< Luka 22 >

1 Wakati huu Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa imekaribia.
Now the feast of unleavened bread was near, which is called the Passover.
2 Viongozi wa makuhani na walimu wa sheria walikuwa wanatafuta njia ya kumuua Yesu, kwa sababu waliwaogopa watu.
And the chief priests and the scribes were looking for a chance to put him to death, but they went in fear of the people.
3 Shetani akamwingia Yuda, aliyeitwa Iskariote, mmoja wa wale Kumi na Wawili.
And Satan came into Judas Iscariot, who was one of the twelve.
4 Yuda akaenda kwa viongozi wa makuhani na kwa maafisa wa walinzi wa Hekalu, akazungumza nao jinsi ambavyo angeweza kumsaliti Yesu.
And he went away and had a discussion with the chief priests and the rulers, about how he might give him up to them.
5 Wakafurahi na wakakubaliana kumpa fedha.
And they were glad, and undertook to give him money.
6 Naye akakubali, akaanza kutafuta wakati uliofaa wa kumsaliti Yesu kwao, wakati ambapo hakuna umati wa watu.
And he made an agreement with them to give him up to them, if he got a chance, when the people were not present.
7 Basi ikawadia siku ya Mikate Isiyotiwa Chachu, siku ambayo mwana-kondoo wa Pasaka huchinjwa.
And the day of unleavened bread came, when the Passover lamb is put to death.
8 Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohana, akisema, “Nendeni mkatuandalie chakula cha Pasaka ili tuweze kuila.”
And Jesus sent Peter and John, saying, Go and make the Passover ready for us, so that we may take it.
9 Wakamuuliza, “Unataka tukuandalie wapi?”
And they said to him, Where are we to get it ready?
10 Yesu akawaambia, “Tazameni, mtakapokuwa mkiingia mjini, mtakutana na mwanaume amebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka kwenye nyumba atakayoingia.
And he said to them, When you go into the town you will see a man coming to you with a vessel of water; go after him into the house into which he goes.
11 Nanyi mwambieni mwenye nyumba, ‘Mwalimu anauliza: Kiko wapi chumba cha wageni, ambamo mimi na wanafunzi wangu tutakula Pasaka?’
And say to the master of the house, The Master says, Where is the guest-room, where I may take the Passover with my disciples?
12 Atawaonyesha chumba kikubwa ghorofani, kikiwa kimepambwa vizuri. Andaeni humo.”
And he will take you up to a great room with a table and seats: there make ready.
13 Wakaenda, nao wakakuta kila kitu kama Yesu alivyowaambia. Hivyo wakaiandaa Pasaka.
And they went, and it was as he had said: and they made the Passover ready.
14 Wakati ulipowadia, Yesu akaketi mezani pamoja na wale mitume wake.
And when the time had come, he took his seat, and the Apostles with him.
15 Kisha akawaambia, “Nimetamani sana kuila Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
And he said, I have had a great desire to keep this Passover with you before I come to my death;
16 Kwa maana, nawaambia, sitaila tena Pasaka mpaka itakapotimizwa katika Ufalme wa Mungu.”
For I say to you, I will not take it till it is made complete in the kingdom of God.
17 Akiisha kukichukua kikombe, akashukuru, akasema, “Chukueni hiki mnywe wote.
And he took a cup and, having given praise, he said, Make division of this among yourselves;
18 Kwa maana nawaambia tangu sasa sitakunywa tena katika uzao wa mzabibu, hadi Ufalme wa Mungu utakapokuja.”
For I say to you, I will not take of the fruit of the vine till the kingdom of God has come.
19 Kisha akachukua mkate, akashukuru, akaumega, na kuwapa, akisema, “Huu ni mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.”
And he took bread and, having given praise, he gave it to them when it had been broken, saying, This is my body, which is given for you: do this in memory of me.
20 Vivyo hivyo baada ya kula, akakitwaa kikombe, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu, imwagikayo kwa ajili yenu.
And in the same way, after the meal, he took the cup, saying, This cup is the new testament, made with my blood which is given for you.
