< Yohana 1 >

1 Hapo mwanzo alikuwako Neno, huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.
Au commencement était le Verbe, et le Verbe était en Dieu, et le Verbe était Dieu.
2 Tangu mwanzo huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu.
Il était au commencement en Dieu.
3 Vitu vyote viliumbwa kwa yeye, wala pasipo yeye hakuna chochote kilichoumbwa ambacho kimeumbwa.
Tout par lui a été fait, et sans lui n'a été fait rien de ce qui existe.
4 Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima na huo uzima ulikuwa nuru ya watu.
En lui était la vie, et la vie était la lumière des hommes,
5 Nuru hungʼaa gizani nalo giza halikuishinda.
Et la lumière luit dans les ténèbres, et les ténèbres ne l'ont point reçue.
6 Alikuja mtu mmoja aliyetumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana.
Il y eut un homme, envoyé de Dieu; son nom était Jean.
7 Alikuja kama shahidi apate kuishuhudia hiyo nuru, ili kwa kupitia kwake watu wote waweze kuamini.
Celui-ci vint en témoignage, pour rendre témoignage à la lumière, afin que tous crussent par lui:
8 Yeye mwenyewe hakuwa ile nuru, bali alikuja kuishuhudia hiyo nuru.
non que celui-ci fût la lumière, mais il avait à rendre témoignage à la lumière.
9 Kwamba nuru halisi, imwangaziayo kila mtu ilikuwa inakuja ulimwenguni.
La lumière, la vraie, celle qui éclaire tout homme, venait dans le monde.
10 Huyo Neno alikuwako ulimwenguni na ingawa ulimwengu uliumbwa kupitia kwake, haukumtambua.
Il (le Verbe) était dans le monde, et le monde par lui a été fait, et le monde ne l'a pas connu.
11 Alikuja kwa walio wake, lakini wao hawakumpokea.
Il vint chez lui, et les siens ne l'ont pas reçu.
12 Bali wote waliompokea, aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake.
Mais quant à tous ceux qui l'ont reçu, Il leur a donné le pouvoir de devenir enfants de Dieu, à ceux qui croient en son nom,
13 Hawa ndio wasiozaliwa kwa damu, wala kwa mapenzi ya mwili au kwa mapenzi ya mtu, bali kwa mapenzi ya Mungu.
Qui non du sang, ni de la volonté de la chair, ni de la volonté de l'homme, mais de Dieu sont nés.
14 Neno alifanyika mwili, akakaa miongoni mwetu, nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba, amejaa neema na kweli.
Et le Verbe s'est fait chair, et il a habité parmi nous, (et nous avons vu sa gloire, gloire comme celle qu'un fils unique tient de son Père) tout plein de grâce et de vérité.
15 Yohana alishuhudia habari zake, akapaza sauti, akisema, “Huyu ndiye yule niliyewaambia kwamba, ‘Yeye ajaye baada yangu ni mkuu kuniliko mimi, kwa kuwa alikuwepo kabla yangu.’”
Jean lui rend témoignage, et s'écrie en ces termes: " Voici celui dont je disais: Celui qui vient après moi, est passé devant moi, parce qu'il était avant moi. "
16 Kutokana na ukamilifu wake, sisi sote tumepokea neema juu ya neema.
Et c'est de sa plénitude, que nous avons tous reçu, et grâce sur grâce;
17 Kwa kuwa sheria ilitolewa kwa mkono wa Mose, lakini neema na kweli imekuja kupitia Yesu Kristo.
parce que la loi a été donnée par Moïse, la grâce et la vérité sont venues par Jésus-Christ.
18 Hakuna mtu yeyote aliyemwona Mungu wakati wowote, ila ni Mungu Mwana pekee, aliye kifuani mwa Baba ndiye ambaye amemdhihirisha.
Dieu, personne ne le vit jamais: le Fils unique, qui est dans le sein du Père, c'est lui qui l'a fait connaître.
19 Huu ndio ushuhuda wa Yohana wakati Wayahudi walipowatuma makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu kumuuliza, “Wewe ni nani?”
Et voici le témoignage que rendit Jean, lorsque les Juifs envoyèrent de Jérusalem des prêtres et des lévites pour lui demander: " Qui êtes-vous? "
20 Yohana alikiri waziwazi pasipo kuficha akasema, “Mimi si Kristo.”
Il déclara, et ne le nia point; il déclara: " Je ne suis point le Christ. "
21 Wakamuuliza, “Wewe ni nani basi? Je, wewe ni Eliya?” Yeye akajibu, “Hapana, mimi siye.” “Je, wewe ni yule Nabii?” Akajibu, “Hapana.”
