< Luka 21 >

1 Yesu alipoinua macho yake, aliwaona matajiri wakiweka sadaka zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu.
And looking up, he saw the men of wealth putting their offerings in the money-box.
2 Akamwona pia mjane mmoja maskini akiweka humo sarafu mbili ndogo za shaba.
And he saw a certain poor widow putting in a farthing.
3 Yesu akasema, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka humo zaidi ya watu wengine wote.
And he said, Truly I say to you, This poor widow has given more than all of them:
4 Hawa watu wengine wote wametoa sadaka kutokana na wingi wa mali zao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake vyote alivyokuwa navyo, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
For they gave out of their wealth, having more than enough for themselves: but she, even out of her need, has put in all her living.
5 Baadhi ya wanafunzi wake wakawa wanamwonyesha jinsi Hekalu lilivyopambwa kwa mawe mazuri na kwa vitu vilivyotolewa kuwa sadaka kwa Mungu. Lakini Yesu akawaambia,
And some were talking about the Temple, how it was made fair with beautiful stones and with offerings, but he said,
6 “Kuhusu haya mnayoyaona hapa, wakati utafika ambapo hakuna jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali kila moja litabomolewa.”
As for these things which you see, the days will come when not one stone will be resting on another, but all will be broken down.
7 Wakamuuliza, “Mwalimu, mambo haya yatatukia lini? Ni dalili gani itaonyesha kwamba yanakaribia kutendeka?”
And they said to him, Master, when will these things be? and what sign will there be when these events are to take place?
8 Yesu akawajibu, “Jihadharini msije mkadanganywa. Maana wengi watakuja kwa Jina langu, wakidai, ‘Mimi ndiye,’ na, ‘Wakati umekaribia.’ Msiwafuate.
And he said, Take care that you are not tricked: for a number of people will come in my name, saying, I am he; and, The time is near: do not go after them.
9 Lakini msikiapo habari za vita na machafuko, msiogope. Kwa maana hayo ni lazima yatokee kwanza, ila ule mwisho hautakuja wakati huo.”
And when news of wars and troubled times comes to your ears, have no fear; for these things have to be, but the end will not be now.
10 Kisha akawaambia: “Taifa litainuka dhidi ya taifa jingine, na ufalme mmoja dhidi ya ufalme mwingine.
Then he said to them, Nation will be moved against nation and kingdom against kingdom:
11 Kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, na njaa kali, na magonjwa ya kuambukiza katika sehemu mbalimbali. Pia kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni.
There will be great earth-shocks and outbursts of disease in a number of places, and men will be without food; and there will be wonders and great signs from heaven.
12 “Lakini kabla yote hayajatokea, watawakamata ninyi na kuwatesa. Watawatia mikononi mwa wakuu wa masinagogi na kuwafunga magerezani. Nanyi mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya Jina langu.
But before all this, they will take you and be very cruel to you, giving you up to the Synagogues and to prisons, taking you before kings and rulers, because of my name.
13 Hii itawapa nafasi ya kushuhudia.
And it will be turned to a witness for you.
14 Lakini kusudieni mioyoni mwenu msisumbuke awali kuhusu mtakalosema mbele ya mashtaka.
So take care not to be troubled before the time comes, about what answers you will give:
15 Kwa maana nitawapa maneno na hekima ambayo hakuna hata adui yenu mmoja atakayeweza kushindana nayo wala kuipinga.
For I will give you words and wisdom, so that not one of those who are against you will be able to get the better of you, or to put you in the wrong.
16 Mtasalitiwa hata na wazazi, ndugu, jamaa na marafiki, na baadhi yenu watawaua.
But you will be given up even by your fathers and mothers, your brothers and relations and friends; and some of you will be put to death.
17 Mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya Jina langu.
And you will be hated by all men, because of me.
18 Lakini hapatakuwa na unywele mmoja wa kichwa chenu utakaoangamia.
But not a hair of your head will come to destruction.