21 Lakini mkono wake huyo atakayenisaliti uko hapa mezani pamoja nami.
But the hand of him who is false to me is with me at the table.
22 Mwana wa Adamu anaenda zake kama ilivyokusudiwa. Lakini ole wake mtu huyo amsalitiye.”
For it will be done to the Son of man after the purpose of God, but unhappy is that man by whom he is given up.
23 Wakaanza kuulizana wenyewe ni nani miongoni mwao angeweza kufanya jambo hilo.
And they were wondering among themselves which of them it was who would do this thing.
24 Pia yakazuka mabishano katikati ya wanafunzi kwamba ni nani aliyeonekana kuwa mkuu kuliko wote miongoni mwao.
And there was an argument among them about which of them was the greatest.
25 Yesu akawaambia, “Wafalme na watu wa Mataifa huwatawala watu kwa nguvu. Nao wenye mamlaka juu yao hujiita ‘Wafadhili.’
And he said, The kings of the Gentiles are lords over them, and those who have authority are given names of honour.
26 Lakini ninyi msifanane nao. Bali yeye aliye mkuu kuliko wote miongoni mwenu, inampasa kuwa kama yeye aliye mdogo wa wote, naye atawalaye na awe kama yeye ahudumuye.
But let it not be so with you; but he who is greater, let him become like the younger; and he who is chief, like a servant.
27 Kwani ni nani aliye mkuu? Ni yule aketiye mezani au ni yule ahudumuye? Si ni yule aliyekaa mezani? Lakini mimi niko miongoni mwenu kama yule ahudumuye.
For which is greater, the guest who is seated at a meal or the servant who is waiting on him? is it not the guest? but I am among you as a servant.
28 Ninyi mmekuwa pamoja nami katika majaribu yangu.
But you are those who have kept with me through my troubles;
29 Nami kama Baba yangu alivyonipa ufalme, kadhalika mimi nami ninawapa ninyi,
And I will give you a kingdom as my Father has given one to me,
30 ili mpate kula na kunywa mezani pangu katika karamu ya ufalme wangu, na kukaa katika viti vya enzi, mkihukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.”
So that you may take food and drink at my table in my kingdom, and be seated like kings, judging the twelve tribes of Israel.
31 Yesu akasema, “Simoni, Simoni, sikiliza, Shetani ameomba kuwapepeta ninyi wote kama ngano.
Simon, Simon, Satan has made a request to have you, so that he may put you to the test as grain is tested:
32 Lakini nimekuombea wewe Simoni ili imani yako isishindwe, nawe ukiisha kunirudia, uwaimarishe ndugu zako.”
But I have made prayer for you, that your faith may not go from you: and when you are turned again, make your brothers strong.
33 Petro akajibu, “Bwana, niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani na hata kifoni.”
And he said to him, Lord, I am ready to go with you to prison and to death.
34 Yesu akamjibu, “Ninakuambia Petro, kabla jogoo hajawika usiku wa leo, utakana mara tatu kwamba hunijui mimi.”
And he said, I say to you, Peter, before the cock's second cry today, you will say three times that you have no knowledge of me.
35 Kisha Yesu akawauliza, “Nilipowatuma bila mfuko, wala mkoba, wala viatu, mlipungukiwa na kitu chochote?” Wakajibu, “La, hatukupungukiwa na kitu chochote.”
And he said to them, When I sent you out without money or bag or shoes, were you in need of anything? And they said, Nothing.
36 Akawaambia, “Lakini sasa, aliye na mfuko na auchukue, na aliye na mkoba vivyo hivyo. Naye asiye na upanga, auze joho lake anunue mmoja.
And he said to them, But now, he who has a money-bag, or a bag for food, let him take it: and he who has not, let him give his coat for money and get a sword.
37 Kwa sababu, nawaambia, andiko hili lazima litimizwe juu yangu, kwamba, ‘Alihesabiwa pamoja na wakosaji’; kwa kweli yaliyoandikwa kunihusu mimi hayana budi kutimizwa.”
