< Yohana 16 >

1 “Nimewaambia mambo haya yote ili msije mkaiacha imani.
"These things I have spoken to you in order to clear stumbling-blocks out of your path.
2 Watawatenga na masinagogi. Naam, saa yaja ambayo mtu yeyote atakayewaua atadhani kwa kufanya hivyo anamtumikia Mungu.
You will be excluded from the synagogues; nay more, the time is coming when any one who has murdered one of you will suppose he is offering service to God.
3 Nao watawatenda haya kwa sababu hawamjui Baba wala mimi.
And they will do these things because they have failed to recognize the Father and to discover who I am.
4 Lakini nimewaambia ninyi mambo haya, ili saa hiyo ikiwadia mpate kukumbuka ya kuwa nilikuwa nimewaambia. Sikuwaambia mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.
But I have spoken these things to you in order that when the time for their accomplishment comes you may remember them, and may recollect that I told you. I did not, however, tell you all this at first, because I was still with you.
5 “Sasa mimi ninakwenda kwake yeye aliyenituma, lakini hakuna hata aniulizaye, ‘Unakwenda wapi?’
But now I an returning to Him who sent me; and not one of you asks me where I am going.
6 Kwa sababu nimewaambia mambo haya, mioyo yenu imejawa na huzuni.
But grief has filled your hearts because I have said all this to you.
7 Lakini nawaambia kweli, yafaa mimi niondoke, kwa kuwa nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu, lakini nikienda nitamtuma kwenu.
"Yet it is the truth that I am telling you--it is to your advantage that I go away. For unless I go away, the Advocate will not come to you; but if I go, I will send Him to you.
8 Naye atakapokuja, atauthibitishia ulimwengu kuhusu dhambi, haki na hukumu.
And He, when He comes, will convict the world in respect of sin, of righteousness, and of judgement; --
9 Kwa habari ya dhambi, kwa sababu hawaniamini mimi,
of sin, because they do not believe in me;
10 kwa habari ya haki, kwa sababu ninakwenda kwa Baba, nanyi hamtaniona tena,
of righteousness, because I am going to the Father, and you will no longer see me;
11 kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa.
of judgement, because the Prince of this world is under sentence.
12 “Bado ninayo mambo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili sasa.
"I have much more to say to you, but you are unable at present to bear the burden of it.
13 Atakapokuja huyo Roho wa kweli atawaongoza awatie katika kweli yote. Yeye hatanena kwa ajili yake mwenyewe, bali atanena yale yote atakayosikia, naye atawaonyesha mambo yajayo.
But when He has come--the Spirit of Truth--He will guide you into all the truth. For He will not speak as Himself originating what He says, but all that He hears He will speak, and He will make known the future to you.
14 Atanitukuza mimi, kwa maana atayachukua yaliyo yangu na kuwajulisha ninyi.
He will glorify me, because He will take of what is mine and will make it known to you.
15 Vyote alivyo navyo Baba ni vyangu. Ndiyo maana nimesema Roho atachukua yaliyo yangu na kuwajulisha ninyi.
Everything that the Father has is mine; that is why I said that the Spirit of Truth takes of what is mine and will make it known to you.
16 “Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona.”
"A little while and you see me no more, and again a little while and you shall see me."
17 Baadhi ya wanafunzi wakaulizana, “Ana maana gani asemapo, ‘Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona’? Naye ana maana gani asemapo, ‘Kwa sababu ninakwenda kwa Baba’?”
Some of His disciples therefore said to one another, "What does this mean which He is telling us, 'A little while and you do not see me, and again a little while and you shall see me,' and 'Because I am going to the Father'?"
18 Wakaendelea kuulizana, “Ana maana gani asemapo, ‘Kitambo kidogo’? Hatuelewi hilo analosema.”
So they asked one another repeatedly, "What can that 'little while' mean which He speaks of? We do not understand His words."
19 Yesu akatambua kuwa walitaka kumuuliza juu ya hilo, hivyo akawaambia, “Je, mnaulizana nina maana gani niliposema, ‘Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona’?