Et ils lui demandèrent: " Quoi donc! Etes-vous Elie? " Il dit: " Je ne le suis point — Etes-vous le prophète? " Il répondit: " Non. —
22 Ndipo wakasema, “Basi tuambie wewe ni nani ili tupate jibu la kuwapelekea wale waliotutuma. Wewe wasemaje juu yako mwenyewe?”
Qui êtes-vous donc, lui dirent-ils, afin que nous donnions une réponse à ceux qui nous ont envoyés. Que dites-vous de vous-même? "
23 Akawajibu kwa maneno ya nabii Isaya, akisema, “Mimi ni sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Yanyoosheni mapito ya Bwana.’”
Il répondit: " Je suis la voix de celui qui crie dans le désert: Aplanissez le chemin du Seigneur, comme l'a dit le prophète Isaïe. "
24 Basi walikuwa wametumwa watu kutoka kwa Mafarisayo
Or ceux qu'on lui avait envoyés étaient des Pharisiens.
25 wakamuuliza, “Kama wewe si Kristo, wala si Eliya na wala si yule Nabii, kwa nini basi unabatiza?”
Et ils l'interrogèrent, et lui dirent: " Pourquoi donc baptisez-vous, si vous n'êtes ni le Christ, ni Elie, ni le Prophète? "
26 Yohana akawajibu, “Mimi ninabatiza kwa maji, lakini katikati yenu yupo mtu msiyemjua.
Jean leur répondit: " Moi je baptise dans l'eau; mais au milieu de vous il y a quelqu'un que vous ne connaissez pas,
27 Yeye ajaye baada yangu, sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake.”
c'est celui qui vient après moi; je ne suis pas digne de délier la courroie de sa chaussure. "
28 Mambo haya yote yalitukia huko Bethania, ngʼambo ya Mto Yordani, mahali Yohana alipokuwa akibatiza.
Cela se passait à Béthanie, au delà du Jourdain, où Jean baptisait.
29 Siku iliyofuata, Yohana alimwona Yesu akimjia akasema, “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu!
Le lendemain, Jean vit Jésus qui venait vers lui, et il dit: " Voici l'agneau de Dieu, voici celui qui ôte le péché du monde.
30 Huyu ndiye yule niliyewaambia kwamba, ‘Mtu anakuja baada yangu ambaye ni mkuu kuniliko mimi, kwa kuwa alikuwepo kabla yangu.’
C'est de lui que j'ai dit: un homme vient après moi, qui est passé devant moi, parce qu'il était avant moi.
31 Mimi mwenyewe sikumfahamu, lakini sababu ya kuja nikibatiza kwa maji ni ili yeye apate kufunuliwa kwa Israeli.”
Et moi, je ne le connaissais pas, mais c'est afin qu'il fût manifesté à Israël, que je suis venu baptiser dans l'eau. "
32 Kisha Yohana akatoa ushuhuda huu: “Nilimwona Roho akishuka kutoka mbinguni kama hua, akakaa juu yake.
Et Jean rendit témoignage en disant: " J'ai vu l'Esprit descendre du ciel comme une colombe, et il s'est reposé sur lui.
33 Mimi nisingemtambua, lakini yeye aliyenituma nibatize kwa maji alikuwa ameniambia, ‘Yule mtu utakayemwona Roho akimshukia na kukaa juu yake, huyo ndiye atakayebatiza kwa Roho Mtakatifu.’
Et moi, je ne le connaissais pas; mais celui qui m'a envoyé baptiser dans l'eau m'a dit: Celui sur qui tu verras l'Esprit descendre et se reposer, c'est lui qui baptise dans l'Esprit-Saint.
34 Mimi mwenyewe nimeona jambo hili na ninashuhudia kuwa huyu ndiye Mwana wa Mungu.”
Et moi j'ai vu et j'ai rendu témoignage que celui-là est le Fils de Dieu. "
35 Siku iliyofuata, Yohana alikuwa huko tena pamoja na wanafunzi wake wawili.
Le lendemain, Jean se trouvait encore là, avec deux de ses disciples.
36 Alipomwona Yesu akipita, akasema, “Tazama, Mwana-Kondoo wa Mungu!”
Et ayant regardé Jésus qui passait, il dit: " Voici l'Agneau de Dieu. "
37 Wale wanafunzi wawili walipomsikia Yohana akisema haya, wakamfuata Yesu.
Les deux disciples l'entendirent parler, et ils suivirent Jésus.
38 Yesu akageuka, akawaona wakimfuata akawauliza, “Mnataka nini?” Wakamwambia, “Rabi,” (maana yake Mwalimu), “Unaishi wapi?”
