwe. Ondokeni kwangu, ninyi watenda maovu!’
"And then I will tell them plainly, "'I never knew you: begone from me, you doers of wickedness.'
24 “Kwa hiyo kila mtu ayasikiaye haya maneno yangu na kuyatenda, ni kama mtu mwenye busara aliyejenga nyumba yake kwenye mwamba.
"Every one who hears these my teachings and acts upon them will be found to resemble a wise man who builds his house upon rock;
25 Mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, na upepo ukavuma ukaipiga hiyo nyumba. Lakini haikuanguka; kwa sababu msingi wake ulikuwa kwenye mwamba.
and the heavy rain falls, the swollen torrents come, and the winds blow and beat against the house; yet it does not fall, for its foundation is on rock.
26 Naye kila anayesikia haya maneno yangu wala asiyatende, ni kama mtu mjinga aliyejenga nyumba yake kwenye mchanga.
And every one who hears these my teachings and does not act upon them will be found to resemble a fool who builds his house upon sand.
27 Mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, nao upepo ukavuma ukaipiga hiyo nyumba, nayo ikaanguka kwa kishindo kikubwa.”
The heavy rain descends, the swollen torrents come, and the winds blow and burst upon the house, and it falls; and disastrous is the fall."
28 Yesu alipomaliza kusema maneno haya, makutano ya watu wakashangazwa sana na mafundisho yake,
When Jesus had concluded this discourse, the crowds were filled with amazement at His teaching,
29 kwa sababu alifundisha kama yeye aliye na mamlaka, wala si kama walimu wao wa sheria.
for He had been teaching them as one who had authority, and not as their Scribes taught.

< Mathayo 7 >