Jesus perceived that they wanted to ask Him, and He said, "Is this what you are questioning one another about--my saying, 'A little while and you do not see me, and again a little while and you shall see me'?
20 Amin, amin nawaambia, ninyi mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utafurahi. Ninyi mtahuzunika, lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.
In most solemn truth I tell you that you will weep aloud and lament, but the world will be glad. You will mourn, but your grief will be turned into gladness.
21 Mwanamke anapokuwa na utungu wa kuzaa huwa na maumivu kwa sababu saa yake imewadia. Lakini mtoto akiisha kuzaliwa, yule mwanamke husahau maumivu hayo kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa mtoto ulimwenguni.
A woman, when she is in labour, has sorrow, because her time has come. But when she has given birth to the babe, she no longer remembers the pain, because of her joy at a child being born into the world.
22 Hivyo ninyi mna maumivu sasa, lakini nitawaona tena, nayo mioyo yenu itafurahi na furaha yenu hakuna awaondoleaye.
So you also now have sorrow; but I shall see you again, and your hearts will be glad, and your gladness no one will take away from you.
23 Katika siku hiyo hamtaniuliza neno lolote. Amin, amin nawaambia, kama mkimwomba Baba jambo lolote kwa jina langu, yeye atawapa.
You will put no questions to me then. "In most solemn truth I tell you that whatever you ask the Father for in my name He will give you.
24 Mpaka sasa hamjaomba jambo lolote kwa Jina langu. Ombeni nanyi mtapewa, ili furaha yenu ipate kuwa kamili.
As yet you have not asked for anything in my name: ask, and you shall receive, that your hearts may be filled with gladness.
25 “Nimewaambia mambo haya kwa mafumbo. Saa yaja ambapo sitazungumza nanyi tena kwa mafumbo bali nitawaeleza waziwazi kuhusu Baba.
"All this I have spoken to you in veiled language. The time is coming when I shall no longer speak to you in veiled language, but will tell you about the Father in plain words.
26 Siku hiyo mtaomba kwa Jina langu. Wala sitawaambia kwamba nitamwomba Baba kwa ajili yenu,
At that time you will make your requests in my name; and I do not promise to ask the Father on your behalf,
27 kwa maana Baba mwenyewe anawapenda, kwa sababu mmenipenda mimi na mmeamini kwamba nimetoka kwa Mungu.
for the Father Himself holds you dear, because you have held me dear and have believed that I came from the Father's presence.
28 Nilitoka kwa Baba na kuja ulimwenguni, sasa naondoka ulimwenguni na kurudi kwa Baba.”
I came from the Father and have come into the world. Again I am leaving the world and am going to the Father."
29 Ndipo wanafunzi wake wakasema, “Sasa unazungumza waziwazi, wala si kwa mafumbo.
"Ah, now you are using plain language," said His disciples, "and are uttering no figure of speech!
30 Sasa tumejua kwamba wewe unajua mambo yote, wala hakuna haja ya mtu kukuuliza maswali. Kwa jambo hili tunaamini kwamba ulitoka kwa Mungu.”
Now we know that you have all knowledge, and do not need to be pressed with questions. Through this we believe that you came from God."
31 Yesu akawajibu, “Je, sasa mnaamini?
"Do you at last believe?" replied Jesus.
32 Saa inakuja, naam, imekwisha kuwadia, mtakapotawanyika kila mmoja kwenda nyumbani kwake na kuniacha peke yangu. Lakini mimi siko peke yangu kwa sababu Baba yu pamoja nami.
"Remember that the time is coming, nay, has already come, for you all to be dispersed each to his own home and to leave me alone. And yet I am not alone, for the Father is with me.
33 Nimewaambia mambo haya, ili mpate kuwa na amani mkiwa ndani yangu. Ulimwenguni mtapata dhiki. Lakini jipeni moyo, kwa maana mimi nimeushinda ulimwengu.”
"I have spoken all this to you in order that in me you may have peace. In the world you have affliction. But keep up your courage: I have won the victory over the world."

< Yohana 16 >