< Yohana 2 >

1 Siku ya tatu kulikuwa na arusi katika mji wa Kana ya Galilaya, naye mama yake Yesu alikuwepo pale.
Et le troisième jour, il se fit des noces à Cana en Galilée; et la mère de Jésus y était.
2 Yesu pamoja na wanafunzi wake walikuwa wamealikwa arusini pia.
Jésus fut aussi convié aux noces avec ses disciples.
3 Divai ilipokwisha, mama yake Yesu akamwambia, “Wameishiwa na divai.”
Le vin étant venu à manquer, la mère de Jésus lui dit: " Ils n'ont point de vin. "
4 Yesu akamwambia, “Mwanamke, nina nini nawe? Saa yangu haijawadia.”
Jésus lui répondit: " Femme, qu'est-ce que cela pour moi et vous? Mon heure n'est pas encore venue. "
5 Mama yake akawaambia wale watumishi, “Lolote atakalowaambia, fanyeni.”
Sa mère dit aux serviteurs: " Faites tout ce qu'il vous dira. "
6 Basi ilikuwepo mitungi sita ya kuhifadhia maji iliyotengenezwa kwa mawe kwa ajili ya kujitakasa kwa desturi ya Kiyahudi; kila mtungi ungeweza kuchukua vipipa viwili au vitatu.
Or, il y avait là six urnes de pierre destinées aux ablutions des Juifs, et contenant chacune deux ou trois mesures.
7 Yesu akawaambia wale watumishi, “Ijazeni hiyo mitungi maji.” Nao wakaijaza ile mitungi mpaka juu.
Jésus leur dit: " Remplissez d'eau ces urnes. " Et ils les remplirent jusqu'au haut.
8 Kisha akawaambia, “Sasa choteni hayo maji kidogo, mpelekeeni mkuu wa meza.” Hivyo wakachota, wakampelekea.
Et il leur dit: " Puisez maintenant, et portez-en au maître du festin; " et ils en portèrent.
9 Yule mkuu wa meza akayaonja yale maji ambayo yalikuwa yamebadilika kuwa divai. Hakujua divai hiyo ilikotoka ingawa wale watumishi waliochota yale maji wao walifahamu. Basi akamwita bwana arusi kando
Dès que le maître du festin eut goûté l'eau changée en vin (il ne savait pas d'où venait ce vin, mais les serviteurs qui avaient puisé l'eau le savaient), il interpella l'époux,
10 akamwambia, “Watu wote hutoa kwanza divai nzuri, kisha huleta ile divai hafifu wageni wakisha kunywa vya kutosha, lakini wewe umeiweka ile nzuri kupita zote mpaka sasa.”
et lui dit: " Tout homme sert d'abord le bon vin, et, après qu'on a bu abondamment, le moins bon; mais toi, tu as gardé le bon jusqu'à ce moment. " —
11 Huu, ndio uliokuwa muujiza wa kwanza Yesu aliofanya Kana ya Galilaya. Hivyo Yesu alidhihirisha utukufu wake, nao wanafunzi wake wakamwamini.
Tel fut, à Cana de Galilée, le premier des miracles que fit Jésus, et il manifesta sa gloire, et ses disciples crurent en lui.
12 Baada ya hayo, Yesu pamoja na mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake, walishuka mpaka Kapernaumu, wakakaa huko siku chache.
Après cela, il descendit à Capharnaüm avec sa mère, ses frères et ses disciples, et ils n'y demeurèrent que peu de jours.
13 Ilipokaribia wakati wa Pasaka ya Wayahudi, Yesu alipanda kwenda Yerusalemu.
Or la Pâque des Juifs était proche, et Jésus monta à Jérusalem.
14 Huko Hekaluni aliwakuta watu wakiuza ngʼombe, kondoo na njiwa, nao wengine walikuwa wameketi mezani wakibadili fedha.
Il trouva dans le temple les marchands de bœufs, de brebis, et de colombes, et les changeurs assis.
15 Akatengeneza mjeledi kutokana na kamba, akawafukuza wote kutoka kwenye eneo la Hekalu, pamoja na kondoo na ngʼombe. Akazipindua meza za wale wabadili fedha na kuzimwaga fedha zao.
Et ayant fait un petit fouet avec des cordes, il les chassa tous du temple, avec les brebis et les bœufs; il jeta par terre l'argent des changeurs, et renversa leurs tables.
16 Akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa, “Waondoeni hapa! Mnathubutuje kuifanya nyumba ya Baba yangu kuwa mahali pa biashara?”
Et il dit aux vendeurs de colombes: " Enlevez cela d'ici; ne faites pas de la maison de mon Père une maison de trafic. "
17 Wanafunzi wake wakakumbuka kuwa imeandikwa: “Wivu wa nyumba yako utanila.”
Les disciples se ressouvinrent alors qu'il est écrit: " Le zèle de votre maison me dévore. "
18 Ndipo Wayahudi wakamuuliza, “Unaweza kutuonyesha ishara gani ili kuthibitisha mamlaka uliyo nayo ya kufanya mambo haya?”
Les Juifs prenant la parole lui dirent: " Quel signe nous montrez-vous, pour agir de la sorte? "
19 Yesu akawajibu, “Libomoeni hili Hekalu, nami nitalijenga tena kwa siku tatu!”
Jésus leur répondit: " Détruisez ce temple et je le relèverai en trois jours. "
20 Wale Wayahudi wakamjibu, “Hekalu hili lilijengwa kwa muda wa miaka arobaini na sita, nawe wasema utalijenga kwa siku tatu?”
Les Juifs repartirent: " C'est en quarante-six ans que ce temple a été bâti, et vous, en trois jours vous le relèverez! "
21 Lakini yeye Hekalu alilozungumzia ni mwili wake.
Mais lui, il parlait du temple de son corps.
22 Baada ya kufufuliwa kutoka kwa wafu, wanafunzi wake wakakumbuka yale aliyokuwa amesema. Ndipo wakayaamini Maandiko na yale maneno Yesu aliyokuwa amesema.
Lors donc qu'il fut ressuscité d'entre les morts, ses disciples se souvinrent qu'il avait dit cela, et ils crurent à l'Ecriture et à la parole que Jésus avait dite.
23 Ikawa Yesu alipokuwa Yerusalemu kwenye Sikukuu ya Pasaka, watu wengi waliona ishara na miujiza aliyokuwa akifanya, wakaamini katika jina lake.
Pendant que Jésus était à Jérusalem, à la fête de Pâque, beaucoup voyant les miracles qu'il faisait, crurent en son nom.
24 Lakini Yesu hakujiaminisha kwao kwa sababu aliwajua wanadamu wote.
Mais Jésus ne se fiait point à eux, parce qu'il les connaissait tous,
25 Hakuhitaji ushuhuda wa mtu yeyote kuhusu mtu, kwa kuwa alijua yote yaliyokuwa moyoni mwa mtu.
et qu'il n'avait pas besoin qu'on lui rendit témoignage d'aucun homme; car il savait, lui, ce qu'il y avait dans l'homme.

< Yohana 2 >