< Luka 21 >

1 Yesu alipoinua macho yake, aliwaona matajiri wakiweka sadaka zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu.
Looking up He saw the people throwing their gifts into the Treasury--the rich people.
2 Akamwona pia mjane mmoja maskini akiweka humo sarafu mbili ndogo za shaba.
He also saw a poor widow dropping in two farthings,
3 Yesu akasema, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka humo zaidi ya watu wengine wote.
and He said, "In truth I tell you that this widow, so poor, has thrown in more than any of them.
4 Hawa watu wengine wote wametoa sadaka kutokana na wingi wa mali zao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake vyote alivyokuwa navyo, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
For from what they could well spare they have all of them contributed to the offerings, but she in her need has thrown in all she had to live on."
5 Baadhi ya wanafunzi wake wakawa wanamwonyesha jinsi Hekalu lilivyopambwa kwa mawe mazuri na kwa vitu vilivyotolewa kuwa sadaka kwa Mungu. Lakini Yesu akawaambia,
When some were remarking about the Temple, how it was embellished with beautiful stones and dedicated gifts, He said,
6 “Kuhusu haya mnayoyaona hapa, wakati utafika ambapo hakuna jiwe moja litakalobaki juu ya jingine, bali kila moja litabomolewa.”
"As to these things which you now admire, the time is coming when there will not be one stone left here upon another which will not be pulled down."
7 Wakamuuliza, “Mwalimu, mambo haya yatatukia lini? Ni dalili gani itaonyesha kwamba yanakaribia kutendeka?”
"Rabbi, when will this be?" they asked Him, "and what will be the token given when these things are about to take place?"
8 Yesu akawajibu, “Jihadharini msije mkadanganywa. Maana wengi watakuja kwa Jina langu, wakidai, ‘Mimi ndiye,’ na, ‘Wakati umekaribia.’ Msiwafuate.
"See to it," He replied, "that you are not misled; for many will come assuming my name and professing, 'I am He,' or saying, 'The time is close at hand.' Do not go and follow them.
9 Lakini msikiapo habari za vita na machafuko, msiogope. Kwa maana hayo ni lazima yatokee kwanza, ila ule mwisho hautakuja wakati huo.”
But when you hear of wars and turmoils, be not afraid; for these things must happen first, but the end does not come immediately."
10 Kisha akawaambia: “Taifa litainuka dhidi ya taifa jingine, na ufalme mmoja dhidi ya ufalme mwingine.
Then He said to them, "Nation will rise in arms against nation, and kingdom against kingdom.
11 Kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, na njaa kali, na magonjwa ya kuambukiza katika sehemu mbalimbali. Pia kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni.
And there will be great earthquakes, and in places famines and pestilence; and there will be terrible sights and wonderful tokens from Heaven.
12 “Lakini kabla yote hayajatokea, watawakamata ninyi na kuwatesa. Watawatia mikononi mwa wakuu wa masinagogi na kuwafunga magerezani. Nanyi mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya Jina langu.
"But before all these things happen they will lay hands on you and persecute you. They will deliver you up to synagogues and to prison, and you will be brought before kings and governors for my sake.
13 Hii itawapa nafasi ya kushuhudia.
In the end all this will be evidence of your fidelity.
14 Lakini kusudieni mioyoni mwenu msisumbuke awali kuhusu mtakalosema mbele ya mashtaka.
"Make up your minds, however, not to prepare a defence beforehand,
15 Kwa maana nitawapa maneno na hekima ambayo hakuna hata adui yenu mmoja atakayeweza kushindana nayo wala kuipinga.
for I will give you utterance and wisdom which none of your opponents will be able to withstand or reply to.
16 Mtasalitiwa hata na wazazi, ndugu, jamaa na marafiki, na baadhi yenu watawaua.
You will be betrayed even by parents, brothers, relatives, friends; and some of you they will put to death.
17 Mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya Jina langu.
You will be the objects of universal hatred because you are called by my name;
18 Lakini hapatakuwa na unywele mmoja wa kichwa chenu utakaoangamia.
and yet not a hair of your heads shall perish.
