< Luka 3 >

1 Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato akiwa mtawala wa Uyahudi, Herode akiwa mfalme wa Galilaya, Filipo ndugu yake akiwa mfalme wa Iturea na nchi ya Trakoniti, na Lisania akiwa mfalme wa Abilene,
Now in the fifteenth year of the reign of Tiberius Caesar, Pontius Pilate being Governor of Judaea, Herod Tetrarch of Galilee, his brother Philip Tetrarch of Ituraea and Trachonitis, and Lysanias Tetrarch of Abilene,
2 nao Anasi na Kayafa wakiwa makuhani wakuu, neno la Mungu likamjia Yohana, mwana wa Zekaria huko jangwani.
during the High-priesthood of Annas and Caiaphas, a message from God came to John, the son of Zechariah, in the Desert.
3 Akaenda katika nchi yote kandokando ya Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
John went into all the district about the Jordan proclaiming a baptism of the penitent for the forgiveness of sins;
4 Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.
as it is written in the book of the prophet Isaiah, "The voice of one crying aloud! 'In the Desert prepare ye a road for the Lord: make His highway straight.
5 Kila bonde litajazwa, kila mlima na kilima vitashushwa. Njia zilizopinda zitanyooshwa, na zilizoparuza zitasawazishwa.
Every ravine shall be filled up, and every mountain and hill levelled down, the crooked places shall be turned into straight roads, and the rugged ways into smooth;
6 Nao watu wote watauona wokovu wa Mungu.’”
and then shall all mankind see God's salvation.'"
7 Yohana akauambia ule umati wa watu uliokuwa unakuja ili kubatizwa naye, “Ninyi watoto wa nyoka! Ni nani aliyewaonya kuikimbia ghadhabu inayokuja?
Accordingly John used to say to the crowds who came out to be baptized by him, "O vipers' brood, who has warned you to flee from the coming wrath?
8 Basi zaeni matunda yastahiliyo toba. Wala msianze kusema mioyoni mwenu kuwa, ‘Sisi tunaye Abrahamu, baba yetu.’ Kwa maana nawaambia kuwa Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka mawe haya.
Live lives which shall prove your change of heart; and do not begin to say to yourselves, 'We have Abraham as our forefather,' for I tell you that God can raise up descendants for Abraham from these stones.
9 Hata sasa shoka limeshawekwa tayari kwenye shina la kila mti. Basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.”
And even now the axe is lying at the root of the trees, so that every tree which fails to yield good fruit will quickly be hewn down and thrown into the fire."
10 Ule umati wa watu ukamuuliza, “Inatupasa tufanyeje basi?”
The crowds repeatedly asked him, "What then are we to do?"
11 Yohana akawaambia, “Aliye na kanzu mbili amgawie asiye nayo, naye aliye na chakula na afanye vivyo hivyo.”
"Let the man who has two coats," he answered, "give one to the man who has none; and let the man who has food share it with others."
12 Watoza ushuru nao wakaja ili wabatizwe, wakamuuliza, “Bwana na sisi inatupasa tufanyeje?”
There came also a party of tax-gatherers to be baptized, and they asked him, "Rabbi, what are we to do?"
13 Akawaambia, “Msichukue zaidi ya kiwango mlichopangiwa.”
"Do not exact more than the legal amount," he replied.
14 Askari nao wakamuuliza, “Je, nasi inatupasa tufanye nini?” Akawaambia, “Msimdhulumu mtu wala msimshtaki mtu kwa uongo, bali mridhike na mishahara yenu.”
The soldiers also once and again inquired of him, "And we, what are we to do?" His answer was, "Neither intimidate any one nor lay false charges; and be content with your pay."
15 Watu walikuwa na matazamio makubwa. Wakawa wanajiuliza mioyoni mwao iwapo Yohana angeweza kuwa ndiye Kristo.
And while the people were in suspense and all were debating in their minds whether John might possibly be the Anointed One,
16 Yohana akawajibu akawaambia, “Mimi nawabatiza kwa maji. Lakini atakuja aliye na nguvu kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
he answered the question by saying to them all, "As for me, I am baptizing you with water, but One mightier than I is coming, whose very sandal-strap I am not worthy to unfasten: He will baptize you in the Holy Spirit and with fire.
17 Pepeto lake liko mkononi, tayari kusafisha sakafu yake ya kupuria na kuikusanya ngano ghalani, lakini makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.”
His winnowing-shovel is in His hand to clear out His threshing-floor, and to gather the wheat into His storehouse; but the chaff He will burn up in fire unquenchable."
18 Basi, kwa maonyo mengine mengi Yohana aliwasihi na kuwahubiria watu Habari Njema.
With many exhortations besides these he declared the Good News to the people.
19 Lakini Yohana alipomkemea Mfalme Herode kuhusu uhusiano wake na Herodia, mke wa ndugu yake, na maovu mengine aliyokuwa amefanya,
But Herod the Tetrarch, being repeatedly rebuked by him about Herodias his brother's wife, and about all the wicked deeds that he had done,
20 Herode aliongezea jambo hili kwa hayo mengine yote: alimfunga Yohana gerezani.
now added this to crown all the rest, that he threw John into prison.