For I say to you that these words will be put into effect in me, And he was numbered among the evil-doers: for what has been said in the Writings about me has an end.
38 Wanafunzi wake wakamwambia, “Bwana, tazama hapa kuna panga mbili.” Akawajibu, “Inatosha.”
And they said, Lord, here are two swords. And he said, It is enough.
39 Yesu akatoka, akaenda kwenye Mlima wa Mizeituni kama ilivyokuwa kawaida yake, nao wanafunzi wake wakamfuata.
And he came out, and went, as his way was, to the Mountain of Olives, and the disciples went with him.
40 Walipofika huko, akawaambia wanafunzi wake, “Ombeni, msije mkaingia majaribuni.”
And when he came to the place, he said to them, Make a prayer that you may not be put to the test.
41 Akajitenga nao kama umbali wa kutupa jiwe, akapiga magoti, akaomba
And he went a little distance away from them and, falling on his knees in prayer, he said,
42 akisema, “Baba, kama ni mapenzi yako, niondolee kikombe hiki. Lakini si kama nipendavyo, bali mapenzi yako yatendeke.”
Father, if it is your pleasure, take this cup from me: but still, let your pleasure, not mine, be done.
43 Malaika kutoka mbinguni akamtokea, akamtia nguvu.
And an angel from heaven came to him, to give him strength.
44 Naye akiwa katika maumivu makuu, akaomba kwa bidii, nalo jasho lake likawa kama matone ya damu yakidondoka ardhini.
And being in great trouble of soul, the force of his prayer became stronger, and great drops, like blood, came from him, falling to the earth.
45 Baada ya kuomba, akawarudia wanafunzi wake akawakuta wamelala, wakiwa wamechoka kutokana na huzuni.
And, getting up from prayer, he came to the disciples, and saw that they were sleeping for sorrow.
46 Naye akawauliza, “Mbona mmelala? Amkeni, mwombe ili msije mkaingia majaribuni.”
And he said, Why are you sleeping? Get up, and give yourselves to prayer, so that you may not be put to the test.
47 Yesu alipokuwa bado anazungumza, umati mkubwa wa watu ukaja. Uliongozwa na Yuda, ambaye alikuwa mmoja wa wale wanafunzi Kumi na Wawili. Akamkaribia Yesu ili ambusu.
And while he was saying these words, there came a band of people, and Judas, one of the twelve, was in front of them, and he came near to Jesus to give him a kiss.
48 Lakini Yesu akamwambia, “Yuda, je, unamsaliti Mwana wa Adamu kwa busu?”
But Jesus said to him, Judas, will you be false to the Son of man with a kiss?
49 Wafuasi wa Yesu walipoona yale yaliyokuwa yanakaribia kutokea, wakasema, “Bwana, tuwakatekate kwa panga zetu?”
And when those who were with him saw what was coming, they said, Lord, may we not make use of our swords?
50 Mmoja wao akampiga mtumishi wa kuhani mkuu kwa upanga, akamkata sikio la kuume.
And one of them gave a blow to the servant of the high priest, cutting off his right ear.
51 Lakini Yesu akasema, “Acheni!” Akaligusa lile sikio la yule mtu na kumponya.
But Jesus, answering, said, Put up with this, at least. And touching his ear, he made it well.
52 Kisha Yesu akawaambia wale viongozi wa makuhani, maafisa wa walinzi wa Hekalu, pamoja na wazee waliokuwa wamekuja kumkamata, “Mmekuja na panga na marungu, kana kwamba mimi ni mnyangʼanyi?
And Jesus said to the chief priests and the captains of the Temple and the rulers, who had come against him, Have you come out as against a thief, with swords and sticks?
53 Siku kwa siku nilikuwa pamoja nanyi Hekaluni lakini hamkunikamata. Lakini hii ni saa yenu, wakati giza linatawala!”
When I was in the Temple with you every day, your hands were not stretched out against me: but this is your hour, and the authority of the dark power.