19 Kwa kuvumilia mtaokoa roho zenu.
By your patient endurance you will purchase your lives.
20 “Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, basi fahamuni kwamba kuharibiwa kwake kumekaribia.
"But when you see Jerusalem with armies encamping round her on every side, then be certain that her overthrow is close at hand.
21 Wakati huo, wale walio Uyahudi wakimbilie milimani, walio mjini Yerusalemu watoke humo, nao wale walioko mashambani wasiingie mjini.
Then let those who shall be in Judaea escape to the hills; let those who are in the city leave it, and those who are in the country not enter in.
22 Kwa sababu huu utakuwa ni wakati wa adhabu ili kutimiza yote yaliyoandikwa.
For those are the days of vengeance and of fulfilling all that is written.
23 Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! Kutakuwa na dhiki kuu katika nchi na ghadhabu juu ya hawa watu.
"Alas for the women who at that time are with child or who have infants; for there will be great distress in the land, and anger towards this People.
24 Wataanguka kwa makali ya upanga, na wengine watachukuliwa kuwa mateka katika mataifa yote. Nao mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa Mataifa hadi muda wa hao watu wa Mataifa utimie.
They will fall by the sword, or be carried off into slavery among all the Gentiles. And Jerusalem will be trampled under foot by the Gentiles, till the appointed times of the Gentiles have expired.
25 “Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Hapa duniani, mataifa yatakuwa katika dhiki na fadhaa kutokana na ngurumo na misukosuko ya bahari.
"There will be signs in sun, moon, and stars; and on earth anguish among the nations in their bewilderment at the roaring of the sea and its billows;
26 Watu watazimia roho kutokana na hofu kuu na kuyaona yale mambo yanayotokea duniani, kwa maana nguvu za angani zitatikisika.
while men's hearts are fainting for fear, and for anxious expectation of what is coming on the world. For the forces which control the heavens will be disordered and disturbed.
27 Wakati huo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni pamoja na uweza na utukufu mkuu.
And then will they see the Son of Man coming in a cloud with great power and glory.
28 Mambo haya yatakapoanza kutendeka, simameni na mkaviinue vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umekaribia.”
But when all this is beginning to take place, grieve no longer. Lift up your heads, because your deliverance is drawing near."
29 Akawaambia mfano huu: “Uangalieni mtini na miti mingine yote.
And He spoke a parable to them. "See," He said, "the fig-tree and all the trees.
30 Inapochipua majani, ninyi wenyewe mnaweza kuona na kutambua wenyewe ya kuwa wakati wa kiangazi umekaribia.
As soon as they have shot out their leaves, you know at a glance that summer is now near.
31 Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yakitukia, mnatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
So also, when you see these things happening, you may be sure that the Kingdom of God is near.
32 “Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
I tell you in solemn truth that the present generation will certainly not pass away without all these things having first taken place.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.”
Earth and sky will pass away, but it is certain that my words will not pass away.
34 “Jihadharini mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na fadhaa za maisha haya, nayo siku ile ikawakuta ninyi bila kutazamia kama vile mtego unasavyo.
"But take heed to yourselves, lest your souls be weighed down with self-indulgence and drunkenness or the anxieties of this life, and that day come upon you, suddenly, like a falling trap;
35 Kwa maana kama vile mtego unasavyo, ndivyo siku hiyo itakavyowapata wanadamu wote waishio katika uso wa dunia yote.
for it will come on all dwellers on the face of the whole earth.
36 Kesheni daima na mwombe ili mweze kuokoka na yale yote yatakayotokea na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.”
But beware of slumbering; and every moment pray that you may be fully strengthened to escape from all these coming evils, and to take your stand in the presence of the Son of Man."
37 Kila siku Yesu alikuwa akifundisha Hekaluni, na jioni ilipofika, alikwenda zake kwenye Mlima wa Mizeituni na kukaa huko usiku kucha.
His habit at this time was to teach in the Temple by day, but to go out and spend the night on the Mount called the Oliveyard.
38 Nao watu wote walikuja asubuhi na mapema Hekaluni ili kumsikiliza.
And all the people came to Him in the Temple, early in the morning, to listen to Him.

< Luka 21 >