< Luka 20 >

1 Siku moja, Yesu alipokuwa akifundisha watu Hekaluni na kuhubiri habari njema, viongozi wa makuhani, walimu wa sheria, pamoja na wazee wa watu wakamjia.
On one of those days while He was teaching the people in the Temple and proclaiming the Good News, the High Priests came upon Him, and the Scribes,
2 Wakamuuliza, “Tuambie, unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Ni nani aliyekupa mamlaka haya?”
together with the Elders, and they asked Him, "Tell us, By what authority are you doing these things? And who is it that gave you this authority?"
3 Akawajibu, “Nami nitawauliza swali.
"I also will put a question to you, "He said;
4 Je, ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?”
"was John's baptism of Heavenly or of human origin?"
5 Wakahojiana wao kwa wao wakisema, “Kama tukisema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atatuuliza, ‘Mbona hamkumwamini?’
So they debated the matter with one another. "If we say 'Heavenly,'" they argued, "he will say, 'Why did you not believe him?'
6 Lakini tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’ watu wote watatupiga mawe, kwa sababu wanaamini kwamba Yohana alikuwa nabii.”
And if we say, 'human,' the people will all stone us; for they are thoroughly convinced that John was a Prophet."
7 Basi wakajibu, “Hatujui ulikotoka.”
And they answered that they did not know the origin of it.
8 Yesu akawaambia, “Wala mimi sitawaambia ni kwa mamlaka gani ninatenda mambo haya.”
"Nor will I tell you," said Jesus, "by what authority I do these things."
9 Akaendelea kuwaambia watu mfano huu: “Mtu mmoja alipanda shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima fulani, kisha akasafiri kwa muda mrefu.
Then He proceeded to speak a parable to the people. "There was a man," He said, "who planted a vineyard, let it out to vine-dressers, and went abroad for a considerable time.
10 Wakati wa mavuno ulipofika, akamtuma mtumishi wake kwa hao wapangaji ili wampe sehemu ya mavuno ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga, wakamfukuza mikono mitupu.
At vintage-time he sent a servant to the vine-dressers, for them to give him a share of the crop; but the vine-dressers beat him cruelly and sent him away empty-handed.
11 Akamtuma mtumishi mwingine, huyo naye wakampiga, wakamfanyia mambo ya aibu na kumfukuza.
Then he sent a second servant; and him too they beat and ill treated and sent away empty-handed.
12 Bado akamtuma na mwingine wa tatu, huyu pia wakamjeruhi na kumtupa nje ya shamba.
Then again he sent a third; and this one also they wounded and drove away.
13 “Basi yule mwenye shamba la mizabibu akasema, ‘Nifanye nini? Nitamtuma mwanangu mpendwa, huenda yeye watamheshimu.’
Then the owner of the vineyard said, "'What am I to do? I will send my son--my dearly-loved son: they will probably respect him.'
14 “Lakini wale wapangaji walipomwona, wakasemezana wao kwa wao. Wakasema, ‘Huyu ndiye mrithi. Basi na tumuue ili urithi uwe wetu.’
"But when the vine-dressers saw him, they discussed the matter with one another, and said, "'This is the heir: let us kill him, that the inheritance may be ours.'
15 Kwa hiyo wakamtupa nje ya shamba la mizabibu, wakamuua.” “Sasa basi yule mwenye shamba la mizabibu atawafanyia nini wapangaji hawa?
"So they turned him out of the vineyard and murdered him. What then will the owner of the vineyard do to them?
16 Atakuja na kuwaua hao wapangaji, na kuwapa wapangaji wengine hilo shamba la mizabibu.” Watu waliposikia hayo wakasema, “Mungu apishie mbali jambo hili lisitokee!”
He will come and put these vine-dressers to death, and give the vineyard to others." "God forbid!" exclaimed the hearers.
17 Lakini Yesu akawakazia macho, akasema, “Basi ni nini maana ya yale yaliyoandikwa: “‘Jiwe walilolikataa waashi, limekuwa jiwe kuu la pembeni’?
He looked at them and said, "What then does that mean which is written, "'The Stone which the builders rejected has been made the cornerstone'?
18 Kila mtu aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika vipande vipande, lakini yule litakayemwangukia atasagwa kabisa.”
Every one who falls on that stone will be severely hurt, but on whomsoever it falls, he will be utterly crushed."
19 Walimu wa sheria na viongozi wa makuhani wakatafuta njia ya kumkamata mara moja, kwa sababu walifahamu kwamba amesema mfano huo kwa ajili yao. Lakini waliwaogopa watu.
At this the Scribes and the High Priests wanted to lay hands on Him, then and there; only they were afraid of the people. For they saw that in this parable He had referred to them.
20 Kwa hiyo wakawa wanamchunguza na kutuma wapelelezi waliojifanya kuwa wenye haki ili wapate kumtega kwa maneno asemayo, ili wamtie katika uwezo na mamlaka ya mtawala.
So, after impatiently watching their opportunity, they sent spies who were to act the part of good and honest men, that they might fasten on some expression of His, so as to hand Him over to the ruling power and the Governor's authority.
21 Hivyo wale wapelelezi wakamuuliza, “Mwalimu, tunajua unasema na kufundisha yaliyo kweli wala humpendelei mtu, bali wafundisha njia ya Mungu katika kweli.
So they put a question to Him. "Rabbi," they said, "we know that you say and teach what is right and that you make no distinctions between one man and another, but teach God's way truly.