54 Kisha wakamkamata Yesu, wakamchukua, wakaenda naye mpaka nyumbani kwa kuhani mkuu. Lakini Petro akafuata kwa mbali.
And they made him a prisoner and took him away to the house of the high priest. But Peter went after them at a distance.
55 Walipokwisha kuwasha moto katikati ya ua na kuketi pamoja, Petro naye akaketi pamoja nao.
And a fire was lighted in the middle of the open square, and they were seated together, and Peter was among them.
56 Mtumishi mmoja wa kike akamwona kwa mwanga wa moto akiwa ameketi pale. Akamtazama sana, akasema, “Huyu mtu pia alikuwa pamoja na Yesu!”
And a certain woman-servant, seeing him in the light of the fire, and looking at him with attention, said, This man was with him.
57 Lakini Petro akakana, akasema, “Ewe mwanamke, hata simjui!”
But he said, Woman, it is not true; I have no knowledge of him.
58 Baadaye kidogo, mtu mwingine alimwona Petro akasema, “Wewe pia ni mmoja wao!” Petro akajibu, “Wewe mtu, mimi sio mmoja wao!”
And after a little time, another saw him and said, You are one of them; and he said, Man, I am not.
59 Baada ya muda wa kama saa moja hivi, mtu mwingine akazidi kusisitiza, “Kwa hakika huyu mtu naye alikuwa pamoja na Yesu, kwa maana yeye pia ni Mgalilaya.”
And after about an hour, another man said, with decision, Certainly this man was with him, for he is a Galilaean.
60 Petro akajibu, “Wewe mtu, mimi sijui unalosema!” Wakati huo huo, akiwa bado anazungumza, jogoo akawika.
And Peter said, Man, I have no knowledge of these things of which you are talking. And straight away, while he was saying these words, there came the cry of a cock.
61 Naye Bwana akageuka, akamtazama Petro. Ndipo Petro akakumbuka lile neno ambalo Bwana alimwambia: “Kabla jogoo hajawika leo, utanikana mara tatu.”
And the Lord, turning, gave Peter a look. And the words of the Lord came to Peter's mind, how he had said, This night, before the hour of the cock's cry, you will be false to me three times.
62 Naye akaenda nje, akalia kwa majonzi.
And he went out, weeping bitterly.
63 Watu waliokuwa wanamlinda Yesu wakaanza kumdhihaki na kumpiga.
And the men in whose hands Jesus was, made sport of him and gave him blows.
64 Wakamfunga kitambaa machoni na kumuuliza, “Tabiri! Tuambie ni nani aliyekupiga?”
And, covering his eyes, they said to him, Are you prophet enough to say who gave you that blow?
65 Wakaendelea kumtukana kwa matusi mengi.
And they said a number of other evil things against him.
66 Kulipopambazuka, baraza la wazee wa watu, yaani viongozi wa makuhani na walimu wa sheria, wakakutana pamoja, naye Yesu akaletwa mbele yao.
And when it was day, the rulers of the people came together, with the chief priests and the scribes, and they took him before their Sanhedrin, saying,
67 Wakamwambia, “Kama wewe ndiye Kristo, tuambie.” Yesu akawajibu, “Hata nikiwaambia hamtaamini.
If you are the Christ, say so. But he said, If I say so you will not have belief;
68 Nami nikiwauliza swali, hamtanijibu.
And if I put a question to you, you will not give an answer.
69 Lakini kuanzia sasa, Mwana wa Adamu ataketi mkono wa kuume wa Mungu Mwenye Nguvu.”
But in the future the Son of man will be seated at the right hand of the power of God.
70 Wote wakauliza, “Wewe basi ndiwe Mwana wa Mungu?” Yeye akawajibu, “Ninyi mwasema kwamba mimi ndiye.”
And they all said, Are you then the Son of God? and he said, You say that I am.
71 Kisha wakasema, “Tuna haja gani tena ya ushahidi zaidi? Tumesikia wenyewe kutoka kinywani mwake.”
And they said, What more need have we of witness? we have the very words of his mouth.

< Luka 22 >