< Mathayo 6 >

1 “Angalieni msitende wema wenu mbele ya watu ili wawaone. Kwa maana mkifanya hivyo, hamna thawabu kutoka kwa Baba yenu aliye mbinguni.
"But beware of doing your good actions in the sight of men, in order to attract their gaze; if you do, there is no reward for you with your Father who is in Heaven.
2 “Hivyo mnapowapa wahitaji, msipige panda mbele yenu kama wafanyavyo wanafiki katika masinagogi na mitaani, ili wasifiwe na watu. Amin nawaambia wao wamekwisha kupokea thawabu yao.
'When you give in charity, never blow a trumpet before you as the hypocrites do in the synagogues and streets in order that their praises may be sung by men. I solemnly tell you that they already have their reward.
3 Lakini ninyi mtoapo sadaka, fanyeni kwa siri, hata mkono wako wa kushoto usijue mkono wako wa kuume unachofanya,
But when you are giving in charity, let not your left hand perceive what your right hand is doing,
4 ili sadaka yako iwe ni siri. Ndipo Baba yako wa mbinguni, yeye aonaye sirini atakupa thawabu kwa wazi.
that your charities may be in secret; and then your Father--He who sees in secret--will recompense you.
5 “Nanyi msalipo, msiwe kama wanafiki, maana wao hupenda kusali wakiwa wamesimama katika masinagogi na kando ya barabara ili waonekane na watu. Amin nawaambia, wao wamekwisha kupata thawabu yao.
"And when praying, you must not be like the hypocrites. They are fond of standing and praying in the synagogues or at the corners of the wider streets, in order that men may see them. I solemnly tell you that they already have their reward.
6 Lakini wewe unaposali, ingia chumbani mwako, funga mlango na umwombe Baba yako aliye sirini. Naye Baba yako aonaye sirini atakupa thawabu yako.
But you, whenever you pray, go into your own room and shut the door: then pray to your Father who is in secret, and your Father--He who sees in secret--will recompense you.
7 Nanyi mnaposali msiseme maneno kama wafanyavyo watu wasiomjua Mungu. Kwa maana wao hudhani kwamba watasikiwa kwa sababu ya wingi wa maneno yao.
"And when praying, do not use needless repetitions as the Gentiles do, for they expect to be listened to because of their multitude of words.
8 Msiwe kama wao, kwa sababu Baba yenu anajua kile mnachohitaji kabla hamjamwomba.
Do not, however, imitate them; for your Father knows what things you need before ever you ask Him.
9 “Hivi basi, ndivyo iwapasavyo kuomba: “‘Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe.
"In this manner therefore pray: 'Our Father who art in Heaven, may Thy name be kept holy;
10 Ufalme wako uje. Mapenzi yako yafanyike hapa duniani kama huko mbinguni.
let Thy kingdom come; let Thy will be done, as in Heaven so on earth;
11 Utupatie riziki yetu ya kila siku.
give us to-day our bread for the day;
12 Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tulivyokwisha kuwasamehe wadeni wetu.
and forgive us our shortcomings, as we also have forgiven those who have failed in their duty towards us;
13 Usitutie majaribuni, bali utuokoe kutoka kwa yule mwovu [kwa kuwa Ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amen].’
and bring us not into temptation, but rescue us from the Evil one.'
14 Kwa kuwa kama mkiwasamehe watu wengine wanapowakosea, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi pia.
"For if you forgive others their offences, your Heavenly Father will forgive you also;
15 Lakini msipowasamehe watu wengine makosa yao, naye Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.
but if you do not forgive others their offences, neither will your Father forgive yours.
16 “Mnapofunga, msiwe wenye huzuni kama wafanyavyo wanafiki. Maana wao hukunja nyuso zao ili kuwaonyesha wengine kwamba wamefunga. Amin, amin nawaambia wao wamekwisha kupata thawabu yao kamilifu.
"When any of you fast, never assume gloomy looks as the hypocrites do; for they disfigure their faces in order that it may be evident to men that they are fasting. I solemnly tell you that they already have their reward.
17 Lakini mnapofunga, jipakeni mafuta kichwani na kunawa nyuso zenu
But, whenever you fast, pour perfume on your hair and wash your face,
18 ili kufunga kwenu kusionekane na watu wengine ila Baba yenu aketiye mahali pa siri; naye Baba yenu aonaye sirini atawapa thawabu yenu kwa wazi.
that it may not be apparent to men that you are fasting, but to your Father who is in secret; and your Father--He who sees in secret--will recompense you.