22 Je, ni halali sisi kulipa kodi kwa Kaisari, au la?”
Is it allowable to pay a tax to Caesar, or not?"
23 Lakini Yesu akatambua hila yao, kwa hiyo akawaambia,
But He saw through their knavery and replied,
24 “Nionyesheni dinari. Je, sura hii na maandishi haya yaliyoko juu yake ni vya nani?”
"Show me a shilling; whose likeness and inscription does it bear?" "Caesar's," they said.
25 Wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Akawaambia, “Basi mpeni Kaisari kilicho cha Kaisari, naye Mungu mpeni kilicho cha Mungu.”
"Pay therefore," He replied, "what is Caesar's to Caesar--and what is God's to God."
26 Wakashindwa kumkamata kwa yale aliyokuwa amesema hadharani. Nao wakashangazwa mno na majibu yake, wakanyamaza kimya.
There was nothing here that they could lay hold of before the people, and marvelling at His answer they said no more.
27 Baadhi ya Masadukayo, wale wasemao kwamba hakuna ufufuo wa wafu, wakamjia Yesu na kumuuliza,
Next some of the Sadducees came forward (who deny that there is a Resurrection), and they asked Him,
28 “Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu wa mtu akifa na kumwacha mkewe bila mtoto, basi huyo mtu inampasa amwoe huyo mjane ili amzalie ndugu yake watoto.
"Rabbi, Moses made it a law for us that if a man's brother should die, leaving a wife but no children, the man shall marry the widow and raise up a family for his brother.
29 Basi palikuwepo ndugu saba. Yule wa kwanza akaoa, akafa bila kuzaa mtoto.
Now there were seven brothers. The first of them took a wife and died childless.
30 Kisha yule wa pili akamwoa huyo mjane, naye akafa bila mtoto,
The second and the third also took her;
31 naye wa tatu pia akamwoa. Vivyo hivyo ndugu wote saba wakawa wamemwoa huyo mwanamke, na wote wakafa pasipo yeyote kupata mtoto.
and all seven, having done the same, left no children when they died.
32 Mwishowe, yule mwanamke naye akafa.
Finally the woman also died.
33 Sasa basi, siku ya ufufuo huyo mwanamke atakuwa mke wa nani, maana aliolewa na ndugu wote saba?”
The woman, then--at the Resurrection--whose wife shall she be? for they all seven married her."
34 Yesu akawajibu, “Katika maisha haya watu huoa na kuolewa. (aiōn g165)
"The men of this age," replied Jesus, "marry, and the women are given in marriage. (aiōn g165)
35 Lakini wale ambao wamehesabiwa kwamba wanastahili kupata nafasi katika ulimwengu ule na katika ufufuo wa wafu, hawaoi wala hawaolewi. (aiōn g165)
But as for those who shall have been deemed worthy to find a place in that other age and in the Resurrection from among the dead, the men do not marry and the women are not given in marriage. (aiōn g165)
36 Hawa hawawezi kufa tena, kwa maana wao ni kama malaika. Wao ni watoto wa Mungu, kwa sababu ni watoto wa ufufuo.
For indeed they cannot die again; they are like angels, and are sons of God through being sons of the Resurrection.
37 Hata Mose alidhihirisha kuwa wafu wanafufuka, kwa habari ya kile kichaka kilichokuwa kikiwaka moto bila kuteketea, alipomwita Bwana, ‘Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo.’
But that the dead rise to life even Moses clearly implies in the passage about the Bush, where he calls the Lord 'The God of Abraham, the God of Isaac, and the God of Jacob.'
38 Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai, kwa kuwa kwake wote ni hai.”
He is not a God of dead, but of living men, for to Him are all living."
39 Baadhi ya walimu wa sheria wakasema, “Mwalimu, umesema sawasawa kabisa!”
Then some of the Scribes replied, "Rabbi, you have spoken well."
40 Baada ya hayo hakuna mtu aliyethubutu kumuuliza maswali tena.
From that time, however, no one ventured to challenge Him with a single question.
41 Kisha Yesu akawaambia, “Imekuwaje basi wao husema Kristoni Mwana wa Daudi?
But He asked them, "How is it they say that the Christ is a son of David?
42 Daudi mwenyewe anasema katika Kitabu cha Zaburi: “‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume,
Why, David himself says in the Book of Psalms, "'The Lord said to my Lord, Sit at My right hand
43 hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
Until I have made thy foes a footstool under they feet.'
44 Ikiwa Daudi anamwita yeye ‘Bwana,’ basi atakuwaje mwanawe?”
"David himself therefore calls Him Lord, and how can He be his son?"
45 Wakati watu wote walikuwa wanamsikiliza, Yesu akawaambia wanafunzi wake,
Then, in the hearing of all the people, He said to the disciples,
46 “Jihadharini na walimu wa sheria. Wao hupenda kutembea wakiwa wamevaa mavazi marefu, na kusalimiwa kwa heshima masokoni. Hupenda kukaa kwenye viti vya mbele katika masinagogi, na kukaa kwenye nafasi za heshima katika karamu.
"Beware of the Scribes, who like to walk about in long robes, and love to be bowed to in places of public resort and to occupy the best seats in the synagogues or at a dinner party;
47 Wao hula nyumba za wajane, na ili waonekane kuwa wema, wanasali sala ndefu. Watu kama hawa watapata hukumu iliyo kuu sana.”
who swallow up the property of widows and mask their wickedness by making long prayers. They will be punished far more severely than others."

< Luka 20 >