Jésus s'étant retourné, et voyant qu'ils le suivaient, leur dit: " Que cherchez-vous? " Ils lui répondirent: " Rabbi (ce qui signifie Maître), où demeurez-vous? "
39 Yesu akawajibu, “Njooni, nanyi mtapaona!” Hivyo wakaenda na kupaona mahali alipokuwa anaishi, wakakaa naye siku ile, kwa kuwa ilikuwa yapata saa kumi.
Il leur dit: " Venez et vous verrez. " Ils allèrent, et virent où il demeurait, et ils restèrent auprès de lui ce jour-là. Or, c'était environ la dixième heure.
40 Andrea nduguye Simoni Petro, alikuwa mmoja wa wale wawili waliosikia yale Yohana aliyokuwa amesema, naye ndiye alimfuata Yesu.
Or, André, le frère de Simon-Pierre, était l'un des deux qui avaient entendu la parole de Jean, et qui avaient suivi Jésus.
41 Kitu cha kwanza Andrea alichofanya ni kumtafuta Simoni nduguye na kumwambia, “Tumemwona Masiya” (yaani, Kristo).
Il rencontra d'abord son frère Simon, et lui dit: " Nous avons trouvé le Messie (ce qui se traduit Christ). "
42 Naye akamleta kwa Yesu. Yesu akamwangalia na kusema, “Wewe ni Simoni mwana wa Yohana. Utaitwa Kefa” (ambalo limetafsiriwa Petro).
Et il l'amena à Jésus. Jésus, l'ayant regardé dit: " Toi, tu es Simon, fils de Jean; tu seras appelé Céphas (ce qui se traduit Pierre). "
43 Siku iliyofuata Yesu aliamua kwenda Galilaya. Akamkuta Filipo, akamwambia, “Nifuate.”
Le jour suivant, Jésus résolut d'aller en Galilée. Et il rencontra Philippe. Et Jésus lui dit: " Suis-moi. "
44 Basi Filipo alikuwa mwenyeji wa Bethsaida, mji alikotoka Andrea na Petro.
Philippe était de Bethsaïde, la ville d'André et de Pierre.
45 Filipo naye akamkuta Nathanaeli na kumwambia, “Tumemwona yeye ambaye Mose aliandika habari zake katika Sheria na ambaye pia manabii waliandika kumhusu, yaani, Yesu wa Nazareti, mwana wa Yosefu.”
Philippe rencontra Nathanaël et lui dit: " Nous avons trouvé celui dont Moïse a écrit dans la Loi, ainsi que les Prophètes: c'est Jésus, fils de Joseph de Nazareth. "
46 Nathanaeli akauliza, “Nazareti! Je, kitu chochote chema chaweza kutoka Nazareti?” Filipo akamwambia, “Njoo uone.”
Nathanaël lui répondit: " Peut-il sortir de Nazareth quelque chose de bon? " Philippe lui dit: " Viens et vois. "
47 Yesu alipomwona Nathanaeli anakaribia, akanena habari zake akasema, “Tazama huyu ni Mwisraeli kweli kweli; hana hila ndani yake.”
Jésus vit venir vers lui Nathanaël, et dit en parlant de lui: " Voici vraiment un Israélite, en qui il n'y a nul artifice. "
48 Nathanaeli akamuuliza, “Umenifahamuje?” Yesu akamjibu, “Nilikuona ulipokuwa bado uko chini ya mtini, kabla hata Filipo hajakuita.”
Nathanaël lui dit: " D'où me connaissez-vous? " Jésus repartit et lui dit: " Avant que Philippe t'appelât, lorsque tu étais sous le figuier, je t'ai vu. "
49 Nathanaeli akamwambia, “Rabi, wewe ni Mwana wa Mungu! Wewe ni Mfalme wa Israeli!”
Nathanaël lui répondit: " Rabbi, vous êtes le Fils de Dieu, vous êtes le Roi d'Israël. "
50 Yesu akamwambia, “Unaamini kwa kuwa nilikuambia nilikuona ulipokuwa bado uko chini ya mtini? Basi utaona mambo makuu zaidi kuliko hilo.”
Jésus lui repartit: " Parce que je t'ai dit: Je t'ai vu sous le figuier, tu crois! Tu verras de plus grandes choses que celle-là. "
51 Ndipo akawaambia, “Amin, amin nawaambia, ninyi mtaona mbingu ikifunguka na malaika wa Mungu wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Adamu.”
Et il ajouta: " En vérité, en vérité, je vous le dis, vous verrez désormais le ciel ouvert, et les anges de Dieu montant et descendant sur le Fils de l'homme. "

< Yohana 1 >