19 “Msijiwekee hazina duniani, mahali ambapo nondo na kutu huharibu, nao wevi huvunja na kuiba.
"Do not lay up stores of wealth for yourselves on earth, where the moth and wear-and-tear destroy, and where thieves break in and steal.
20 Lakini jiwekeeni hazina mbinguni, mahali ambapo nondo na kutu haviharibu, wala wevi hawavunji na kuiba.
But amass wealth for yourselves in Heaven, where neither the moth nor wear-and-tear destroys, and where thieves do not break in and steal.
21 Kwa sababu mahali hazina yako ilipo, hapo ndipo pia moyo wako utakapokuwa.
For where your wealth is, there also will your heart be.
22 “Jicho ni taa ya mwili. Kama jicho lako ni nyofu, mwili wako wote utajaa nuru.
"The eye is the lamp of the body. If then your eyesight is good, your whole body will be well lighted;
23 Lakini kama jicho lako ni ovu, mwili wako wote utajawa na giza. Kwa hiyo basi, kama nuru iliyomo ndani yako ni giza, hilo ni giza kuu namna gani!
but if your eyesight is bad, your whole body will be dark. If however the very light within you is darkness, how dense must the darkness be!
24 “Hakuna mtu awezaye kuwatumikia mabwana wawili. Kwa kuwa atamchukia huyu na kumpenda yule mwingine, au atashikamana sana na huyu na kumdharau yule mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu pamoja na Mali.
"No man can be the bondservant of two masters; for either he will dislike one and like the other, or he will attach himself to one and think slightingly of the other. You cannot be the bondservants both of God and of gold.
25 “Kwa hiyo nawaambia, msisumbukie maisha yenu kwamba mtakula nini au mtakunywa nini; au msumbukie miili yenu kwamba mtavaa nini. Je, maisha si zaidi ya chakula, na mwili zaidi ya mavazi?
For this reason I charge you not to be over-anxious about your lives, inquiring what you are to eat or what you are to drink, nor yet about your bodies, inquiring what clothes you are to put on. Is not the life more precious than its food, and the body than its clothing?
26 Waangalieni ndege wa angani; wao hawapandi wala hawavuni au kuweka ghalani, lakini Baba yenu wa mbinguni huwalisha. Je, ninyi si wa thamani zaidi kuliko hao ndege?
Look at the birds which fly in the air: they do not sow or reap or store up in barns, but your Heavenly Father feeds them: are not you of much greater value than they?
27 Ni nani miongoni mwenu ambaye kwa kujitaabisha kwake anaweza kujiongezea hata saa moja zaidi katika maisha yake?
Which of you by being over-anxious can add a single foot to his height?
28 “Nanyi kwa nini mnajitaabisha kwa ajili ya mavazi? Fikirini maua ya shambani yameavyo. Hayafanyi kazi wala hayafumi.
And why be anxious about clothing? Learn a lesson from the wild lilies. Watch their growth. They neither toil nor spin,
29 Lakini nawaambia, hata Solomoni katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo ya hayo maua.
and yet I tell you that not even Solomon in all his magnificence could array himself like one of these.
30 Basi ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya shambani, ambayo leo yapo na kesho yanatupwa motoni, je, hatawavika ninyi vizuri zaidi, enyi wa imani haba?
And if God so clothes the wild herbage which to-day flourishes and to-morrow is thrown into the oven, is it not much more certain that He will clothe you, you men of little faith?
31 Kwa hiyo msiwe na wasiwasi, mkisema, ‘Tutakula nini?’ au ‘Tutakunywa nini?’ au ‘Tutavaa nini?’
Do not be over-anxious, therefore, asking 'What shall we eat?' or 'What shall we drink?' or 'What shall we wear?'
32 Watu wasiomjua Mungu ndio wanaoshindania hayo, lakini Baba yenu wa mbinguni anafahamu kuwa mnahitaji haya yote.
For all these are questions that Gentiles are always asking; but your Heavenly Father knows that you need these things--all of them.
33 Lakini utafuteni kwanza Ufalme wa Mungu na haki yake, na haya yote atawapa pia.
But make His Kingdom and righteousness your chief aim, and then these things shall all be given you in addition.
34 Kwa hiyo msiwe na wasiwasi kuhusu kesho, kwa sababu kesho itajitaabikia yenyewe. Yatosha kwa siku masumbufu yake.
Do not be over-anxious, therefore, about to-morrow, for to-morrow will bring its own cares. Enough for each day are its own troubles.

< Mathayo 6 >