19 Kwa kuvumilia mtaokoa roho zenu.
By going through all these things, you will keep your lives.
20 “Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, basi fahamuni kwamba kuharibiwa kwake kumekaribia.
But when you see armies all round about Jerusalem, then be certain that her destruction is near.
21 Wakati huo, wale walio Uyahudi wakimbilie milimani, walio mjini Yerusalemu watoke humo, nao wale walioko mashambani wasiingie mjini.
Then let those who are in Judaea go in flight to the mountains; and those who are in the middle of the town go out; and let not those who are in the country come in.
22 Kwa sababu huu utakuwa ni wakati wa adhabu ili kutimiza yote yaliyoandikwa.
For these are the days of punishment, in which all the things in the Writings will be put into effect.
23 Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! Kutakuwa na dhiki kuu katika nchi na ghadhabu juu ya hawa watu.
It will be hard for women who are with child, and for her with a baby at the breast, in those days. For great trouble will come on the land, and wrath on this people.
24 Wataanguka kwa makali ya upanga, na wengine watachukuliwa kuwa mateka katika mataifa yote. Nao mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa Mataifa hadi muda wa hao watu wa Mataifa utimie.
And they will be put to death with the sword, and will be taken as prisoners into all the nations; and Jerusalem will be crushed under the feet of the Gentiles, till the times of the Gentiles are complete.
25 “Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Hapa duniani, mataifa yatakuwa katika dhiki na fadhaa kutokana na ngurumo na misukosuko ya bahari.
And there will be signs in the sun and moon and stars; and on the earth, fear among the nations and doubt because of the loud noise of the sea and the waves;
26 Watu watazimia roho kutokana na hofu kuu na kuyaona yale mambo yanayotokea duniani, kwa maana nguvu za angani zitatikisika.
Men's strength will go from them in fear and in waiting for the things which are coming on the earth; for the powers of the heavens will be moved.
27 Wakati huo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni pamoja na uweza na utukufu mkuu.
And then they will see the Son of man coming in a cloud, with power and great glory.
28 Mambo haya yatakapoanza kutendeka, simameni na mkaviinue vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umekaribia.”
But when these things come about, let your heads be lifted up, because your salvation is near.
29 Akawaambia mfano huu: “Uangalieni mtini na miti mingine yote.
And he made a story for them: See the fig-tree, and all the trees;
30 Inapochipua majani, ninyi wenyewe mnaweza kuona na kutambua wenyewe ya kuwa wakati wa kiangazi umekaribia.
When they put out their young leaves, you take note of it, and it is clear to you that summer is coming.
31 Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
In the same way, when you see these things taking place you may be certain that the kingdom of God is near.
32 “Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
Truly I say to you, This generation will not come to an end till all things are complete.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”
Heaven and earth will come to an end, but my words will not come to an end.
34 “Jihadharini mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na fadhaa za maisha haya, nayo siku ile ikawakuta ninyi bila kutazamia kama vile mtego unasavyo.
But give attention to yourselves, for fear that your hearts become over-full of the pleasures of food and wine, and the cares of this life, and that day may come on you suddenly, and take you as in a net:
35 Kwa maana kama vile mtego unasavyo, ndivyo siku hiyo itakavyowapata wanadamu wote waishio katika uso wa dunia yote.
For so it will come on all those who are living on the face of all the earth.
36 Kesheni daima na mwombe ili mweze kuokoka na yale yote yatakayotokea na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.”
But keep watch at all times with prayer, that you may be strong enough to come through all these things and take your place before the Son of man.
37 Kila siku Yesu alikuwa akifundisha Hekaluni, na jioni ilipofika, alikwenda zake kwenye Mlima wa Mizeituni na kukaa huko usiku kucha.
And every day he was teaching in the Temple and every night he went out to the mountain which is named the Mountain of Olives to take his rest.
38 Nao watu wote walikuja asubuhi na mapema Hekaluni ili kumsikiliza.
And all the people came early in the morning to give ear to his words in the Temple.

< Luka 21 >