21 Baada ya watu wote kubatizwa, Yesu naye akabatizwa. Naye alipokuwa akiomba, mbingu zilifunguka.
Now when all the people had been baptized, and Jesus also had been baptized and was praying, the sky opened,
22 Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa umbo kama la hua, nayo sauti kutoka mbinguni ikasema: “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
and the Holy Spirit came down in bodily shape, like a dove, upon Him, and a voice came from Heaven, which said, "Thou art My Son, dearly loved: in Thee is My delight."
23 Yesu alikuwa na umri wa miaka thelathini alipoanza huduma yake. Alikuwa akidhaniwa kuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Eli,
And He--Jesus--when He began His ministry, was about thirty years old. He was the son (it was supposed) of Joseph, son of Heli,
24 Eli alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi, Lawi alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Yanai, Yanai alikuwa mwana wa Yosefu,
son of Matthat, son of Levi, son of Melchi, son of Jannai, son of Joseph,
25 Yosefu alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Amosi, Amosi alikuwa mwana wa Nahumu, Nahumu alikuwa mwana wa Esli, Esli alikuwa mwana wa Nagai,
son of Mattathias, son of Amos, son of Nahum, son of Esli, son of Naggai,
26 Nagai alikuwa mwana wa Maathi, Maathi alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Semeini, Semeini alikuwa mwana wa Yoseki, Yoseki alikuwa mwana wa Yoda,
son of Mahath, son of Mattathias, son of Semein, son of Josech, son of Joda,
27 Yoda alikuwa mwana wa Yoanani, Yoanani alikuwa mwana wa Resa, Resa alikuwa mwana wa Zerubabeli, Zerubabeli alikuwa mwana wa Shealtieli, Shealtieli alikuwa mwana wa Neri,
son of Johanan, son of Resa, son of Zerubbabel, son of Shealtiel, son of Neri,
28 Neri alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Adi, Adi alikuwa mwana wa Kosamu, Kosamu alikuwa mwana wa Elmadamu, Elmadamu alikuwa mwana wa Eri,
son of Melchi, son of Addi, son of Cosam, son of Elmadam, son of Er,
29 Eri alikuwa mwana wa Yoshua, Yoshua alikuwa mwana wa Eliezeri, Eliezeri alikuwa mwana wa Yorimu, Yorimu alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi,
son of Joshua, son of Eliezar, son of Jorim, son of Maththat, son of Levi,
30 Lawi alikuwa mwana wa Simeoni, Simeoni alikuwa mwana wa Yuda, Yuda alikuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Yonamu, Yonamu alikuwa mwana wa Eliakimu, Eliakimu alikuwa mwana wa Melea,
son of Symeon, son of Judah, son of Joseph, son of Jonam, son of Eliakim, son of
31 Melea alikuwa mwana wa Mena, Mena alikuwa mwana wa Matatha, Matatha alikuwa mwana wa Nathani, Nathani alikuwa mwana wa Daudi,
Melea, son of Menna, son of Mattatha, son of Nathan, son of David,
32 Daudi alikuwa mwana wa Yese, Yese alikuwa mwana wa Obedi, Obedi alikuwa mwana wa Boazi, Boazi alikuwa mwana wa Salmoni, Salmoni alikuwa mwana wa Nashoni,
son of Jesse, son of Obed, son of Boaz, son of Salmon, son of Nahshon,
33 Nashoni alikuwa mwana wa Aminadabu, Aminadabu alikuwa mwana wa Aramu, Aramu alikuwa mwana wa Hesroni, Hesroni alikuwa mwana wa Peresi, Peresi alikuwa mwana wa Yuda,
son of Amminadab, son of Admin, son of Arni, son of Hezron, son of Perez, son of Judah,
34 Yuda alikuwa mwana wa Yakobo, Yakobo alikuwa mwana wa Isaki, Isaki alikuwa mwana wa Abrahamu, Abrahamu alikuwa mwana wa Tera, Tera alikuwa mwana wa Nahori,
son of Jacob, son of Isaac, son of Abraham, son of Terah, son of Nahor,
35 Nahori alikuwa mwana wa Serugi, Serugi alikuwa mwana wa Reu, Reu alikuwa mwana wa Pelegi, Pelegi alikuwa mwana wa Eberi, Eberi alikuwa mwana wa Sala,
son of Serug, son of Reu, son of Peleg, son of Eber, son of Shelah,
36 Sala alikuwa mwana wa Kenani, Kenani alikuwa mwana wa Arfaksadi, Arfaksadi alikuwa mwana wa Shemu, Shemu alikuwa mwana wa Noa, Noa alikuwa mwana wa Lameki,
son of Cainan, son of Arpachshad, son of Shem, son of Noah, son of Lamech,
37 Lameki alikuwa mwana wa Methusela, Methusela alikuwa mwana wa Enoki, Enoki alikuwa mwana wa Yaredi, Yaredi alikuwa mwana wa Mahalaleli, Mahalaleli alikuwa mwana wa Kenani,
son of Methuselah, son of Enoch, son of Jared, son of Mahalalel, son of Kenan,
38 Kenani alikuwa mwana wa Enoshi, Enoshi alikuwa mwana wa Sethi, Sethi alikuwa mwana wa Adamu, Adamu alikuwa mwana wa Mungu.
son of Enosh, son of Seth, son of Adam, son of God.

< Luka 3 >